Namuogopa X wangu

Namuogopa X wangu

Akikutafuta muulize ni nini lengo lake haswa, kwakuwa umeshajua kipi unapaswa kufanya sidhani kama itakuwa ngumu kwako kuepuka usiyoyataka yatokee.

Ningekuwa najua kwa uchache kuhusu aliyoyafanya ningeshauri zaidi ila sijui ngoja niishie hapa japo napenda sana mzidi kuwa pamoja. Au mwamba hana maisha unayoyataka wewe?
Nikieleza sana anaweza pita hapa akaelewa bure ila nishawahi kumuuliza anadai ananipenda ila sasa maneno na vitendo tofauti.

Kuhusu maisha yake anaonekana ni mlalahoi tu ila nilimpenda hivyo hivyo sbb ndani yake kuna vitu vingi vilinivutia japo yeye anajitutumua nimuone tajiri kitu ambacho kilikua kinanikwaza sbb nilihisi anadhani mim ni malayah wakudanganywa kwa mali wakati nilitamani aniheshimu kama mwanamke ninayempenda yeye kama yeye na ninayehangaika kutafuta riziki yangu kwa njia za halali.
 
Hahaha................Kwa Usalama wa afya zetu, ni muhimu sana kubugia dawa za pressure na Sukari hasa kama tuna appointment na hawa watoto wa elfu 2

Nimewahi kusikia sifa zao kupitia Mzee mwenzangu ERoni kwamba they are so energetic on bed, na kama hautakuwa jirani na dawa zako za pressure na Sukari unaweza kuamkia Kwa Janabi Muhimbili 😜🙌
Mkuu,
Tusisahau dawa za pressure na sukari. Mambo ya kukutwa lodge umenyooka ni aibu sana. Japo mimi na afmbili ni maji na mafuta🤣
 
Nikieleza sana anaweza pita hapa akaelewa bure ila nishawahi kumuuliza anadai ananipenda ila sasa maneno na vitendo tofauti.

Kuhusu maisha yake anaonekana ni mlalahoi tu ila nilimpenda hivyo hivyo sbb ndani yake kuna vitu vingi vilinivutia japo yeye anajitutumua nimuone tajiri kitu ambacho kilikua kinanikwaza sbb nilihisi anadhani mim ni malayah wakudanganywa kwa mali wakati nilitamani aniheshimu kama mwanamke ninayempenda yeye kama yeye na ninayehangaika kutafuta riziki yangu kwa njia za halali.
Hutaki kuongea nae, mbona rahisi sana...block and ignore! Ikitokea akatuma text kwa namba mpya just ignore, kumpotezea mtu ni rahisi sana, unless na wewe unafurahia kusoma texts zake, I know the feeling!!
 
As Salaam Alaikum dear all.

Wakuu,kuna X wangu ambae niliona ili niwe na amani ya moyo na kujilinda na stress ni kukata mawasiliano nae.Yaani simpigii, simtext wala sipokei wala kujibu text zake.

Sasa huyu bwana nilishamwambia mara kibao kuwa sitaki anipigie wala anitext ila siku akijisikia anapiga sipokei. Atakaa tena siku anatext sijibu.

Siku tena akijisikia atapiga au atatext sijibu ila nakua nakasirika kwanini aheshimu ombi langu kuwa sitaki mawasiliano nae!Na simblock sbb nilishawahi kumblock akanitafuta kwa namba nyingine.

Sasa sbb yakuandika huu uzi ni kwamba kuna kitu sijielewi kuhusu huyu mtu na sijui nifanyaje iwe tofauti.

Ni hivi,wakati tuko pamoja nilikua namuheshimu sana na kumuogopa huyu mwanaume ila tatizo ni kwamba pamoja na kuwa tumeachana bado namuogopa flani hivi 🤣 na nahisi kagundua hicho kitu na ndo sababu anapuuzia katazo langu kwa sababu sina ujasiri wa kuongea nae kwa ukali kwa mdomo kwa kumaanisha kuwa sitaki anitafute.

Nina ujasiri tu wa kumwambia kwa text. Tatizo text zangu zenyewe anazidharau tu hata hazijibugi na akijisia anapiga tu saa yeyote au anatext bila kujali kuwa inaweza kuleta shida.

Sasa recently, nimefanya kitu nikajidharau sana. Huyu X alipiga simu usiku mwingi, kuamka naona namba yake. Nikakasirika sana, nikasema huyu leo atanijua mimi nani. Nikaapa kuwa leo namtukana, nampa mineno ya hovyo hadi akome but poor stupid me,😭nilivyopokea tu na nikasikia sauti yake ujasiri wote wa kumtukana ukaisha.

Sikuweza tena kumpa mineno ya hovyo niliyopanga kumpa instead nikawa naongea nae kwa heshima na unyenyekevu ☹️ kama zamani😭.

Alivyokata simu tu ndo nikamuandikia sasa sms kuwa sitaki mawasiliano nae.

Wakuu,sitaki kuendelea kumuogopa huyu mtu.Nifanyaje niweze kumwambia kwa mdomo wangu.

Naamini siku nikiweza kumpandishia sauti huyu ataheshimu ombi langu
Siungesema tu kwamba bado unampenda kuliko unavyo jitetea
 
Mkuu,
Tusisahau dawa za pressure na sukari. Mambo ya kukutwa lodge umenyooka ni aibu sana. Japo mimi na afmbili ni maji na mafuta🤣
Kwa kweli, ni aibu kama ulivyosema

Hongera kuruka viunzi vya watoto wa elfu 2

Mimi pia nitajaribu, weekend hii nitapita barabara ya survey bila kusimamisha gari na kuwasalimia pale Utawala wala geti dogo 😜
 
Umepata penz jipya ndiomaan unamdharau, penz jipya linakuaga tam san had unahis huyo x wako alikua hajui mapenz, ila penz jipya utam wake unaisha baada ya miez 3 hkn rang utaacha kuona
 
Nikieleza sana anaweza pita hapa akaelewa bure ila nishawahi kumuuliza anadai ananipenda ila sasa maneno na vitendo tofauti.

Kuhusu maisha yake anaonekana ni mlalahoi tu ila nilimpenda hivyo hivyo sbb ndani yake kuna vitu vingi vilinivutia japo yeye anajitutumua nimuone tajiri kitu ambacho kilikua kinanikwaza sbb nilihisi anadhani mim ni malayah wakudanganywa kwa mali wakati nilitamani aniheshimu kama mwanamke ninayempenda yeye kama yeye na ninayehangaika kutafuta riziki yangu kwa njia za halali.
Kumbe na humu jf yumo?

Sio kwamba anafanya hivyo ili umuone tajiri, huyo anafanya kwa ajili yako ni vile tu uwezo hana nawewe uwezi kumvumilia.
 
Back
Top Bottom