Nakubaliana na Marekani na NATO kuvamia nchi mbalimbali duniani

Nakubaliana na Marekani na NATO kuvamia nchi mbalimbali duniani

cutelove

JF-Expert Member
Joined
Oct 3, 2017
Posts
3,448
Reaction score
7,972
Wakati vita ikishika kasi kule Ukraine dhidi ya Putin ,nashangaa baadhi ya watu kwenye majukwaa ya mitandao ya kijamii wakimuunga mkono kuivamia Ukraine na inasikitisha sana badala ya kukemea

Wengi hutetea uvamizi wa USA na NATO kwenye mataifa mbalimbali duniani ikiwemo Libya ,Iraq nk

Ukweli ni kuwa uvamizi unaokuwa unafanywa na NATO na USA huwa ni wa halali kabisa,ukiangalia nchi zilizowahi kuvamiwa kote kuna migogoro ya kisiasa na kijamii ndani ya nchi hizo ,na mbaya zaidi kuna makundi kwenye nchi hizo huwa yanapata mateso ya kibinadamu yamekithiri na kupindukia haki za binadamu na kuhatarisha usalama wa kikanda na kidunia kwa ujumla

Na kama unasema huwa wanawaonea, kwa nini USA na NATO wakisha vamia wanakaribishwa na wananchi kwa vigelegele na nderemo na magari ya kijeshi yanatandikiwa nguo yapite juu kwa heshima?

Wapi USA na NATO wamewahi kuvamia wananchi wakashirikiana na jeshi la nchi yao kuwapiga au kuweka upinzani wa uvamizi?

Twende Ukraine, Moscow anamvamia Ukraine ,nchi inakuwa moja na kwa hamasa ambayo inatia machozi ya huruma na furaha na maajabu ambayo hujawahi kuyaona kwenye uvamizi wa USA na NATO

Hakuna mwananchi hata mmoja wa Ukraine ambaye amesema hatumtaki Rais wao ,hakuna hakuna ,hakuna na hakuna tena

Nchi ya Ukraine imekuwa moja tuache yale majimbo yanayotaka kujitenga lakini miji mikubwa ya Ukraine imeshindikana kutekwa,si watoto,wamama na wazee wanawapa wanajeshi wao moyo wa kupigania nchi yao ?

Cha msingi ni kwamba Putin hajui na hana sababu ya kuivamia Ukraine, na siku zake hapa duniani zinahesabika angalia sasa dunia inavyomtenga kwa kila nyanja ,ushujaa wake unaanza kufifia kama mshumaa

Putin ni mtu katili duniani hapaswi kuigwa na mtu yeyote,yaani imefikia muda sasa unapangiwa namna ya kuishi na nyie ni Taifa huru,Kuna siku Kenya itajiunga na NATO halafu Tanzania tuivamie Kenya kwamba kwa nini anajiunga na NATO, huu ndo upumbavu wa standard gauge
 
Wakati vita ikishika kasi kule Ukraine dhidi ya Putin ,nashangaa baadhi ya watu kwenye majukwaa ya mitandao ya kijamii wakimuunga mkono kuivamia Ukraine na inasikitisha sana badala ya kukemea...
Nakumbusha kwamba Crimea ilikuwa Ukraine kule wakaamza harakati za kujitenga na majimbo mawili aliyochukua majuzi Russia.

Nakutaka tena nenda youtube nafikiri inakuwepo taarifa ya habari ya leo asbh ambayo imetokewa na BBC wakiwahoji wale watalii waliokwama Zanzibar hapo utawasikia wamesema nini juu ya Rais wao wasasa
 
Nakumbusha kwamba Crimea ilikuwa Ukraine kule wakaamza harakati za kujitenga na majimbo mawili aliyochukua majuzi Russia.

Nakutaka tena nenda youtube nafikiri inakuwepo taarifa ya habari ya leo asbh ambayo imetokewa na BBC wakiwahoji wale watalii waliokwama Zanzibar hapo utawasikia wamesema nini juu ya Rais wao wasasa

Sent using Jamii Forums mobile app
Wengi wetu tupo brain washed na western propaganda
 
Futa ulichoandika kama huelewi kitu

Hakuna taifa lenye ushetan lililoutenda kama USA+ NATO hawa jawafai hata kushabikiwa, ni vile tu misaada yao imewalemaza na kuwaona wao Miungu watu, media zisikudanganye kijana hujui lolote wew kazana kuombea nchi yako isifike huko.
1646044062736.jpg
 
Futa ulichoandika kama huelewi kitu

Hakuna taifa lenye ushetan lililoutenda kama USA+ NATO hawa jawafai hata kushabikiwa, ni vile tu misaada yao imewalemaza na kuwaona wao Miungu watu, media zisikudanganye kijana hujui lolote wew kazana kuombea nchi yako isifike huko.View attachment 2134435
“This is not Russia’s war. This is a military crime by an unelected, unaccountable, authoritarian, and frankly increasingly deranged dictator.”
 
Umeandika mambo mazito kwa vijana wadogo
Vijana siku hizi hawataki kusoma. Uchambuzi wao wanautoa kwa kuangalia BBC, CNN, FOX NEWS, SKY NEWS, MSNBC, DW-TV n.k

Akimaliza hapo anajiona amemaliza kila kitu na matokeo yake ndiyo kama haya anahalalisha yaliyofanywa na US na NATO. Ukiwaambia bado kuna picha unapaswa uione tena, jawabu lao ni msemo unaosema "umeandika porojo".
 
Back
Top Bottom