Namshukuru Mungu JF imenipa mke mwema

Namshukuru Mungu JF imenipa mke mwema

Kuna kipindi nilikuja hapa jukwaani kulalamika na kuomba wanajukwaa hili wanisaidie kumpata mwanamke niliyempenda sana na ni member anayejulikana kwa jina la rubii baada ya jitihada za kumbembeleza akashindwa kabisa kunikubali pengine baada ya kujua biashara yangu ( kuuza na kusambaza majeneza, sanda na vifaa vyote vya kuzikia).

Nilitumia kila njia kumbembeleza pamoja na kuahidi kumwoa na kumpa kila atakachotaka lakini ilishindikana. Kama ujuavyo kila jambo hupangwa na Mungu, kuna member waliokuja Pm ili kutaka japo kunifariji.

Mwisho wa yote kuna mdada mmoja akavutiwa na mimi na kuanza mawasiliano ambapo baadae tulikubaliana kuonana nikamtumia nauli akaja Dom tukafahamiana she is naturally beauty na amekubaliana na maisha yangu na tuko katika maandalizi ya kwenda kweo kutoa posa.

Nimeamini kwamba sio kila mwanamke aliye JF ni malaya au mchunaji kuna wanawake wako serious kuolewa. Ningemtaja lakini kulingana na umaarufu wake hapa jukwaani sintomtaja mapema mpaka tukishafunga ndoa. Ana elimu nzuri na ni mwajiriwa serikalini na ameikubali kazi yangu.

Nawashukuru mods na waanzilishi wa JF pamoja na wote mlioniombea mema.
Mungu atangulie mipango iweze kukamikika ili muweze kufurahia uumbaji wa Mungu!
 
[emoji57][emoji57] mimi kiumbe sio...! Ama nini


Bro You are mistaken I think!
Anyway sio wewe walaaaa namaanisha mwingine kabisaa kuna mmoja alitaka kuleta habari za kuna petro na kuna yuda akajishaua eti don't quote or mention me anywhere khakhaakhaa nikacheeeeekaa
Miye teinaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa lol mpaka waleo heshima inachukua mkondo wake

mzeewakungoa Maisha haya ukizoea watu sanaaaaa waeza hatarisha ndoa yako takatifu

Cc Smart911
 
Back
Top Bottom