Uchaguzi 2020 Namshauri Lissu asifanye kampeni, panakaribia kucha

Ni wakati wa ni yeye kujipima uzito. Kama uzito ni mkubwa kwa kiwango tunachofikiri basi ana nafasi ya kushinda. Mzani ameshapewa kaambiwa asifanye kampeni siku saba.
 
Watanzania Wa ccm ni wasahaulifu kweli,washasahau kuwa wao ndo walimfikisha Lisu ubelgiji,sa hii wanasema alienda kujigijigi.
 

[emoji2][emoji2][emoji2]hizi bangi huwa mnavutia wapi??

unadhani jeshi la serikali ni kama hao mbavu wavaa miwani wa hapo ufipa,kwamba msipowalipa wanagoma kufungua geti.

nyinyi endeleeni na campaign za kumnadi mgombea wenu,atumie vizuri kila nafasi atakayoipata,isijetokea huko mbele mtu anasema ameonewa.
 
Ukimuona kifaranga kajaa chungu ujuwe kunamamayake lisu limama lake nilikubwa kama tembo sisi tutulie ukombozi umekaribia labda
Si kweli. Hakuna Mama wala mjomba. Kuna kukanyaga haki tu, kisha waliokanyagiwa haki wakituambia umenikanyagia haki tunawasingizia kutumwa na wamama wakubwa
 


Sheria zetu na kanuni za uchaguzi zinaweza kuwa na upungufu hata kwenye baadhi ya maamuzi ya watendaji wake. Hata hivyo kwa sheria za Tanzania mamlaka ya juu kabisa katika masuala ya uchaguzi ni Tume. Huwezi kukata rufaa dhidi ya maamuzi yake. Hivyo ni busara kuheshimu maamuzi hayo vinginevyo Lisu ataingia kwenye mvutano hasi na vyombo vya dola. Asifike huko hakutakuwa na tija kwake au chama chake. Na ngonjela za Hague zitabakia ngonjela tu kwa sababu mchakato wake ni mgumu na mrefu. Huu ni ushauri mdogo tu, asijipime ubavu na dola.
 
Kusingizia mwenzako katumwa na mabeberu ni mbinu chafu ya kampeni. Kuadhibu mpinzani wako kwa kumzuia asikampeni ni mbinu chafu nyingine. Wanaofanya hivi wana jeshi kubwa ajabu la kampeni ardhini. Msijidanganye kuwa mgombea wao amechoka au anaumwa. Yuko fit. Wanataka kuwalaza usingizi wa siku saba, mkiamka boli liko wavuni. Fanyeni kampeni hata iweje. Mbona mlikuwa na usemi eti hakuna kulala hadi kieleweke? Hakijaeleweka! Fanya kampeni!
 
Bora afanye kampeni na wajaribu kumzuia ili dunia ione na ikusanye vizuri ushahidi juu ya hawa wauaji na watu wenye roho mbaya

Ingawa hili tu la kumzuia kufanya kampeni kwa siku 7 ni ushahidi tosha

I fully agree! Kama kanuni zimekiukwa agizo ni batili, aendelee na kampeni, wafanye wafanyacho kila mtu auone uovu wa mfumoCCM!
 
Dunia itawafanyia nini? Kwa sasa kila mtu yupo kwenye ujisaidie mwenyewe mode........zaidi watatoa tu maneno yao yakupeana moyo ndo imekwisha hio
Ndo mnavyojidanganya hapo Lumumba??? Endeleeni tu na ujinga wenu!! Mtajua hamjui mwaka huu
 
Ndo mnavyojidanganya hapo Lumumba??? Endeleeni tu na ujinga wenu!! Mtajua hamjui mwaka huu
Mshapapaswa tayari mlichofanya ni kutoa povu tu na bado tarehe 28 mtapigwa soft touch za kutosha andaeni mabambucha hayo
 
Mshapapaswa tayari mlichofanya ni kutoa povu tu na bado tarehe 28 mtapigwa soft touch za kutosha andaeni mabambucha hayo
Mmepagawa CCM au tumepagawa Chadema????

Unatumia kiungo gani kufikiri???
 
Nani kasema?
Wewe unaonaje??? Lissu ana furaha, bashasha tele. Chadema wana raha, furaha na amani Ila CCM hawana amani, ni kutoa vitisho kwa wananchi na kuhamasisha ubaguzi tu kupitia mgombea wao Jiwe!!!

Au wewe huna akili hujaona haya?
 
Wewe unaonaje??? Lissu ana furaha, bashasha tele. Chadema wana raha, furaha na amani Ila CCM hawana amani, ni kutoa vitisho kwa wananchi na kuhamasisha ubaguzi tu kupitia mgombea wao Jiwe!!!

Au wewe huna akili hujaona haya?
Nimeona tarehe 28 Magufuli anaendelea na miaka 5 tena , kila mtu ana uhuru wa kuona apendacho maisha ni kuchagua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…