Nandy, Mafiga matatu yatakuponza

Nandy, Mafiga matatu yatakuponza

[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] nisome hapa utanielewa vema


Sent using Jamii Forums mobile app
Ahsante nitapitia

BARIKIWA
 
Kila mtu ana kipawa, talanta na kipaji chake , lakini kati ya hivyo vitatu kimoja ndio hujitokeza zaidi na kwa baadhi viwili ndio huonekana zaidi

Talanta na kipawa hivi viko kiroho na kiimani zaidi huku kipaji kikiwa kiko kimwili na kidunia zaidi. Kwenye hii dunia kuna falme kuu mbili , ufalme wa Nuru na ufalme wa giza...ufalme wa nuru uko kiimani zaidi kwa maana ya Kimungu na ufalme wa giza uko kidunia zaidi kwa maana ya shetani ...hizi ni falme mbili zisizochangamana

Nandy binti mwenye kipaji cha uimbaji kupitia nyimbo zilizomtambulisha za kidunia alianza na kufanya vema sana kwenye hii kaliba, lakini sasa anapotea..anachanja mbuga kuelekea porini...Pengine kwakuwa jasiri muongoza njia hayupo tena..

Pressure ya kubaki kileleni, mashindano ya vipaji vipya na ugumu wa soko huku akiwa hana washauri wazuri vinaweza kuwa matokeo ya yale anayofanya sasa

Nandy kashindwa kushika moja, anachanganya mambo matatu kwa wakati mmoja
Bongo fleva
Bongo movie
Gospel
Hivi vitu vitatu huwa kamwe havipikiki chungu kimoja hata siku moja...kila kimoja kina chemistry yake, ladha yake na mashabiki yake... Lazima ujitambulishe na kukubalika kwenye moja ya makundi hayo

Kuchanganya bongo fleva na bongo movie ni kujiua kisanii kwakuwa iko wazi kabisa kuwa sisi wabongo na haya mambo ya sinema za kisasa tumefeli big time..HATUWEZI.. Sisi tuko vizuri kwenye mziki walau kwasasa

Kuchanganya bongo fleva na gospel ni sawa na kuzipambanisha falme mbili zenye kutofautiana kwenye kila kitu....leo uombe nogesha kesho uimbe Mungu ni mwema ...HUTAELEWEKA KAMWE... Utajimaliza mwenyewe

Figa tatu alizochagua Nandy hazirandani asilani..anatawanya na kupoteza nguvu zake bila kujua.....Na hapaswi kutafuta mchawi kwenye hili zaidi ya washauri wake

Shetani akizeeka huwa malaika.. Usitake kuwa malaika kabla hujazeeka. Yuko wapi Stara Thomas? Mzee Yusuph ndio huyo anatanga na njia sasa...Kuna wakongwe kama Cosmas Chidumule na Mzee Makassy hawa walipoamua kuipa dunia kisogo na kumgeukia Mungu hawakuyumba wala kurudi nyuma.

Kina TID wameamua kuingia bongo movie kwakuwa hawana nafasi tena kwenye soko la mziki...huko wanalazimisha tuu...ili walau siku zisonge

Kwa umri wake Nandy na kipaji kilichomtoa cha bongo fleva angejenga mhimili imara kwanza huko.... Wakati anahangaika na bongo movie kina Zuchu wanampiku kwenye chart za umaarufu...!!!

All in all kama kaamua moja la kumrudia Mola wake na kuimba Gospel katika umri huo , awe na nia thabiti ya kiroho asije akageuka na kurudi alikotoka...ataishia kuchanganyikiwa... Kumrudia Mungu ni vita sio bata... Amuige Hafsa Kazinja...

Kama anashaurika basi atulie na kuanza upya na ashike moja tuu kwakuwa mshika mawili moja humponyoka...sasa yeye kashika matatu kwa mpigo...!!!
TID si yupo bongo movie toka enzi za ile movie ya 'Girlfriend' wayback
 
Leo anaimba nyimbo video zake amevaa vichupi
Kesho yuko kwenye gospel kwakweli sio jambo jema kabisa huko ni kumjaribu Mungu
Achague Moja tu kama ni wa moto awe wamoto na kama ni wabaridi awe hivyo pia na sio vugu vugu
 
Kuchanganya bongo fleva na bongo movie ni kujiua kisanii kwakuwa iko wazi kabisa kuwa sisi wabongo na haya mambo ya sinema za kisasa tumefeli big time..HATUWEZI.. Sisi tuko vizuri kwenye mziki walau kwasasa
Kuchanganya bongo fleva na gospel ni sawa na kuzipambanisha falme mbili zenye kutofautiana kwenye kila kitu....leo uombe nogesha kesho uimbe Mungu ni mwema ...HUTAELEWEKA KAMWE... Utajimaliza mwenyewe
Ok, tujadili hizo hoja.
Hiyo hoja ya kwanza ya kusema kuwa filamu haifanyi vizuri hivyo yeye kuchanganya filamu na bongo fleva haina uhalisia kwa sababu hujaeleza ni kwa jinsi gani kutokufanya vizuri kwa filamu za Tanzania kutafanya yeye ashuke katika bongo fleva. Au watu watasema “fvck! Nandy ameanza kuigiza!? Mimi sipendi bongo movie kwa hiyo kama nandy ameanza kuigiza basi sifuatilii muziki wake” (kitu ambacho hakina uhalisia). Au atawekeza sana kwenye filamu na atapotesa focus kwenye muziki? Hii nayo haonekani kufanya kazi kwa sababu sidhani kama nandy yupo serious sana filamu kiasi a’risk bongo fleva yake.

Tuje kwenye hiyo hoja ya pili kuwa bongo fleva na gospel ni falme mbili tofauti (giza na mwanga) hivyo kuchanganya ni kupambanisha falme mbili tofauti.

Kwanza kabisa, mimi siamini katika hayo mambo ya giza na mwanga, shetani sijui dhambi. Siamini katika hizo mambo so pia siamini kama hiyo vita unayoiongelea inaweza kutokea. Lakini pia dhana ya kuwa kuna madhara ya kuchanganya bongo fleva na gospel haifanyi kazi kwenye uhalisia kwa sababu kila muziki una maudhui yake na una sehemu yake. hivi kwa mfano mchungaji na mkewe wakiwa faragha, mke wa mchungaji akaamua kumuimbia mme wake wimbo wa nandy (let say ‘ninogeshe’) huku akicheza mbele yake, atakuwa anapambanisha falme mbili tofauti kwa kuwa yeye ni mke wa mchungaji na anaimba wimbo wa bongo fleva? Au nandy akiamua kutenga muda wake kuimba wimbo wa kumsifu Mungu atakuwa anapambanisha falme mbili tofauti kwa kuwa yeye anaimba bongo fleva?

Kuamini kuwa muziki wa bongo fleva ni muziki wa giza (au wa kishetani) na mziki wa gospel ni muziki wa mwanga (Mungu) ni dhana ambayo haipaswi kuendekezwa kwa sababu haina uhalisia. Watu tunapitia hali tofauti na tunahitaji mahitaji tofauti kukidhi hali hizo tofauti. Kuna wakati mtu atahitaji kusikiliza nyimbo za mapenzi na kuna wakati mtu anahitaji kusikiliza gospel. Sasa kama mtu mmoja anaweza kusikiliza bongo fleva na gopel kwa nyakati tofauti kuna ubaya gani msanii mmoja akafanya gospel na bongo fleva kwa nyakati tofauti? Na pia umeonyesha kuwa ili nandy afanikiwe ki bongo fleva anatakiwa aachane na gospel na kulingana na mtizamo wako (wa giza na mwanga) unamshauri amwache Mungu ili afanikiwe katika shetani. Wewe ni nani unayehimiza watu wafanikiwe katika shetani? Hakuna uhalisia.

Simaanishi kuwa nandy hawezi kushuka kimuziku (bongo leva) kwa kuchanganya hivyo vitatu, lakini hoja ulizoweka sidhani kama zinafanya kazi, hazina uhalisia.

Njia pekee ambayo itamshusha nandy kwa kuchanganya vitu hivi vitatu ni kama atakosa focus, kwamba leo kaacha bongo fleva kahamia kwenye gospel, muda kidogo baadaye anaacha gospel na kuhamia kwenye filamu, baada ya muda tena anaanza kufanya vyote vitatu nk nk.
 
Ok, tujadili hizo hoja.
Hiyo hoja ya kwanza ya kusema kuwa filamu haifanyi vizuri hivyo yeye kuchanganya filamu na bongo fleva haina uhalisia kwa sababu hujaeleza ni kwa jinsi gani kutokufanya vizuri kwa filamu za Tanzania kutafanya yeye ashuke katika bongo fleva. Au watu watasema “fvck! Nandy ameanza kuigiza!? Mimi sipendi bongo movie kwa hiyo kama nandy ameanza kuigiza basi sifuatilii muziki wake” (kitu ambacho hakina uhalisia). Au atawekeza sana kwenye filamu na atapotesa focus kwenye muziki? Hii nayo haonekani kufanya kazi kwa sababu sidhani kama nandy yupo serious sana filamu kiasi a’risk bongo fleva yake.

Tuje kwenye hiyo hoja ya pili kuwa bongo fleva na gospel ni falme mbili tofauti (giza na mwanga) hivyo kuchanganya ni kupambanisha falme mbili tofauti.

Kwanza kabisa, mimi siamini katika hayo mambo ya giza na mwanga, shetani sijui dhambi. Siamini katika hizo mambo so pia siamini kama hiyo vita unayoiongelea inaweza kutokea. Lakini pia dhana ya kuwa kuna madhara ya kuchanganya bongo fleva na gospel haifanyi kazi kwenye uhalisia kwa sababu kila muziki una maudhui yake na una sehemu yake. hivi kwa mfano mchungaji na mkewe wakiwa faragha, mke wa mchungaji akaamua kumuimbia mme wake wimbo wa nandy (let say ‘ninogeshe’) huku akicheza mbele yake, atakuwa anapambanisha falme mbili tofauti kwa kuwa yeye ni mke wa mchungaji na anaimba wimbo wa bongo fleva? Au nandy akiamua kutenga muda wake kuimba wimbo wa kumsifu Mungu atakuwa anapambanisha falme mbili tofauti kwa kuwa yeye anaimba bongo fleva?

Kuamini kuwa muziki wa bongo fleva ni muziki wa giza (au wa kishetani) na mziki wa gospel ni muziki wa mwanga (Mungu) ni dhana ambayo haipaswi kuendekezwa kwa sababu haina uhalisia. Watu tunapitia hali tofauti na tunahitaji mahitaji tofauti kukidhi hali hizo tofauti. Kuna wakati mtu atahitaji kusikiliza nyimbo za mapenzi na kuna wakati mtu anahitaji kusikiliza gospel. Sasa kama mtu mmoja anaweza kusikiliza bongo fleva na gopel kwa nyakati tofauti kuna ubaya gani msanii mmoja akafanya gospel na bongo fleva kwa nyakati tofauti? Na pia umeonyesha kuwa ili nandy afanikiwe ki bongo fleva anatakiwa aachane na gospel na kulingana na mtizamo wako (wa giza na mwanga) unamshauri amwache Mungu ili afanikiwe katika shetani. Wewe ni nani unayehimiza watu wafanikiwe katika shetani? Hakuna uhalisia.

Simaanishi kuwa nandy hawezi kushuka kimuziku (bongo leva) kwa kuchanganya hivyo vitatu, lakini hoja ulizoweka sidhani kama zinafanya kazi, hazina uhalisia.

Njia pekee ambayo itamshusha nandy kwa kuchanganya vitu hivi vitatu ni kama atakosa focus, kwamba leo kaacha bongo fleva kahamia kwenye gospel, muda kidogo baadaye anaacha gospel na kuhamia kwenye filamu, baada ya muda tena anaanza kufanya vyote vitatu nk nk.
Stephano nashindwa kuendeleza mjadala nawe kwakuwa kuna mahali tuna maono tofauti
1. Si mfuatiliaji wa bongo muvi (hata mimi pia) lakini hujahangaika japo uone episode moja ama kusaka habari za mhusika na kaliba yake hiyo ya sinema...kwahiyo kwako hapa ni ngumu kujadili kile nilichoandika

2. Huamini katika mambo ya kiimani na kiroho , falme mbili za giza na mwanga, kitu ambacho kiko kwenye mada yangu..hapa ni ngumu pia kujenga hoja jadilika kwakuwa tayari nilichoandika hakina mashiko kwako

Ishu ya mke wa mchungaji kumwimbia mumewe chumbani sio hoja kwakuwa hayo ni mambo binafsi faraghani na hapa hatujadili faragha ya Nandy

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kila mtu ana kipawa, talanta na kipaji chake , lakini kati ya hivyo vitatu kimoja ndio hujitokeza zaidi na kwa baadhi viwili ndio huonekana zaidi

Talanta na kipawa hivi viko kiroho na kiimani zaidi huku kipaji kikiwa kiko kimwili na kidunia zaidi. Kwenye hii dunia kuna falme kuu mbili , ufalme wa Nuru na ufalme wa giza...ufalme wa nuru uko kiimani zaidi kwa maana ya Kimungu na ufalme wa giza uko kidunia zaidi kwa maana ya shetani ...hizi ni falme mbili zisizochangamana

Nandy binti mwenye kipaji cha uimbaji kupitia nyimbo zilizomtambulisha za kidunia alianza na kufanya vema sana kwenye hii kaliba, lakini sasa anapotea..anachanja mbuga kuelekea porini...Pengine kwakuwa jasiri muongoza njia hayupo tena..

Pressure ya kubaki kileleni, mashindano ya vipaji vipya na ugumu wa soko huku akiwa hana washauri wazuri vinaweza kuwa matokeo ya yale anayofanya sasa

Nandy kashindwa kushika moja, anachanganya mambo matatu kwa wakati mmoja
Bongo fleva
Bongo movie
Gospel
Hivi vitu vitatu huwa kamwe havipikiki chungu kimoja hata siku moja...kila kimoja kina chemistry yake, ladha yake na mashabiki yake... Lazima ujitambulishe na kukubalika kwenye moja ya makundi hayo

Kuchanganya bongo fleva na bongo movie ni kujiua kisanii kwakuwa iko wazi kabisa kuwa sisi wabongo na haya mambo ya sinema za kisasa tumefeli big time..HATUWEZI.. Sisi tuko vizuri kwenye mziki walau kwasasa

Kuchanganya bongo fleva na gospel ni sawa na kuzipambanisha falme mbili zenye kutofautiana kwenye kila kitu....leo uombe nogesha kesho uimbe Mungu ni mwema ...HUTAELEWEKA KAMWE... Utajimaliza mwenyewe

Figa tatu alizochagua Nandy hazirandani asilani..anatawanya na kupoteza nguvu zake bila kujua.....Na hapaswi kutafuta mchawi kwenye hili zaidi ya washauri wake

Shetani akizeeka huwa malaika.. Usitake kuwa malaika kabla hujazeeka. Yuko wapi Stara Thomas? Mzee Yusuph ndio huyo anatanga na njia sasa...Kuna wakongwe kama Cosmas Chidumule na Mzee Makassy hawa walipoamua kuipa dunia kisogo na kumgeukia Mungu hawakuyumba wala kurudi nyuma.

Kina TID wameamua kuingia bongo movie kwakuwa hawana nafasi tena kwenye soko la mziki...huko wanalazimisha tuu...ili walau siku zisonge

Kwa umri wake Nandy na kipaji kilichomtoa cha bongo fleva angejenga mhimili imara kwanza huko.... Wakati anahangaika na bongo movie kina Zuchu wanampiku kwenye chart za umaarufu...!!!

All in all kama kaamua moja la kumrudia Mola wake na kuimba Gospel katika umri huo , awe na nia thabiti ya kiroho asije akageuka na kurudi alikotoka...ataishia kuchanganyikiwa... Kumrudia Mungu ni vita sio bata... Amuige Hafsa Kazinja...

Kama anashaurika basi atulie na kuanza upya na ashike moja tuu kwakuwa mshika mawili moja humponyoka...sasa yeye kashika matatu kwa mpigo...!!!
Nilikua natetea sana bangi ila kwa sasa naomba wazuie tu.
Hapo namaanisha hivi kweli uimbe bongo fleva umevaa vyupi, harafu upate nguvu za kuimba gospel umevaa kanzu.
 
Ok, tujadili hizo hoja.
Hiyo hoja ya kwanza ya kusema kuwa filamu haifanyi vizuri hivyo yeye kuchanganya filamu na bongo fleva haina uhalisia kwa sababu hujaeleza ni kwa jinsi gani kutokufanya vizuri kwa filamu za Tanzania kutafanya yeye ashuke katika bongo fleva. Au watu watasema “fvck! Nandy ameanza kuigiza!? Mimi sipendi bongo movie kwa hiyo kama nandy ameanza kuigiza basi sifuatilii muziki wake” (kitu ambacho hakina uhalisia). Au atawekeza sana kwenye filamu na atapotesa focus kwenye muziki? Hii nayo haonekani kufanya kazi kwa sababu sidhani kama nandy yupo serious sana filamu kiasi a’risk bongo fleva yake.

Tuje kwenye hiyo hoja ya pili kuwa bongo fleva na gospel ni falme mbili tofauti (giza na mwanga) hivyo kuchanganya ni kupambanisha falme mbili tofauti.

Kwanza kabisa, mimi siamini katika hayo mambo ya giza na mwanga, shetani sijui dhambi. Siamini katika hizo mambo so pia siamini kama hiyo vita unayoiongelea inaweza kutokea. Lakini pia dhana ya kuwa kuna madhara ya kuchanganya bongo fleva na gospel haifanyi kazi kwenye uhalisia kwa sababu kila muziki una maudhui yake na una sehemu yake. hivi kwa mfano mchungaji na mkewe wakiwa faragha, mke wa mchungaji akaamua kumuimbia mme wake wimbo wa nandy (let say ‘ninogeshe’) huku akicheza mbele yake, atakuwa anapambanisha falme mbili tofauti kwa kuwa yeye ni mke wa mchungaji na anaimba wimbo wa bongo fleva? Au nandy akiamua kutenga muda wake kuimba wimbo wa kumsifu Mungu atakuwa anapambanisha falme mbili tofauti kwa kuwa yeye anaimba bongo fleva?

Kuamini kuwa muziki wa bongo fleva ni muziki wa giza (au wa kishetani) na mziki wa gospel ni muziki wa mwanga (Mungu) ni dhana ambayo haipaswi kuendekezwa kwa sababu haina uhalisia. Watu tunapitia hali tofauti na tunahitaji mahitaji tofauti kukidhi hali hizo tofauti. Kuna wakati mtu atahitaji kusikiliza nyimbo za mapenzi na kuna wakati mtu anahitaji kusikiliza gospel. Sasa kama mtu mmoja anaweza kusikiliza bongo fleva na gopel kwa nyakati tofauti kuna ubaya gani msanii mmoja akafanya gospel na bongo fleva kwa nyakati tofauti? Na pia umeonyesha kuwa ili nandy afanikiwe ki bongo fleva anatakiwa aachane na gospel na kulingana na mtizamo wako (wa giza na mwanga) unamshauri amwache Mungu ili afanikiwe katika shetani. Wewe ni nani unayehimiza watu wafanikiwe katika shetani? Hakuna uhalisia.

Simaanishi kuwa nandy hawezi kushuka kimuziku (bongo leva) kwa kuchanganya hivyo vitatu, lakini hoja ulizoweka sidhani kama zinafanya kazi, hazina uhalisia.

Njia pekee ambayo itamshusha nandy kwa kuchanganya vitu hivi vitatu ni kama atakosa focus, kwamba leo kaacha bongo fleva kahamia kwenye gospel, muda kidogo baadaye anaacha gospel na kuhamia kwenye filamu, baada ya muda tena anaanza kufanya vyote vitatu nk nk.
Subiri matokeo ndo yatakuaminisha .....!!!
 
Stephano nashindwa kuendeleza mjadala nawe kwakuwa kuna mahali tuna maono tofauti
1. Si mfuatiliaji wa bongo muvi (hata mimi pia) lakini hujahangaika japo uone episode moja ama kusaka habari za mhusika na kaliba yake hiyo ya sinema...kwahiyo kwako hapa ni ngumu kujadili kile nilichoandika

2. Huamini katika mambo ya kiimani na kiroho , falme mbili za giza na mwanga, kitu ambacho kiko kwenye mada yangu..hapa ni ngumu pia kujenga hoja jadilika kwakuwa tayari nilichoandika hakina mashiko kwako

Ishu ya mke wa mchungaji kumwimbia mumewe chumbani sio hoja kwakuwa hayo ni mambo binafsi faraghani na hapa hatujadili faragha ya Nandy

Sent using Jamii Forums mobile app
Vyovyote vile iwavyo, linapokuja swala la vipaji vya sanaa, sidhani kama ni jambo zuri kumwambia mtu aache kufanya kitu fulani kwa sababu huwezi jua hicho kitu kina mizizi kiasi gani katika furaha yake. Ni vema kushauri namna bora ya kuvifanya katika namba ambayo haitaadhiri sanaa yake kuu ambayo kwa kiasi kikubwa ndiyo inayoleta chakula mezani.

Yeye mwenyewe akiamua kuachana na kitu fulani ni sawa kwa kuwa atakuwa amepima nakuona faida na hasara zake.
 
Vyovyote vile iwavyo, linapokuja swala la vipaji vya sanaa, sidhani kama ni jambo zuri kumwambia mtu aache kufanya kitu fulani kwa sababu huwezi jua hicho kitu kina mizizi kiasi gani katika furaha yake. Ni vema kushauri namna bora ya kuvifanya katika namba ambayo haitaadhiri sanaa yake kuu ambayo kwa kiasi kikubwa ndiyo inayoleta chakula mezani.

Yeye mwenyewe akiamua kuachana na kitu fulani ni sawa kwa kuwa atakuwa amepima nakuona faida na hasara zake.
Ok thanks kwa mchango wako nimekupata vema[emoji1545][emoji1545][emoji1545]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tofauti na zile cover songs mbili za gospel, kuna nyingine katoa?

Huyu hayupo kwenye gospel. Ni mwana bongo fleva na mkata mauno tu.
 
Ebwanae umeongea vzr sana sina neno la kutia,Nandy nafikiri katokea kwny familia za zilizoshika dini sasa huenda kuna msukumo kutoka katika familia unaomkosoa kufanya nyimbo za kidunia,so kuacha ameshindwa na kuamua kushika vyote,
Hata hivyo Mungu amekataza michanganyo ya hivyo,Nusu kwenye dunia nusu unamtumikia
Kuna mistari kwny biblia inasema bora kuwa wa baridi au moto kuliko kuchagua vuguvugu
Nandy anachofanya nikuamua kuwa vuguvugu.
 
Back
Top Bottom