Namna ya kuachana na tabia za ngono zisizofaa: Maturbation & Ngono za kulipia

Namna ya kuachana na tabia za ngono zisizofaa: Maturbation & Ngono za kulipia

01savag

Member
Joined
May 24, 2023
Posts
57
Reaction score
120
Poleni na changamoto za hapa na pale, wanajamii wenzangu.

Naomba kupewa mwongozo kwenye hili suala (ruksa kunifokea).

Ukiachana na changamoto nyingine, suala la ngono nalo linaongoza kuharibu akili na maisha kiujumla hasa kwa vijana wa kiume wa miaka 18-29. Huu sio utafiti rasmi ila naongelea nilichokiona kwenye jamii sehemu mbalimbali nilizoishi.

1: Chaputa
Mara tu baada ya kuingia kwenye balehe, nilijikuta nimeingia kwenye uraibu wa masturbation. Hii tabia nimekaa nayo kwa miaka 5-6 mpaka nilipokuja kujichunguza na kugundua inaniathiri kisaikolojia. Sasa hivi ninautafuta mwezi wa tatu tangu nilipoacha huu mchezo na sina mpango wa kurudi huko haijalishi nini kitatokea.

2: Kulipia Ngono
Wiki za mwanzo baada ya kuacha masturbation, nilijikuta hamu ya ngono inaongezeka kupita maelezo na ubaya ni kwamba sikuwa na mahusiano yoyote. Hali ilizidi kuwa mbaya, ikafika hatua siwezi kufanya kazi vizuri. Nia ya kutafuta mtu wa kuwa naye kwenye mahusiano ikawa ngumu kidogo kulingana na namna nilivyojizoesha.

Ndipo nikapata wazo la kufanya ngono za kulipia wakati nikiendelea kumtafuta atakayenifaa kwenye safari ya maisha. Tinder, Badoo, na Tagged ndiyo zikawa sehemu zangu kubwa. Karibu kila wikiendi, naita mtu anakuja nyumbani namaliza nachohitaji, anasepa.

Hii tabia imenifanya niutelekeze hata ule mpango wa kutafuta wa kudumu, kwa sababu niliona kipengele cha kujuana kinanipotezea muda.

Nimelileta hili kwenu kwa sababu nataka kuachana na hizo tabia. Nimeona zina madhara kiuchumi, kisaikolojia na kijamii kiujumla.

Naomba mnipe mbinu ya kutumia kupambana na hamu ya ngono wakati nikiendelea kutafuta ubavu wangu wa pili tuoane.

Naamini ushauri wenu utanisaidia mimi na vijana wengine wengi walionasa kwenye hili tatizo.

Natanguliza shukrani zangu za dhati.
 
Ni rahisi sana, Fanya kazi masaa 14-16 Kwa siku walau Kwa wiki Tatu mfululizo, Monday - Saturday - pumzika siku moja tu… pesa utakazo pata ziwekee malengo mfano- mtaji wa biashara, ujenzi, ununuzi wa Vifaa vya kilimo etc…
Achana kuwazia papuchi Kila Wakati, Waza zaidi malengo yako.

Uchovu wa kazi wa siku sita Kwa wiki utakuondoa huko kwenye kinyama ugomvi.

Ukianza kutoboa kwenye malengo yako itakuwa motivation ya kutosha kuachana na kuchungulia magaguro Yao na maumbile Yao …
 
Kwa

Kwan rc huwezi kuokoka?? Nenda kalismatic, ni kundi ndani ya rc walio okoka.

Pia ushauri wangu, aisee oa tu haijalishi uchumi wako uponye, utajiset tu.
Hapo kama umenielewa vizuri ni kwamba nimechagua kutokufungamana/kutokuamini mambo ya dini.
Ila ninaheshim sana imani ya kila mtu,
 
Kila kitu ni nguvu ya maamuzi yako na kila mtu anayo hiyo nguvu ila kujiendekeza na kuona bado muda upo ndio vinatugharimu.

Nilikuwa addicted na baadhi ya tabia ila kuna siku nilijitafakari sana ni faida gani napata zaidi ya majuto, nikadhamiria kuacha japo haikuwa rahisi. Baada ya kupita muda mrefu bila kurudi kule nilipokuwa huwa nasema ni maamuzi tu hasa ukiwa timamu.
Mtegemee Mungu kama unaamini, fanya kazi, fanya mazoezi, ijali afya yako, jali maisha yako na ishi maisha yako. ✊✌
 
Ni rahisi sana, Fanya kazi masaa 14-16 Kwa siku walau Kwa wiki Tatu mfululizo, Monday - Saturday - pumzika siku moja tu… pesa utakazo pata ziwekee malengo mfano- mtaji wa biashara, ujenzi, ununuzi wa Vifaa vya kilimo etc…
Achana kuwazia papuchi Kila Wakati, Waza zaidi malengo yako.

Uchovu wa kazi wa siku sita Kwa wiki utakuondoa huko kwenye kinyama ugomvi.

Ukianza kutoboa kwenye malengo yako itakuwa motivation ya kutosha kuachana na kuchungulia magaguro Yao na maumbile Yao …
Nitajaribu kupita umo mpaka tarehe 10/07 (Nitaleta ushuhuda).
Shukrani zangu nyingi zikufikie mkuu🙏
 
Nitajaribu kupita umo mpaka tarehe 10/07 (Nitaleta ushuhuda).
Shukrani zangu nyingi zikufikie mkuu🙏
Na mimi nimeipenda comment ya kamanda hapo juu. Suala lako ni suala mtambuka na ni suala linalowaathiri watu wengi sana waume kwa wanawake, mabinti kwa vijana sema tu tulio wengi hatuko tayari kutamka. Kwa hiyo comment nyingi zimelenga kukushambulia kama kawaida yetu tunattak person na personality badala ya hoja.

Suala la kuokoka halijawahi kufanyiwa researches na halina uhakika , ni very subjective, ndio maana sioni kama ni solution bora, ila hoja ya Kamanda hii imeshanyiwa researches nyingi na zimeonyesha positive results, ingawa si 100% lakini matokeo ni mazuri by averages. Tunawaliohokoka wengi ila ukichunguza matendo yao yanazidi sisi wakatumeni. Wengine ni ndugu zangu na walikuwa wakitunyooshea vidole ila baadae wakatenda vitu mpaka sisi tunaogopa.ila hili suala la kuokoka tuliache kwani limekaa kiimani zaidi, turudi kwenye sayansi. Tunaomba utupe mrejesho baada ya kutekeleza.
 
Huwezi kuacha unyetukalization hata iweje lazima utarudia tu hiyo shughuli sababu umeifuzu kwa miaka 6.

Kuhusu kuoa hata ukioa ukishazoea tu mkeo then lazima utanyetuka. Wanaume wengi ndani ya ndoa kwasasa wanastruggle na nyeto kwasababu ni kitu wamekifanya kipindi cha nyuma na ilikuwa ni easy fix au escape ya kupata utulivu wa kimwili na kiakili.
 
Back
Top Bottom