Nani amelielewa tangazo hili la Bank of Tanzania (BoT), atufafanulie!

Nani amelielewa tangazo hili la Bank of Tanzania (BoT), atufafanulie!

Hapa wanawalenga wale wanaohifadhi pesa kwenye ndio chini ya godoro na sehemu mbali mbali tofauti na benki, lengo ni wajue Tanzania Kuna matajiri wangapi
 
Noti gani hizo za zamani ziko kwenye mzunguko? Labda kama kuna watu walidhihifadhi kama kumbukumbu kuwa kuliwahi kuwa na noti za namna hiyo. Actually huwa zipo, unakuta mtu kwenye pochi yake moja ya kifuko kaweka noti ya zamani kama show tu
 
Hela zinazotumika sa hivi hazihusiani hapo na Kusanyo hilo na ndo maana wametoa muda mfupi sana wa kuzikusanya... Ni ngumu sana Nchi zilizokuwa Africa eti urudishe fedha zote kwa miezi mi tatu tuu.

Hapo zinaondolewa zile noti za zamani ukiacha ambazo ziko kwenye mzunguko wa sa hivi. Na nyongeza pia hata noti za mia tano zilizotoka 2010.

Shilingi 50 na 200 na 100 na 500 za sarafu hazihusiani hapo kwani hizi zipo za mwaka 1994 au 1995 nyingi ila wameongelea noti ndo zinakusanywa..

Tangazo liko wazi kabisa ila naona watu wemefikiria mengi mara kwasababu ya uchaguzi mara kwasababu ya wanaoficha hela...

Wakati ni kama naona lina wapa nafasi walokosa matumizi wa hizo hela za zaman sa hivi zinawapa nafasi kwenda kubadilishiwa(ukute ni njia ya kuingiza fedha ambazo watu walikosa pa kuzitumia au pakupeleka)
Yaani naona wameends kuhalalisha kitu ambacho watu walishaamini hakina matumizi tena
 
1000117360.jpg
 
Sura yake ikiwekwa kwenye noti! Itabidi niwe ninatumia Dola au fedha ya kenya
 
Tangazo ni hili
--
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUONDOA KWENYE MZUNGUKO NOTI ZA ZAMANI ZA SHILINGI YA TANZANΝΙΑ

Benki Kuu ya Tanzania inapenda kuufahamisha Umma kuhusu zoezi la kuondoa kwenye mzunguko noti za zamani za shilingi ishirini (20), mia mbili (200), mia tano (500), elfu moja (1000), elfu mbili (2000), elfu tano (5000) na elfu kumi (10000) kwa matoleo ya mwaka 1985 hadi mwaka 2003, na noti ya shilingi mia tano (500) iliyotolewa mwaka 2010 zenye sifa zilizoainishwa kwenye Tangazo la Serikali Na. 858 la tarehe 11 Oktoba 2024.

Zoezi la ubadilishwaji linatarajiwa kuanza tarehe 06 Januari 2025 hadi tarehe 05 Aprili 2025 kupitia Ofisi zote za Benki Kuu na benki zote za biashara kwa kupatiwa malipo yenye thamani sawasawa na kiasi kitakachowasilishwa. Aidha, matumizi ya noti hizo yatafikia ukomo wa kuwa fedha halali za Tanzania kuanzia tarehe 06 Aprili, 2025. Baada ya tarehe hiyo, mtu yeyote au taasisi yoyote inayomiliki fedha hizo haitaruhusiwa kuzitumia katika kufanya malipo popote duniani; na benki zote hazitaruhusiwa kulipa wala kupokea amana au maombi ya kubadilisha noti zilizoondolewa kwenye mzunguko.

Hivyo, Benki Kuu inatoa rai kwa wananchi wote wenye akiba ya noti hizo za zamani, kuzibadilisha au kuziweka amana kwenye benki yoyote ndani ya kipindi kilichotolewa.

Kwa taarifa/msaada zaidi tafadhali wasiliana na: Kurugenzi ya Usimamizi wa Sarafu, Benki Kuu ya Tanzania, 2 Mtaa wa Mirambo, S.L.P 2939 Dar es Salaam; au kwa Barua Pepe: info@bot.go.tz au botcommunications@bot.go.tz; au kwa simu +255745 802 007.

Emmanuel M. Tutuba.

GAVANA

View attachment 3135997

Sawa, Noti mpya za Fedha tayari zimechapishwa, lakini waTanzania hatujaelezwa sababu hasa za msingi na zenye mashiko zilizopelekea kuchapishwa kwa Noti hizo mpya.
1. Zopi hasa sababu za msingi kabisa za kuchapishwa kwa Noti hizo mpya ikiwa Noti za awali zilizopo kwenye mzunguko bado zipo imara Sana hazijachakaa wala haziijachoka? What are the Motives behind for printing of these new Banknotes?
2. Kwa nini wameamua kuingiza kwenye mzunguko Noti hizo Mpya kwenye kipindi hiki kibaya wakati nchi ikiwa kwenye mzigo mkubwa zaidi wa Bajeti ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025? Kwa nini hasa wameamua kuwaongezea Wananchi mzigo wa Kodi ili kugharamia mchakato mzima wa uchapishaji wa hizo Noti Mpya? Je, kulikuwa na ULAZIMA sana wa kufanya hivyo katika kipindi hiki cha Bajeti ya Uchaguzi Mkuu?
3. Je, Gharama kiasi gani ambazo zimetumika kwenye mchakato mzima wa kuzalisha hizo Noti mpya?
Hivi kweli kulikuwa na ULAZIMA wa kufanya hivyo kweli??


Naona kama kuna mashaka makubqa sana kuhusiana na Mchakato wa Uchapishaji wa hizo Noti mpya. Hapakuwa na uwazi kabisa kwenye utekelezaji wa suala hili. Habari ya kuwepo kwa Noti mpya ilikuja kama shambulizi la kushitukiza "ambush". Wananchi hatukuwahi kutaarifiwa kabla kuhusiana na suala zima la uwepo wa Zabuni au kuwepo kwa nia ya kutaka kuchapisha noti Mpya.
Isije ikawa zoezi hilo limefanywa kwa nia ovu ya kupata Fedha zisizo haliali za kugharamia zoezi la uchaguzi Mkuu ujao wa Oktoba 2025. Kwa sababu Wahusika wanajua ni vigumu Sana kwa Wananchi kuweza ku-detect ufisadi kuhusiana na Fedha Mpya ambazo bado hazijawahi kuingia kwenye mzunguko wa Fedha unaodhibitiwa na Benki Kuu kwa sababu Fedha hizo Mpya zinakuwa bado hazijawa discounted na Benki Kuu.
 
Back
Top Bottom