Namna makampuni makubwa ya kiteknolojia yanavyotumia mwanya huu kusahihisha kosa walilofanya miaka ya nyuma wakidhan wangezuia ushindani

Namna makampuni makubwa ya kiteknolojia yanavyotumia mwanya huu kusahihisha kosa walilofanya miaka ya nyuma wakidhan wangezuia ushindani

kali linux

JF-Expert Member
Joined
May 21, 2017
Posts
2,192
Reaction score
5,685
Hello bosses...

Tumesikia toka mwaka jana makampunj kama paypal, google, Meta(fb & insta owner), stripe, microsoft etc.... yakifukuza watu kwa kasi ya ajabu sana.

Leo hii tena mida hiihii nmepata taarifa kwamba Meta itafukuza tena wafanyakazi zaidi 10,000 baada ya round ya kwanza ya layoffs.

Lakini nmekua kwenye technology field kwa muda kiasi na nmefuatilia sana job market kwenye hii sector. Hio imefanya niweze kuona mambo kiutofauti kidogo na ambavyo yalivyo sababu kuna msemo unasema "Mambo yanavyoonekana mara nyingi sio yalivyo kiukweli"

Okay... let get to the point, kwanza kabisa ukiangalia makampun mengi yamefukuza watu kazi lkn toka yaanze data zinasema employment rate haijashuka inavyopaswa kuwa na bado payrolls ziko juu na zinazidi kukua, what does that mean? (Refer to NFP data toka waanze layoffs) Hio inamaanisha hawa wanaofukuzwa wanapata kazi sehemu nyingine papohapo, na hio kupata kazi tena inamaanisha wao wana ujuzi mzr na kazi zao na ukiongezea fact kwamba wamefanya kazi kwenye hayo makampuni makubwa ndipo utaona CV zao zinakua nzito.

Sasa kama umenielewa kwenye paragraph ya juu hapo utaona haya makampuni makubwa yaliajiri vichwa ili kupunguza competition. Ukiangalia kiundani kabisa pia utagundua products zao ni rahisi kutengenezeka alternative hivyo wakaanza program ya kuajiri watu wengi vichwa kwenye hio sector ili tu kuua product yako. Hawa jamaa walikua wakiona mna startup inatengeneza alternative solution kwa product yao basi aidha utapewa offer uajiriwa kwao au wanunue hio product yako then wanaiua polepole. Nliwahi kusoma makala fln jamaa ex-CEO na Founder wa insta ilibidi hadi akimbie kampuni lake sababu Meta (fb) kipindi kile ilikua inaipa insta resources chache sana, lengo lao mwanzo lilikua ni kuipa nguvu facebook.com kwa kuinyonya insta, yaan facebook.com iimeze insta lkn wakasoma mawimbi kwamba hilo haliwezekani, time waliopoteza huko ndipo ikawapa chance kampuni kama SNAPCHAT INC kuiyumbisha Meta kdg kwenye social media. Meta wakastuka baada ya kushindwa kununua snapchat ndipo wakaongeza nguvu kwa insta. Huo ni mfano tu lkn pia ni testimony ya huyo exCEO wa insta na alikua cofounder wa hio app(sorry nmesahau jina lake but u can google it) hio ilifanya jamaa akimbie kampuni yy mwenyewe aloianzisha.

Sasa haya makampuni hasahasa yaliopo kwenye sector ya search engines, payment apps, social media, na software dev yaliiga mbinu hio ili kuuwa competition/ushindani. Mfano mwingine ni Alphabet inc/Google. Hawa jamaa wanamakampuni zaidi ya miambili (200) baadhi wanayaua polepole mengi wameacquaire startups tu.

Sasa hio strategy ikafanya kuwe na wafanyakazi wengi lkn kazi chache, companies kama google na fb kuna muda zikawa na idlers wengi.

Na ndipo muda huu wanatumia hii chance kurekebisha mistake walofanya sababu imeonekana ni ngumu kuuwa ushindani kwa hio njia. Huku wakiweka kisingizio cha rising interest rates.

Kama bado haukubaliani na mimi kwa nini usijiulize mbona kampuni kama Apple Inc halijafukuza hata mfanyakazi mmoja? Hio ni kwa sababu products za Apple ni ngumu kucreate alternatives to, hivyo competition inakua chini, so hawakua na ulazima wa kuabsorb startups na waajiriwa wake ili kuuwa competition. Ila mambo kama search engines, social media etc hata graduate akiamua anatengeneza.

That's it..

Happy coding...
kali linux
 
Ukiangalia report za Mapato yao wanatangaza Faida kubwa sana, ila unasikia wamepunguza watu sababu ya uchumi mbaya.

Hilo la kuua Competition lina ukweli, pia jengine ni kuridhisha investors.
Ofcoz

Ila sana sana naona wanaitumia kama justified cause kufukuza kazi watu, na ukisoma barua zao za kutangaza layoffs ni kama vile wanaandikiwa na mtu mmoja.

Umeshafuatilia comp za Executives wao, hao jamaa wao kwa wao (execs) wanalipana hio mishahara sio ya uchumi wanaouongelea.

Kuna mdau mmoja muhanga wa hii kitu aliandika blog post akiulliza kwa nini comp za executives ndo zisipunguzwe kama kweli uchumi mbaya?
 
Kwanini wanatumia nguvu kubwa wakati bidhaa zao hazina mpinzani!!? Kama facebook ni bidhaa ambayo hata iundwe nyingine ya kufanana nayo haiwezi kuiua fb!
 
Kwanini wanatumia nguvu kubwa wakati bidhaa zao hazina mpinzani!!? Kama facebook ni bidhaa ambayo hata iundwe nyingine ya kufanana nayo haiwezi kuiua fb!
Kwanini unahisi hawana mpinzani? Na Technology ilivyo mtu anaweza kuanzia kampuni ghafla ikakutoa sokoni.

Twitter walikuwa na kampuni yao inaitwa Vine, muanzilishi wa short Videos, ila imeshakufa sasa hivi alietoboa ni tiktok, na huyo tiktok sasa hivi anakwenda kupambana na Youtube.

Facebook uti wake wa mgongo ni kukusanya Data na kuuza matangazo hio ndo source yao kubwa ya income na wapinzani wake ni kampuni kama Google na Adsense yao, hivyo kampuni yoyote yenye uwezo wa kukusanya data na kuuza matangazo kwao ni threat.
 
Back
Top Bottom