Namna ya kuishi kwa kipato cha chini ya Tsh. 330,000/- kwa mwezi

Namna ya kuishi kwa kipato cha chini ya Tsh. 330,000/- kwa mwezi

mjusilizard

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2019
Posts
1,027
Reaction score
1,869
Wasalaam,

Watu wengi maeneo ya mijini vipato vyao ni wastani wa Tsh. 10,000 kwa siku, hii inafanya wengi wafikishe angalau Tsh. 330,000 kwa mwezi.

Kwa kipato hiki wapo wanaishi vizuri kabisa kwa familia za watu wachache na wanaishi bila kuwa na madeni. Mchanganuo rahisi ni kama huu hapa chini kwa faida ya wengi.

Kwanza kabisa hakikisha kwamba mke, mtoto na wewe msitumie zaidi Tsh. 200,000 kwa mwezi. Pia, mke na mtoto wawe na bima za afya kwa mwaka ambazo unalipia Tsh. 170000.

Wazazi wapewe Tsh. 80,000 tu, yaani, upande wa kike wapate Tsh. 40,000 na upande wa kike wapate hivyo hivyo. Kila mmoja, hasa mwanaume, awe na pocket money yake isiyozidi Tsh. 20,000 kwa mwezi.

Kama mmejenga tumieni sola tu, ila kama hamjajenga pangeni chumba kodi iwe si zaidi ya Tsh. 35,000 kwa mwezi. Inayobaki mnaweza kusevu. Ila hakikisha mama mjengo naye awe na sehemu ya kujipatia riziki ili kuziba mapengo yatakayojitokeza katikati hapo.

Mwisho kabisa, msipande magari safari fupi fupi ama kusafiri kwa daladala labda iwe ni lazima sana. Kila la heri!
 
Utabana na bado maisha yatakupiga tobo kwa kipato hicho pekee. Hapo jitahidi zaidi kuongeza kipato kuliko kubana matumizi. Fanya kazi za ziada kazini kwenu, fanya kazi nje ya kazini kwenu, fanya biashara na kadhalika. Vinginevyo hakuna kitu. Wazazi wako wataishije kwa hiyo Tsh 40,000 kwa mwezi? Au wanakula vocha tu?
 
Wasalaam,

Watu wengi maeneo ya mijini vipato vyao ni wastani wa Tsh. 10,000 kwa siku, hii inafanya wengi wafikishe angalau Tsh. 330,000 kwa mwezi.

Kwa kipato hiki wapo wanaishi vizuri kabisa kwa familia za watu wachache na wanaishi bila kuwa na madeni.
Sijakuelewa
 
Nafkiri mtu anaweza kuishi kwa kipato chochote kile. Ni yeye tu kuridhika Maisha yataenda. Asiporidhia hiyo hali ndio alternative nyingine inabidi azifanye ili afikeanakotaka.
 
Kwa iyo pesa lazima mke akukimbie ,...

Ni bora uwe single ,uteseke mwenyewe kwa hicho kipato huku ukijipanga kuongeza chanzo kingine cha kupata hela zaidi ....

Huwezi kuishi hivyo kama ulivoandika ....
 
Wasalaam,

Watu wengi maeneo ya mijini vipato vyao ni wastani wa Tsh. 10,000 kwa siku, hii inafanya wengi wafikishe angalau Tsh. 330,000 kwa mwezi.

Kwa kipato hiki wapo wanaishi vizuri kabisa kwa familia za watu wachache na wanaishi bila kuwa na madeni. Mchanganuo rahisi ni kama huu hapa chini kwa faida ya wengi.

Kwanza kabisa hakikisha kwamba mke, mtoto na wewe msitumie zaidi Tsh. 200,000 kwa mwezi. Pia, mke na mtoto wawe na bima za afya kwa mwaka ambazo unalipia Tsh. 170000.

Wazazi wapewe Tsh. 80,000 tu, yaani, upande wa kike wapate Tsh. 40,000 na upande wa kike wapate hivyo hivyo. Kila mmoja, hasa mwanaume, awe na pocket money yake isiyozidi Tsh. 20,000 kwa mwezi.

Kama mmejenga tumieni sola tu, ila kama hamjajenga pangeni chumba kodi iwe si zaidi ya Tsh. 35,000 kwa mwezi. Inayobaki mnaweza kusevu. Ila hakikisha mama mjengo naye awe na sehemu ya kujipatia riziki ili kuziba mapengo yatakayojitokeza katikati hapo.

Mwisho kabisa, msipande magari safari fupi fupi ama kusafiri kwa daladala labda iwe ni lazima sana. Kila la heri!
Duh kweli mkuu nakubali
 
Wanaume wa Dar watakwambia usioe kwa hela hiyo, ndio maana wanaume wa dar wataendelea kusemwa tu.
 
Mmmmmmh kumbe ndio maana CHAPUTA inazidi kuwa na followers [emoji2960][emoji2960][emoji2960][emoji174]
 
Afadhali wewe unayepata 330,000/= kwa mwezi. Mwenzio sasa napokea 170,000/= baada ya Bodi ya Mkopo wa Elimu ya Juu kunimulika hivi karibuni.

Nafikiri kuhamia bonde la mto Rufiji nikawe Mabala the farmer.😕
 
Pia, mke na mtoto wawe na bima za afya kwa mwaka ambazo unalipia Tsh. 170000.
Hili swala la Bima limenishinda kabisa Mimi Mungu kanivusha mwaka 2021 hatujaugua sasa hiyo 170k ndo inakua imepotea au inasogezwa mwaka mwingine?
 
Back
Top Bottom