Nampenda binti wa kitajiri ila ana kiburi, jeuri na dharau. Je, nimuoe?

Nampenda binti wa kitajiri ila ana kiburi, jeuri na dharau. Je, nimuoe?

kikoozi

JF-Expert Member
Joined
Jun 24, 2015
Posts
2,094
Reaction score
3,108
Habari za uzima ndugu, nina binti mmoja nipo nae kwenye mahusiano. Huyu binti kiukweli kabisa kutoka moyoni ni binti ambaye si wife material (kwangu), ila kuna kitu huwa nakiwaza sana kichwani.

Huyu binti kwao ni watu wenye uwezo mkubwa sana kipesa, yaani wana pesa sana sana sana wameiacha familia yangu kiuchumi kwa asilimia kama 75%.

Nina kazi yangu na nina shughuli zangu zingine za kunifanya niishi mjini bila shida yeyote ile lakini kuna muda wazo kichwani linaniambia kwamba, nimuoe huyu huyu nimzalishe pia nikiwa na uhakika wa asilimia 100% watoto wataishi kwenye good-life hata kama ikitokea mungu amenichukua.

Nikiwa nawaza hivyo roho yangu inashindwa kunifanya nimuache huyu binti, ila ni binti mwenye kiburi, jeuri, dharau na mambo mengine mengi tu ila ndio nipo naye.

Naombeni ushauri wenu wa dhati ndugu zangu, ili nichukue maamuzi sahihi kabisa.
 
Kama utamuoa kwasababu watoto wataishi kwenye good life ukifa sawa, nina uhakika utakufa mapema zaidi kwa tabia za huyo mwanamke...hakuna mwanaume rijali ambaye atakubali dharau,kejeli,kebehi,utovu wa nidhamu kwa mke wake hakuna na kama wapo ndio hawa marioo wa mjini, Sasa kwakuwa naww utaenda kuwa marioo basi kifo kitakuwa karibu nawe maana sononi zote zitakuwa zako..

Komaa kama mwanaume na ulichonacho hata kama kiduchu,.maana heri ya nusu shari kuliko shari kamili.
 
Sawa Mkuu, hawa Viumbe tunaishi nao kwa akili ya kiwango cha juu sana,
Mtengenezee mazingira ya kujiona ana deserve kua na ww katika nyakati zozote zile na kuonesha kua una mjali,atajihisi ni mtu sahihi sana kua na wew

Ila mambo ya kipato sio ya kutegemea sana Kwan kuna wakati anaweza kuonesha dharahu kwan anajua maisha yako yanamtegemea yeye unapokwama yeye ndo kimbilio lake japo sio vibaya kusaidiana ila inashusha ile egoo yako kama mwanaume
 
Mapenz ya kizaz hiki ni balaa tupu yan tunapenda imradi tumependa tu.Me naona usiwe mnyonge kwake hata kama kwao wana wadhifa town...onesha uanaume wako nadhan akishajua upoje kichwani hata dharau atapunguza kwako.

Wanaume wengi tunafeli sana kuonyesha udhaifu wetu kwa wanawake ndo maana dharau zinakua kubwa sana.

Kingine ni piga rungu, piga runguu mpk azilai ( joke )
 
Utaweza kuishi na dharau, kejeli, kebehi, kiburi etc? Pesa utatafuta zako bwana wee, usiingie kwenye ndoa kisa mwanamke ana pesa au anatoka familia matawi.
Shukrani
 
Mapenz ya kizaz hiki ni balaa tupu yan tunapenda imradi tumependa tu.Me naona usiwe mnyonge kwake hata kama kwao wana wadhifa town...onesha uanaume wako nadhan akishajua upoje kichwani hata dharau atapunguza kwako.

Wanaume wengi tunafeli sana kuonyesha udhaifu wetu kwa wanawake ndo maana dharau zinakua kubwa sana.

kingine ni piga rungu, piga runguu mpk azilai ( joke )
Shukrani
 
Sawa Mkuu, hawa Viumbe tunaishi nao kwa akili ya kiwango cha juu sana,
Mtengenezee mazingira ya kujiona ana deserve kua na ww katika nyakati zozote zile na kuonesha kua una mjali,atajihisi ni mtu sahihi sana kua na wew

Ila mambo ya kipato sio ya kutegemea sana Kwan kuna wakati anaweza kuonesha dharahu kwan anajua maisha yako yanamtegemea yeye unapokwama yeye ndo kimbilio lake japo sio vibaya kusaidiana ila inashusha ile egoo yako kama mwanaume
Sawa mkuu
 
kwanini usijiamini..? Kwani wewe huna uwezo wa kupambana ili baadae watoto wako wakae mahali pazuri kwa asilimia 💯,HATA SIKU MOJA USIWEKE MATUMAINI KWA MWANAMKE MWENYE PESA!!
Nimekuelewa mkuu, nawaza mbeleni uko kama nikiwa bahati mbaya sipo watoto wapate kuishi kuzuri pia
 
Kama unauwezo wa kumla tunda na hakuletei dharau na kibur kitandan bac una uwezo pia wa kumnyoosha,Kama anakupenda ataona unatimiza wajib wako kumfanya awe mke mwema ila kama hakupend na hauon kam ana uelekeo wa kubadirika achana nae mal n za kwao na wazaz wake aende zake !
 
Hata hayo maisha mazuri unayoyaona kwa familia ya huyo binti ujue kuna mwanaume alipambana..!,bado una muda wa kupambana na kufika walipo na hata kuwa zaidi yao as long as hujakata tamaa,weka kwanza vigezo vya mke unayemtaka mbele kama hajafit kwenye vigezo vyako na pia nafsi yako inakupa mashaka move on mkuu, usiendeshwe na woga wa maisha na mapenzi achana na hilo jipu kama hana values unazotaka.wazee walisema kosea vyote ila usikosee kuoa.
 
Back
Top Bottom