Rahma Salum
Member
- Sep 7, 2020
- 30
- 59
Rais wa Korea Kaskazini alionekana akiwa hai mara baada ya vyombo vya habari vya Kimataifa kama CNN kuripoti kuwa amefariki dunia. Je, ni kitu gani kilipelekea vyombo hivyo vya habari kutoa taarifa kuhusu kifo chake?
Mwaka 2020 kulitokea uvumi kuhusu kifo cha Rais wa Korea Kaskazini, Kim Jong-Un. Ripoti zilizotolewa na vyombo vya habari zilieleza kuwa amefariki dunia, vingine vikieleza kuwa yupo katika hatari ya kufa na vingine vikiripoti kuwa yupo kwenye hali ya ‘coma’.
Kitendo hicho kiligeuka kuwa aibu kwa CNN na vyombo vya habari vingine duniani, pamoja na vyombo vya habari vya kijasusi mara baada ya Kim kuonekana wiki moja baada ya kutangazwa kifo chake, akiwa anakata utepe wa moja ya kiwanda cha mbolea nje ya Pyongyang, Mji Mkuu wa Korea Kaskazini.
Ingawa ni vigumu sana kujua mambo yanayoendelea ndani ya Korea Kaskazini, picha hiyo ilidhihirisha mkanganyiko wa habari potofu na uvumi kwa Vyombo vya Habari.
Uvumi huo ulionekana kuanzia ndani ya nchi ya Korea Kusini, kutoka katika tovuti ambayo ilitoa taarifa kuhusu hali ya afya ya Kim. Tovuti hiyo kwa jina la Daily NK inahusiana na kutoa taarifa na uvumi kutoka Korea Kaskazini.
Ripoti ya Daily NK ya Aprili 20, 2020 ilisema kuwa Kim yupo hospitali kwa matibabu ya utaratibu wa moyo na mifupa ikidaiwa kuwa ni matokeo ya uvutaji wa sigara kupita kiasi na unene kupita kiasi, na kwamba inasemekana kuwa yupo katika hali nzuri. Daily NK ya lugha ya Kingereza ilieleza kuwa hali ile ilipelekea kufanyiwa upasuaji wa moyo.
Uvumi huo ulipata uzito zaidi kwa kuwa Kim hakuonekana kuanzia Aprili 11, 2020 hususan kwenye sherehe ya kila mwaka inayofanyika Aprili 15 ya Maadhimisho ya siku ya jua, ya kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa Kim II Sung ambaye ni babu yake Kim Jong-un.
Aprili 21, 2020 CNN iliripoti kuwa Kim baada ya kufanyiwa upasuaji wa moyo hali yake imekuwa mbaya na yupo mahututi katika hali ya nusu umauti. Taarifa hiyo ilitolewa huku ikitaja vyanzo vya taarifa kama ofisi za ujasusi kutoka Marekani ambayo haikutaja moja kwa moja ni nani.
Mtangazaji wa televisheni ya Marekani ya MSNBC, Katy Tur, aliandika katika ukurasa wake wa Twiiter kuwa Kim ubongo wake umekufa, baadae alifuta na kuomba radhi kwa kutoa ujumbe huo.
Rais wa kipindi hicho Donald Trump ambaye mara nyingi amekuwa akiviita vyombo vya habari vya Marekani ‘Taasisi za habari za uongo’, alisema kuwa taarifa iliyotolewa na CNN ni ya uongo. Aliongeza kuwa, yeye ana mahusiano mazuri na Kim Jong-Un hivyo ana imani kuwa yupo salama. Siku kadhaa baadae Trump alisema kuwa anafahamu vizuri kuhusu afya ya Kim lakini hatolizungumzia kwa muda huo.
Majibu yote yalijibiwa mara baada ya Korea Kaskazini kutoa picha za Kim akiwa na afya njema na mwenye tabasamu murua.
“Usiamini kabla ya kuhakiki taarifa. Ikiwa ni vigumu kupata taarifa kutoka Korea Kaskazini hata katika kipindi kizuri, inawezekana vipi kupata taarifa za afya ya Kim bila nchi kusika kutoa taarifa? Nchi ilikuwa katika hali ya kificho kwa sababu ya mlipuko wa Corona”, Alisema Jean H. Lee, Mkurugenzi wa Programu wa Korea katika kituo cha Wilson huko Washington.
Aliongeza kuwa, Korea Kusini sio chanzo kizuri cha taarifa. Ni lazima utafute vithibitisho na kuhakiki taarifa yoyote inayotokea katika vyanzo vya habari vya Korea Kusini.
Mwaka 2020 kulitokea uvumi kuhusu kifo cha Rais wa Korea Kaskazini, Kim Jong-Un. Ripoti zilizotolewa na vyombo vya habari zilieleza kuwa amefariki dunia, vingine vikieleza kuwa yupo katika hatari ya kufa na vingine vikiripoti kuwa yupo kwenye hali ya ‘coma’.
Kitendo hicho kiligeuka kuwa aibu kwa CNN na vyombo vya habari vingine duniani, pamoja na vyombo vya habari vya kijasusi mara baada ya Kim kuonekana wiki moja baada ya kutangazwa kifo chake, akiwa anakata utepe wa moja ya kiwanda cha mbolea nje ya Pyongyang, Mji Mkuu wa Korea Kaskazini.
Ingawa ni vigumu sana kujua mambo yanayoendelea ndani ya Korea Kaskazini, picha hiyo ilidhihirisha mkanganyiko wa habari potofu na uvumi kwa Vyombo vya Habari.
Uvumi huo ulionekana kuanzia ndani ya nchi ya Korea Kusini, kutoka katika tovuti ambayo ilitoa taarifa kuhusu hali ya afya ya Kim. Tovuti hiyo kwa jina la Daily NK inahusiana na kutoa taarifa na uvumi kutoka Korea Kaskazini.
Ripoti ya Daily NK ya Aprili 20, 2020 ilisema kuwa Kim yupo hospitali kwa matibabu ya utaratibu wa moyo na mifupa ikidaiwa kuwa ni matokeo ya uvutaji wa sigara kupita kiasi na unene kupita kiasi, na kwamba inasemekana kuwa yupo katika hali nzuri. Daily NK ya lugha ya Kingereza ilieleza kuwa hali ile ilipelekea kufanyiwa upasuaji wa moyo.
Uvumi huo ulipata uzito zaidi kwa kuwa Kim hakuonekana kuanzia Aprili 11, 2020 hususan kwenye sherehe ya kila mwaka inayofanyika Aprili 15 ya Maadhimisho ya siku ya jua, ya kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa Kim II Sung ambaye ni babu yake Kim Jong-un.
Aprili 21, 2020 CNN iliripoti kuwa Kim baada ya kufanyiwa upasuaji wa moyo hali yake imekuwa mbaya na yupo mahututi katika hali ya nusu umauti. Taarifa hiyo ilitolewa huku ikitaja vyanzo vya taarifa kama ofisi za ujasusi kutoka Marekani ambayo haikutaja moja kwa moja ni nani.
Mtangazaji wa televisheni ya Marekani ya MSNBC, Katy Tur, aliandika katika ukurasa wake wa Twiiter kuwa Kim ubongo wake umekufa, baadae alifuta na kuomba radhi kwa kutoa ujumbe huo.
Rais wa kipindi hicho Donald Trump ambaye mara nyingi amekuwa akiviita vyombo vya habari vya Marekani ‘Taasisi za habari za uongo’, alisema kuwa taarifa iliyotolewa na CNN ni ya uongo. Aliongeza kuwa, yeye ana mahusiano mazuri na Kim Jong-Un hivyo ana imani kuwa yupo salama. Siku kadhaa baadae Trump alisema kuwa anafahamu vizuri kuhusu afya ya Kim lakini hatolizungumzia kwa muda huo.
Majibu yote yalijibiwa mara baada ya Korea Kaskazini kutoa picha za Kim akiwa na afya njema na mwenye tabasamu murua.
“Usiamini kabla ya kuhakiki taarifa. Ikiwa ni vigumu kupata taarifa kutoka Korea Kaskazini hata katika kipindi kizuri, inawezekana vipi kupata taarifa za afya ya Kim bila nchi kusika kutoa taarifa? Nchi ilikuwa katika hali ya kificho kwa sababu ya mlipuko wa Corona”, Alisema Jean H. Lee, Mkurugenzi wa Programu wa Korea katika kituo cha Wilson huko Washington.
Aliongeza kuwa, Korea Kusini sio chanzo kizuri cha taarifa. Ni lazima utafute vithibitisho na kuhakiki taarifa yoyote inayotokea katika vyanzo vya habari vya Korea Kusini.