Abraham Lincolnn
JF-Expert Member
- Apr 12, 2018
- 2,754
- 4,975
Wakati unapojikuta umerushiwa mabomu ya kutoa machozi bila shaka utakuwa unapitia madhara ya kemikali hiyo. Lakini unaweza kufanya yafatayo kupunguza nguvu ya athari yake.
- Songea sehemu yenye hewa safi haraka iwezekanavyo
- Osha uso wako kwa kutumia maji ya baridi. Pia, unaweza kutumia mchanganyiko wa salini
- Mabomu ya kutoa machozi yanaweza kushika kwenye nguo, kwa hiyo, pindi unapofika nyumbani, toa nguo ulizokuwa umevaa na kuziosha peke yake.
- Aidha, kuna wale ambao wanasema kuosha uso kwa maziwa na maji inaweza kusaidia kupunguza hisia za kuchomeka.
- Hata hivyo, unashauriwa kunywa maji mengi kusaidia kuondoa chembe zozote za mabomu ya kutoa machozi zilizosalia kwenye mfumo wako.
- Ikiwa dalili zako ni kali au una shida ya kupumua, ni vyema kutafuta matibabu hospitalini.