Namuona Edgar Devis kwenye damu ya Pappy Tshishimbi

Namuona Edgar Devis kwenye damu ya Pappy Tshishimbi

Daaaaah... kuna jamaa alisema ni DHAMBI kufananisha KIPAPLIPAPLI na FURSANA....

Umesema nani na Edgar Davis???
Nipe namba yake "Huyo Jamaa" ili tumsaidie kumtoa umbumbumbu.
 
Hakuna aliyekuwa na chembe ya shaka baada ya kukamilika kwa mtanange wa ngao ya hisani kuhusu Pappy.

Man of the Match Mkongomani Pappy Kabamba Tshishimbi anaonekana kuwa na damu yenye vina saba na mchezaji wa Taifa la Holand Edgar Davis.

Tutegemee tuzo ya mchezaji bora wa kigeni msimu wa 2017/18 kutua mikononi mwa Pappy K. Tshishimbi.
Huyu Jamaa anafanya kazi ambayo ilikuwa ikifanywa na wachezaji wawili wa msimu uliopita yaani (Niyonzima + Zullu).

Nisiongee sana ngoja nitafakari jinsi Dogo Gadiel MICHAEL alivyomuweka mfukoni Emmanuel A. Okwi.
Matokeo vipi??
Huyu mkongo niwe mkweli yuko vizuri, kiango chake sio cha kuchezea yanga! Yanga watamuharibu!
 
Endelea kubisha, Maana ulibisha msimu wa 2016/17 Yanga hawezi kuwa Bingwa. Ukabisha hata kumtambua Bingwa lakini mwisho wa siku ulimtambua kwa lazima.
Jamaa kaziba pengo la Niyonzima halafu kapitiliza. Ni mtamu kuliko muwa wa mtibwa. Hongera kamati ya Usajili ya yanga.
 
Mkubwa jaribu kuwa serious kidogo,acha kumfananisha mwanadamu na msukule,kumfananisha Davis na Shishibaby ni dharau zilizopitiliza matokeo ya kipimo cha mkojo!
Hajamfananisha. Kasema damu ya Kabanga INA vinasaba na damu ya Edgar.
Labda ni MTU na binamu yake. Edgar ni Msurinam ( black from west africa).
 
Back
Top Bottom