Namna ya kukabiliana na mabomu ya kutoa machozi

Namna ya kukabiliana na mabomu ya kutoa machozi

Abraham Lincolnn

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2018
Posts
2,754
Reaction score
4,975
20240921_163709.jpg

Wakati unapojikuta umerushiwa mabomu ya kutoa machozi bila shaka utakuwa unapitia madhara ya kemikali hiyo. Lakini unaweza kufanya yafatayo kupunguza nguvu ya athari yake.
  • Songea sehemu yenye hewa safi haraka iwezekanavyo
  • Osha uso wako kwa kutumia maji ya baridi. Pia, unaweza kutumia mchanganyiko wa salini
  • Mabomu ya kutoa machozi yanaweza kushika kwenye nguo, kwa hiyo, pindi unapofika nyumbani, toa nguo ulizokuwa umevaa na kuziosha peke yake.
  • Aidha, kuna wale ambao wanasema kuosha uso kwa maziwa na maji inaweza kusaidia kupunguza hisia za kuchomeka.
  • Hata hivyo, unashauriwa kunywa maji mengi kusaidia kuondoa chembe zozote za mabomu ya kutoa machozi zilizosalia kwenye mfumo wako.
  • Ikiwa dalili zako ni kali au una shida ya kupumua, ni vyema kutafuta matibabu hospitalini.
Kwa ujumla athari za mabomu ya kutoa machozi zinaweza kutofautiana kulingana na umri, afya ya mtu lakini kiujumla madhara hayo ni ya muda mfupi na huweza kuondoka baada ya kuchukua hatua za awali.
20240921_163647.jpg
 
nawakumbusha muende na beto kama self defence mtu vipoti vikijichanganya pita navyo
Kwanza hakuna kijeba yeyote wa kwenda barabarani keshokutwa,achia mbali hizi sarakasi za jf na X.

Halafu ukienda ktk maandamano usibebe silaha yoyote wala usiokote silaha yoyote,utapigwa risasi.
Kama unataka kujaribu watu beba hata upinde,utakuja kunishukuru.
 
Back
Top Bottom