Najua wapo watakaoniona malaya, ila bora niseme liwalo na liwe.
Sababu za mimi kufungua ID mpya ni kwamba nkitumia ID yangu ya zamani bwana wangu atajua kuhusu hili. Na sina uhakika kuhusu huyu
Relief Mirzska maana namuona tu alivyo na kasi hizi siku za karibuni.
Kiukweli mimi nampenda sana huyu kaka na natamani niwe nae, nimepitia thread zake najua ameoa ila nipo tayar vyovyote iwavyo na iwe. Jamani msinione malaya na msiniulize nampendea nini. Moyo ukipenda hula nyama mbichi, napenda anavyoandika, napenda kusoma English yake, mimi ni rafiki yake ila naona amekuwa mgumu kuelewa. Saa nyengine anaringaaa, ovyooo!!!
Kuna wadada humu kila anachopost wao wana-like tu, jamani wengine mnatuumiza na ndio maana nimeamua kuja hapa. Wadau hebu naombeni msaada wenu, shemeji yenu kila nkimwambia mimi sipendi anywe pombe hataki kuacha mpaka namchukia sasa na nadhani naingia kwenye penzi na
Relief Mirzska ndio maana moyo wangu unamchukia huyu jamaa.
Kwani mtu raha si unatakiwa ujipe mwenyewe??
Na wewe
Relief Mirzska punguza kuringa, mimi nipo tayar tupige shoo moja ya kibabe moyo wangu utatulia. Najua ushanijua, tafadhali we mkaka jamani aggghhhh.