Namuacha kwa sababu ana matumizi makubwa ya pesa

Namuacha kwa sababu ana matumizi makubwa ya pesa

Jiko Koa

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2023
Posts
248
Reaction score
825
Huyu mpenzi wangu nilitaka nimuoe ila nimeahirisha. Kila nikiacha hela asubuhi, hata kama ni nyingi, lazima aitumie yote.

Mfano; Leo niliacha elfu 50 na ndani kuna shehena za unga, mchele, maharagwe, mafuta ya kupikia, unga wa ngano, viungo vyote vya mboga n.k. Lakini nimerudi nakuta imetumika yote.

Halafu vitu vinavyoonekana alinunua leo ni maziwa ya unga 400g, cocoa ya elfu 5 na tea masala ya elfu 5. Eti elfu 50 imeisha. Kwanza hivyo vitu vina umuhimu gani zaidi ya kuchezea hela tu? Yaani halafu kwao ni maskini, hauwezi amini kwanini haheshimu pesa.

Nikimuuliza, ananipandishia sauti. Nimewaza nimkatae tu.
 
Tatizo wewe ndio umemzoesha Hivyo! Tatizo umemzoesha toka mwanzo wa maisha yenu, Alishazoea na mbaya zaidi ni kuwa ukimwambia na yeye ANAKUJA juu, Hana utii kabisa kwako mpige chini ulikosea mwenyewe au mkalishe chini umwambie kuhusu matumizi yake na jinsi anavyokujia juu, akishupaza shingo achana nae
 
Hongera zake kupata bwana anayemwachia 50 per day hata kabla hajaolewa Wala kuzaa na huyo bwana.
Siyo kwamba nipo vizuri Ila huwa naacha hela ninayokadiria kuwa itamaliza siku tatu au nne lakini mwenzangu anaitumia yote. Mara chocolate ya Elfu 10, mara chips kuku wakati ndani Kuna vyakula aina nyingi tu. Sasa tutakuwa tunachumia matumbo
 
Huyu mpezi wangu Nilitaka nimuoe ila nimeahirisha. Kila Nikiacha hela asubuhi, hata kama Ni nyingi lazima aitumie yote.

Mfano; leo niliacha elfu 50 na Ndani Kuna shehena za unga, mchele, maharagwe, mafuta ya kupikia, unga wa ngano, viungo vyote vya mboga n.k lakini nimerudi nakuta imetumika yote.

Alafu vitu vinavyoonekaza alinunua leo Ni maziwa ya unga 400g, cocoa ya elfu 5 na tea masala ya elfu 5 eti elfu 50 imeisha. Kwanza hivyo vitu vina umuhimu gani zaidi ya kuchezea hela tu?

Nikimuuliza ananipandishia sauti. Nimewaza nimkatae.
Una uhakika uliacha elfu 50? Usije ukawa unaongeza masifuri ili kujihalaliishia maamuzi yako
 
Huyu mpezi wangu Nilitaka nimuoe ila nimeahirisha. Kila Nikiacha hela asubuhi, hata kama Ni nyingi lazima aitumie yote.

Mfano; leo niliacha elfu 50 na Ndani Kuna shehena za unga, mchele, maharagwe, mafuta ya kupikia, unga wa ngano, viungo vyote vya mboga n.k lakini nimerudi nakuta imetumika yote.

Alafu vitu vinavyoonekaza alinunua leo Ni maziwa ya unga 400g, cocoa ya elfu 5 na tea masala ya elfu 5 eti elfu 50 imeisha. Kwanza hivyo vitu vina umuhimu gani zaidi ya kuchezea hela tu?

Nikimuuliza ananipandishia sauti. Nimewaza nimkatae.
Jaribu kusoma attitude na tabia yake, hasa hilo la kukupandishia sauti halina picha nzuri.....ni bora ukaweka msingi mapema kabla mambo hayajawa magumu mbeleni.
 
Tatizo wewe ndio umemzoesha Hivyo! Tatizo umemzoesha toka mwanzo wa maisha yenu,Alishazoea na mbaya zaidi ni kuwa ukimwambia na yeye ANAKUJA juu,Hana utii kabisa kwako mpige chini ulikosea mwenyewe au mkalishe chini umwambie kuhusu matumizi yake na jinsi anavyokujia juu,akishupaza shingo achana nae
Yaani alafu kwao ni maskini hauwezi amini kwanini haheshimu pesa
 
Pole braza
Mi nakushauri tafuta hela tu chief
Elf 50 ni ndogo na yeye ana matumizi yake
Huyu mpezi wangu Nilitaka nimuoe ila nimeahirisha. Kila Nikiacha hela asubuhi, hata kama Ni nyingi lazima aitumie yote.

Mfano; leo niliacha elfu 50 na Ndani Kuna shehena za unga, mchele, maharagwe, mafuta ya kupikia, unga wa ngano, viungo vyote vya mboga n.k lakini nimerudi nakuta imetumika yote.

Alafu vitu vinavyoonekaza alinunua leo Ni maziwa ya unga 400g, cocoa ya elfu 5 na tea masala ya elfu 5 eti elfu 50 imeisha. Kwanza hivyo vitu vina umuhimu gani zaidi ya kuchezea hela tu?

Nikimuuliza ananipandishia sauti. Nimewaza nimkatae.
 
Back
Top Bottom