Nakubaliana na mchungaji Msigwa kuwa level of thinking Tanzania imeshuka

Nakubaliana na mchungaji Msigwa kuwa level of thinking Tanzania imeshuka

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Kuna clip iko kwenye mitandao ikionyesha mahojiano aliyofanyiwa mchungu Msigwa na Darmpya tv, ambapo mchungaji Msigwa anasikika akiongelea swala la critical thinking.

Msigwa anasikika akisema, wakati wa Mwalimu, vijana wa chuo kikuu walikuwa na uhuru wa kusema chochote wawapo maeneo ya chuo na walikuwa na kinga ila kinga hiyo ilikuja ondolewa enzi za Mwinyi baada ya wanafunzi wa chuo kikuu wakati huo kumkosoa mzee Mwinyi.

Kwa maelezo yake, Msigwa anasema Mwalimu aliruhusu mijadala vyuo vikuu na kwamba vyuoni ni sehemu ambapo watu wana-think critically tofauti na sasa ambapo wanafunzi wa vyuo vikuu hawawezi hata kuuuliza maswali ya how,why, n.k.

Msigwa amesema wanafunzi hawa sio wa kulaumiwa kwani hata walimu wao nao hawa-think critically huku akitaja kutishwa kuwa ni moja ya sababu ya walimu wao kuwa hivyo.

Msigwa anahoji kama ma-proffesor wetu wanaka chini na kuumiza vichwa kuhusu hatima ya Tanzania yetu kiuchumi, n.k katika miaka 30 ijayo huku akitoltea mfano wa nchi kama Israel ambayo inauza "brain" duniani na wamarekani wanaowaza nishati mbadala ya mafuta kwa miaka 30 ijayo.

Kwa mfano, Msigwa anahoji tumejiandaa vipi kuacha kuitegema bandari kama chanzo cha mapato ikitokea miaka ya mbeleni zinabuniwa ndege kubwa zinazoweza kubeba mizigo mikubwa na kwa gharama nafuu kutokana na kukua kwa teknolojia akitolea mfano wa wamarekani wanaowaza/wanaobuni nishati mbadala ya mafuta ikitokea mafuta yanatoweka duniani.

Msigwa kaongea mengi yanayoeleza ni jinsi gani watanzania wa leo hatuwazi critically.

Binafsi naungana na Msigwa kwasababu moja kubwa: Watanzania wa leo hii sehemu kubwa ya mijadala yetu mitandaoni ni kujadili matukio, maandiko na kauli au matamshi ya watu maarufu (wanasiasa, wasanii, n.k)yanayopatikana mitandaoni na kwenye vyombo vya habari na sio kujadili au kubuni mambo yanaweza kuleta suluhu ya matatizo yetu kama nchi.

Kwa maneno mengine,tunatumua muda mwingi au niseme interest zetu ni kulalamikia matatizo tuliyonayo huku tukitumia muda mchache kuandika, kujadili na kupendekeza solution za matatizo yetu, tunasahau matukio yanakuja na kupita, wakati matatizo yetu yako pale pale huku watawala nao wakiwa hawana solution ya baadhi ya matatizo tuliyonayo.

Kama anavyosema Msigwa, kwa sasa hatuna mijadala sababu mojawapo likiwa ni uoga lakini pia kwa sasa level yetu ya ku-think critically imeshuka.

Kwenye mitandao kwa sasa, mtu aki- post habari kuhusu tukio fulani au kauli ya mwanasiasa fulani, watu wanakuwa interested sana kujadili ila mtu akija na idea kuhusu namna gani tunaweza kutatua tatizo fulani katika jamii na nchi kwa ujumla, mijadala huwa ni ya kiwango cha chini sana(wa kukosoa na kuungana mkono ni wachache mno).

Kwa mfano, hivi sasa watanzania tunatakiwa tuwe na mjadala utakaosaidia kupatikana kwa vyanzo vipya vya mapato, ila hilo alipo, badala yake tunalalamika kukamuliwa kodi huku TRA nao wakiwa wameishiwa ubunifu wa kupata vyanzo vipya vya mapato na matokeo sasa wanatuhumiwa kutoza kodi kubwa inayoua mitaji ya wafanyabiashara(hakuna mwenye solution juu ya vyanzo vipya vya mapato badala yake wote tunalalamika!)

Mimi naamini vyanzo vya mapato nchi bado viko vingi tu, tatizo ni watu kushindwa kukaa chini na kuumiza vichwa ikiwa ni pamoja na kushirikishi wananchi na wataalumu katika mijadala ya pamoja yenye lengo la kubuni vyanzo vipya vya mapato.

Hata mnapoona wasomi na wanaoitwa wataalamu wanakimbilia kwenye siasa, mjue kweli level of thinking imeshuka, hivyo wanashindwa kutumia elimu zao kujiongezea vipato halafu mkabaki mnategemea watu wa aina hiyo ndio wawaletee maendeleo.Kama mnaamini hivyo, mjue tu huko ni kujidanganya mchana kweupe.

Watanzania tubadilike, dunia inatuacha nyuma.
 
Tunawasubir Hao kina msigwa wataalam wa kufikir wafikirie kivip kina halima mdee na na wenzake kwa nn wataendelea kua wabunge na watabaki kua wanachama wa chadema!?
 
Tunawasubir Hao kina msigwa wataalam wa kufikir wafikirie kivip kina halima mdee na na wenzake kwa nn wataendelea kua wabunge na watabaki kua wanachama wa chadema!?
Mwisho wa kuwaza kwako, research ya Msigwa isha pita,
 
Binafsi naona kuna sababu zinazosababisha hilo tatizo kukua, kama ulivyosema mojawapo ni hiyo ya ushabiki wa vyama vya siasa, mtu akiwa upande mmoja anaona rahisi kushambulia upande wa pili kwa sababu nyepesi tu za kijinga, bila kufikiria mada iliyopo mezani, mfano wa hili angalia wanaoiponda mada yako hapo juu, badala ya kuendeleza ulipoishia wengi wamemgeukia Msigwa personally, small minded.

Lakini pia, ukiondoa aina ya utawala tulionao hivi sasa ambao unawafunga midomo wakosoaji, tujiulize hivi ni wangapi kati yetu wenye huo uwezo wa kukosoa critically kama unavyosema badala ya kukosoa kwa lugha zisizofaa? ukweli ni wachache.

Hili limesababishwa kwa kiasi kikubwa na aina ya wasomi wetu wanaozalishwa na vyuo vyetu hapa ndani, wengi wana graduate kwa kukariri madesa, sasa unategemea vipi mtu wa aina hii awe na uwezo wa criticize kwa kujenga hoja zenye ushawishi wa kutosha zinazoambatana na mifano ili kumshawishi wa upande wa pili? hili nalo ni tatizo.

Lakini la tatu na mwisho, nikichukulia mfano huku jf, wengi wetu hawapo tayari kujifunza, huku kila mtu ni mjuaji hata kama kiukweli hajui, mtu yupo tayari kubisha tu the whole day ilimradi asionekane kawa defeated na mwenzake, hili linasababisha kudumaza uelewa wa mtu kwasababu huyu mtu kama hayuko tayari kuingiza kitu kipya kichwani mwake basi ataendelea kukua kiumri tu, lakini kiakili atabaki palepale, matokeo yake his level of thinking nayo itadumaa.

Lazima tujue kwamba hakuna mtu anaezaliwa anajua kila kitu, uwezo wa mtu kiakili unaongezeka kwa kusoma vitabu, na kuwa tayari kujifunza kwa wengine pale ambapo utaona uwezo wako kwenye jambo husika ni mdogo (na hili sio kosa ndio ustaarabu wenyewe).
 
Korea kaskazini hawana uhuru wa kutukana Kama huku ila wako juu kila Kona hasa teknolojia.
 
Insanity is keep doing the same then expect different results?
 
" You are going to come across people in your life who will say the right words at all the right times. But in the ends, it's always their actions you should judge with them by. It's actions not words that matter"
 
naunga mkono hoja kuhusu watanzania wengi kushughulika na vitu vidogo. mfano wangu upo humuhumu jf kwa 'great thinkers', nilikuja na thread fikirishi kabisa inayohusu haja ya kuajiri walimu wa kike kuanzia miaka 35 badala ya hii 18,19,20....25. mada ilichangiwa na wadau wachache sana huku nikipata kiji'like' kimoja tu. katika hao wachacheee waliochangia, asilimia 98 waliishia kunitukana tu....tena wengine matusi ya nguoni. 😵😵

ajabu ni kuwa threads za kidukulilo za kumiliki visiwa sehemu mbali mbali duniani na magari ya kifahari zaidi ya ronaldo na messi zinapata ma'likes' na 'replies' nyingi ajabu.

kitu kingine nilichogundua humu ambacho kinaendana na ulichoandika mtoa mada ni kuwa hata humu, kwa ma'great thinkers', mada huangaliwa kwanza imetoka kwa nani ili ajibiwe au isomwe......kama hauna jina humu si ajabu mada zako hata kufunguliwa zisifunguliwe. ni dalili tosha ya ulichokisema.....tatizo la kukosa critical thinking limetuvamia hadi humu.
 
naunga mkono hoja kuhusu watanzania wengi kushughulika na vitu vidogo. mfano wangu upo humuhumu jf kwa 'great thinkers', nilikuja na thread fikirishi kabisa inayohusu haja ya kuajiri walimu wa kike kuanzia miaka 35 badala ya hii 18,19,20....25. mada ilichangiwa na wadau wachache sana huku nikipata kiji'like' kimoja tu. katika hao wachacheee waliochangia, asilimia 98 waliishia kunitukana tu....tena wengine matusi ya nguoni. 😵😵

ajabu ni kuwa threads za kidukulilo za kumiliki visiwa sehemu mbali mbali duniani na magari ya kifahari zaidi ya ronaldo na messi zinapata ma'likes' na 'replies' nyingi ajabu.

kitu kingine nilichogundua humu ambacho kinaendana na ulichoandika mtoa mada ni kuwa hata humu, kwa ma'great thinkers', mada huangaliwa kwanza imetoka kwa nani ili ajibiwe au isomwe......kama hauna jina humu si ajabu mada zako hata kufunguliwa zisifunguliwe. ni dalili tosha ya ulichokisema.....tatizo la kukosa critical thinking limetuvamia hadi humu.
Nimecheka Sana...Mimi sikuiona Mkuu...ulikuwa Mwaka Jana au lini?
 
naunga mkono hoja kuhusu watanzania wengi kushughulika na vitu vidogo. mfano wangu upo humuhumu jf kwa 'great thinkers', nilikuja na thread fikirishi kabisa inayohusu haja ya kuajiri walimu wa kike kuanzia miaka 35 badala ya hii 18,19,20....25. mada ilichangiwa na wadau wachache sana huku nikipata kiji'like' kimoja tu. katika hao wachacheee waliochangia, asilimia 98 waliishia kunitukana tu....tena wengine matusi ya nguoni. 😵😵

ajabu ni kuwa threads za kidukulilo za kumiliki visiwa sehemu mbali mbali duniani na magari ya kifahari zaidi ya ronaldo na messi zinapata ma'likes' na 'replies' nyingi ajabu.

kitu kingine nilichogundua humu ambacho kinaendana na ulichoandika mtoa mada ni kuwa hata humu, kwa ma'great thinkers', mada huangaliwa kwanza imetoka kwa nani ili ajibiwe au isomwe......kama hauna jina humu si ajabu mada zako hata kufunguliwa zisifunguliwe. ni dalili tosha ya ulichokisema.....tatizo la kukosa critical thinking limetuvamia hadi humu.
UMEONGEA vyema ndugu...kuna tatizo humu jf kama viongozi wa jf wasipofanya marekebisho mapema kuna hatihati ya hii platform kuja kufa japo siombei iwe hivyo. Kuna wadau wanaoleta mada fikirishi sana kiasi kwamba ukikaa chini ukaichambua ina mantiki ila ndio hivyo wengi wetu humu tunapenda mada za ngono,umbea n.k ndizo zinapewa kipaumbele sana ..kwa mfano leo Kuna member kaleta mada humu ikisema kwamba kwanini mkuu wa nchi(rais) kwenye mitandao ya kijamii hususan Twitter watu wana chuki naye hususan kwenye lile swala la kupigiwa kura mtandaoni la kukuza demokrasia ,watu wanahimizana wasimpigie.lakini ghafla ule uzi ulifutwa haraka sana . nikitafakari nakosa jibu sana. Alichoongea msigwa kina tafakarisha sana kwa kweli.
 
naunga mkono hoja kuhusu watanzania wengi kushughulika na vitu vidogo. mfano wangu upo humuhumu jf kwa 'great thinkers', nilikuja na thread fikirishi kabisa inayohusu haja ya kuajiri walimu wa kike kuanzia miaka 35 badala ya hii 18,19,20....25. mada ilichangiwa na wadau wachache sana huku nikipata kiji'like' kimoja tu. katika hao wachacheee waliochangia, asilimia 98 waliishia kunitukana tu....tena wengine matusi ya nguoni. 😵😵

ajabu ni kuwa threads za kidukulilo za kumiliki visiwa sehemu mbali mbali duniani na magari ya kifahari zaidi ya ronaldo na messi zinapata ma'likes' na 'replies' nyingi ajabu.

kitu kingine nilichogundua humu ambacho kinaendana na ulichoandika mtoa mada ni kuwa hata humu, kwa ma'great thinkers', mada huangaliwa kwanza imetoka kwa nani ili ajibiwe au isomwe......kama hauna jina humu si ajabu mada zako hata kufunguliwa zisifunguliwe. ni dalili tosha ya ulichokisema.....tatizo la kukosa critical thinking limetuvamia hadi humu.
Kwenye mada yako ulikumbuka kusema hao walimu wenye miaka chini ya 35 wapelekwe wapi?

Au vyuo viache kuzalisha walimu wenye umri chini ya huo? kama vyuo vikiwazalisha mahitaji yao kimaisha (kula na mengine) watayapata kwa nani?

Inaonekana huo uzi wako ulikuwa na maswali mengi sana kuliko majibu.

N.B: Kama unataka mada yako usiejulikana ipate wachangiaji wengi sharti ihusu tukio lenye kuvuta hisia za watu, mfano; Ndugai kasema nini kuhusu Chadema, au Bunge limepitisha sheria gani ya ajabu, au viongozi gani wa upinzani kapatwa na jambo gani ( kufukuzwa uanachama n.k)

Lakini ukileta mada fikirishi wewe usiejulikana pole sana, hutapata wachangiaji wa kutosha, wenye hiyo privillege ni wachache kama Pasco sababu ya ukongwe wake humu jf.
 
UMEONGEA vyema ndugu...kuna tatizo humu jf kama viongozi wa jf wasipofanya marekebisho mapema kuna hatihati ya hii platform kuja kufa japo siombei iwe hivyo. Kuna wadau wanaoleta mada fikirishi sana kiasi kwamba ukikaa chini ukaichambua ina mantiki ila ndio hivyo wengi wetu humu tunapenda mada za ngono,umbea n.k ndizo zinapewa kipaumbele sana ..kwa mfano leo Kuna member kaleta mada humu ikisema kwamba kwanini mkuu wa nchi(rais) kwenye mitandao ya kijamii hususan Twitter watu wana chuki naye hususan kwenye lile swala la kupigiwa kura mtandaoni la kukuza demokrasia ,watu wanahimizana wasimpigie.lakini ghafla ule uzi ulifutwa haraka sana . nikitafakari nakosa jibu sana. Alichoongea msigwa kina tafakarisha sana kwa kweli.
Sababu ni Uoga, kupelekwa mahakamani kila siku imekuwa psychological defeat of a certain kind, hata kama unashinda kesi lakini bado hujiamini 100%
 
Back
Top Bottom