Doctor Mama Amon
JF-Expert Member
- Mar 30, 2018
- 2,089
- 2,725
Kardinali Rugambwa akiwa na Rais Kikwete, lakini kabla hajawa Kardinali
Kwa dhati, nampongeza Askofu Protase Rugambwa Prosper Iholana, ambaye familia yake inayo makazi ya kudumu katika Kijiji cha Kasheshe, Kata ya Nyaishozi, Wilaya ya Karagwe, mkoani Kagera, kwa Kuteuliwa kuwa Kardinali Mpya.
Nawapongeza waumini wa Nyaishozi Karagwe, mkoani Kagera, kwa kumzaa na kulea Kardinali Rugabwa.
Pia nawapongeza wanafunzi wake wote wa Seminari Ndogo ya Katoke, Biharamulo kwa mwalimu wao kuwa Kardinali.
Pia namkaribisha sana Kardinali Rugambwa huku kwetu "Sumbawanga Town".
Wote tumwekeni katika maombi.