Nakuja Dar kusaka maisha! Treni ndio imeanza safari kutoka Kigoma kuja Dar, Mwenye kazi naomba tuwasiliane

Sawa bana Mpuuzi, wafikishie wapuuzi wenzako salamu waambie kulikoni tupo miaka 57 ya uhuru, lakini ukisafiri kutoka mwisho wa reli(Kigoma ujiji) kwenda Pwani/Dar es Salaam unachukua siku 3?
Badala ya kufuraia we unakosoa hapo unafanya utalii wa ndani wa kutosha na. Kama train ina kunguni inakupa nafasi ya kupata study mpya za maisha ungekuwa na haraka ungetumia usafiri mwingine

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa yote hayo, Ahsante!
 
Huko angeanza tuu na ufugaji wa kuku kwani huko chakula cha kuku kinapatikana kwa wingi.

Angefanya hivo angeweza hata kuwa anafuata sabuni pale sido anaenda kuzipanga mwandiga ama mjini?

Angefanya hivo angeweza kufuata mikungu ya ndizi hata miatono hapo manyovu kwa 6000 mpaka 7000 akifika mjini angeuza kwa bei ya leja leja.

Angefanya hivo angeweza kufuata sagaa pale kibilizi ama katonga na kuzileta mjini na akafunga kwenye vipakti

Angefanya hivo angeweza hata kufanya n.k nyiingi sana, huo mkoa ni full fursa aseee
Angeuza simu anayoitumia akaongezea kwenye nauli alolipa pamoja na malazi ya njiani ungekuwa mtaji tosha huko kwao kigoma angeanza kuchoma mahindi au kuuza karanga kukimbilia hapa mjini itamcost

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuyaandika hapa tu, ni rahisi sana!
 
Umeanza nyodo ukiwa njiani kwenda kusaka maisha dasalama hihihihi. Maisha yakigoma dasalama utarudi hapo hapo itigi kulima alizeti
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…