Nani amesema Mzee Dosa Aziz Ali alifirisika kwa kupigania uhuru?

Nani amesema Mzee Dosa Aziz Ali alifirisika kwa kupigania uhuru?

Namkumbuka mzee mmoja humu wa kuitwa mohamed SAID akiandika alichokiita historia ya wazee wake wa sijui Gerezani au Kariakoo ndiye aliyekuwa analalamika sana kuhusu Dossa Aziz kufilisika na kufa maskini akiishia kuzikwa kwao Bagamoyo bila aliowafadhili kuhudhuria.soon atakuja kukuparura ktk post yako hii maana waonyesha upo against nae....utaniambia!
Dosa hakuzikwa bagamoyo bali mlandizi.
 
Kuna watu wanadai mzee Dosa alifilisika kwasababu alitumia rasilimali zake kupigania uhuru wa Tanganyika. Yuko wapi mwenye ushahidi huo?
Wewe ndiyo ulipaswa kutufahamisha historia ya Mzee Dosa kama unaijua kisha kuomba ushahidi kwa wengine sasa wewe umakuja na povu tu unauliza hili kijua au unataka kujua?
 
Sawa nani alimtuma kama alitoa kwa hiyari we unalalamika nini?
Wakati anatoa alikwambia anahitaji utajo Mahala popote

Haya malalamiko umemsikia mwenyewe akilalamika???

Usiwe kama walete Kati imepenya
kuwa mwanaume kamili ukihisi kuzungumza la msingi ni gharama bora kunyamaza
 
Wakati anatoa alikwambia anahitaji utajo Mahala popote

Haya malalamiko umemsikia mwenyewe akilalamika???

Usiwe kama walete Kati imepenya
kuwa mwanaume kamili ukihisi kuzungumza la msingi ni gharama bora kunyamaza
Wapi nimesema huyo jamaa alilalamika?
 
Lengo la huu uzi ni kuwakata kidomodomo wale wanafiki wooote wanaojifanya wana midomo mirefu kama ya kasuku kuwaongelea wengine. Mtu anaandika uzi mrefu sana eti mzee Dossa alifilisika kwasababu alishiriki harakati za ukombozi wa Tanganyika. Mtoa uzi huo alikuwa na lengo la kupotosha umma kwa malengo yake machafu.

Mzee Dossa kama wengine mf. kina Rupia, Sykes n.k walishiriki kwa hali na mali ili kuona Tanganyika inapata uhuru wake. Kama Dossa alifilisika basi alifilisika kwasababu nyingine na sio kupigania uhuru.

Acheni upotoshaji vijana
 
Yule aliyesema hivyo alikuja na sababu na pia aliwahi kumhoji mhusika moja kwa moja,sasa angalau na wewe ungekuja na sababu au utafiti kidogo kukanusha la kuelezea kuwa hakufilisika kwa ajili ya siasa. Mimi sikubaliani na yule aliyeleta mada au wewe,lakini kwa faida ya wengi ni vema ukaja na usahihisho.
 
Mzee Dosa Aziz ni miongoni mwa mashujaa walio tukuka katika historia ya nchi hii

Ni kweli marehemu Dossa Aziz alitoa mchango mkubwa katika kupigania uhuru wa nchi hii. Yeye kama ilivyokuwa kwa marehemu John Rupia hakupewa cheo serikalini bali alikuwa mjumbe wa kamati kuu ya Chama tawala . Ingawa yeye hakutunukiwa vyeo seriklini lakini ndugu zake kama vile Hamza Aziz alikuja kuwa Inspector General wa polisi!!

Kama kufilisika Dossa hakufilisika wakati wa kugombea uhuru bali mali ilikuja kumtupa mkono miaka mingi baada ya uhuru wakati huo akiwa amemuoa mama mmoja wa kiarabu dada ya mke wa zamani wa Abbas Sykes!!!
 
Namkumbuka mzee mmoja humu wa kuitwa mohamed SAID akiandika alichokiita historia ya wazee wake wa sijui Gerezani au Kariakoo ndiye aliyekuwa analalamika sana kuhusu Dossa Aziz kufilisika na kufa maskini akiishia kuzikwa kwao Bagamoyo bila aliowafadhili kuhudhuria.soon atakuja kukuparura ktk post yako hii maana waonyesha upo against nae....utaniambia!
Sir...
Umeanza kwa kuandika katika lugha ya kifedhuli...''alichokiita,'' ''sijui.''
Namna hii ya kuchangia hatutakuwa na mjadala wenye manufaa hata
kidogo ila tutakaribisha watu wa mfano huo na mjadala utavurugika.

Hili la kuita historia wala si mimi peke yangu ukitazama ''catalogue,'' ya
''Library of Congress,'' ambako yako mengi niliyoandika utaona yapo
chini ya ''history.''

Ukipenda unaweza pia ukapita Cambridge Journal of African History.
Kote mambo ni kama unavyosoma.

Hili mosi.
Pili haiwezekani mimi nikasema Dossa Aziz kwao, Bagamoyo.

Baba yake Dossa, Aziz Ali na nyumba ya babu yangu Salum Abdallah
zilikuwa jirani Gerezani katika miaka ya 1930s

Nawafahamu vizuri akina Dossa Aziz na historia ya ukoo wao.
 
Lengo la huu uzi ni kuwakata kidomodomo wale wanafiki wooote wanaojifanya wana midomo mirefu kama ya kasuku kuwaongelea wengine. Mtu anaandika uzi mrefu sana eti mzee Dossa alifilisika kwasababu alishiriki harakati za ukombozi wa Tanganyika. Mtoa uzi huo alikuwa na lengo la kupotosha umma kwa malengo yake machafu.

Mzee Dossa kama wengine mf. kina Rupia, Sykes n.k walishiriki kwa hali na mali ili kuona Tanganyika inapata uhuru wake. Kama Dossa alifilisika basi alifilisika kwasababu nyingine na sio kupigania uhuru.

Acheni upotoshaji vijana
Amani Msumari,
Ikiwa mwandishi kapotosha itapendeza mwenye ukweli na yeye akaandika.

Historia ya Dossa ni maarufu inajulikana.

Historia ya Mshume Kiyate pia maarufu inajulikana na harakati za uhuru
zilichukua fedha nyingi katika mali zao.

Labda ikiwa mtu hajui historia za watu hawa.
Laiti kama nisingeandika historia zao hakuna mtu angewajua hadi sasa.

Kuna mtu alipata kumsikia Abdul na Ally Sykes wakitajwa katika historia
ya TANU na kudai uhuru?

Kipi kiliipata serikali hadi kuwapa medali katika kumbukumbu ya miaka 50
ya uhuru ilhali kwa miaka hiyo yote 50 hawakuwapo katika historia ya TANU?
 
Amani Msumari,
Ikiwa mwandishi kapotosha itapendeza mwenye ukweli na yeye akaandika.

Historia ya Dossa ni maarufu inajulikana.

Historia ya Mshume Kiyate pia maarufu inajulikana na harakati za uhuru
zilichukua fedha nyingi katika mali zao.

Labda ikiwa mtu hajui historia za watu hawa.
Laiti kama nisingeandika historia zao hakuna mtu angewajua hadi sasa.

Kuna mtu alipata kumsikia Abdul na Ally Sykes wakitajwa katika historia
ya TANU na kudai uhuru?

Kipi kiliipata serikali hadi kuwapa medali katika kumbukumbu ya miaka 50
ya uhuru ilhali kwa miaka hiyo yote 50 hawakuwapo katika historia ya TANU?
Ni kweli pasi na shaka kuwa muandishi wa habari huibua mambo na kuwapasha watu habari

Hatahivyo,unapoandika habari unapaswa ujrdhshe kabla ya kuandika. Kwa mfano katika kuandika habari hiyo hakuna popote unapothbtsha uhusiano wa kujitoa kwa marehemu Dossa na kufilisika kwake.

Aidha kuwa jirani na mtu sio lazima kuijua historia yake. Pia sidhani kama ni kweli kuwa usingeandika wewe basi wengine tusingejua. Tunakushukuru kwa kusambaza habari ambayo naamini na wewe umepekua mabuku kuisoma.
 
Kuna watu wanadai mzee Dosa alifilisika kwasababu alitumia rasilimali zake kupigania uhuru wa Tanganyika. Yuko wapi mwenye ushahidi huo?

Ni kweli alifilisika kwa kujitolea mali zake kupigania uhuru. Kwa bahati mbaya hakuna anayemkumbuka na walau angetumia mali yake hiyo kutoa sadaka na kusaidia masikini pengine Mola wake angemlipa pepo ya daraja la juu kabisa.
 
Ni kweli pasi na shaka kuwa muandishi wa habari huibua mambo na kuwapasha watu habari

Hatahivyo,unapoandika habari unapaswa ujrdhshe kabla ya kuandika. Kwa mfano katika kuandika habari hiyo hakuna popote unapothbtsha uhusiano wa kujitoa kwa marehemu Dossa na kufilisika kwake.

Aidha kuwa jirani na mtu sio lazima kuijua historia yake. Pia sidhani kama ni kweli kuwa usingeandika wewe basi wengine tusingejua. Tunakushukuru kwa kusambaza habari ambayo naamini na wewe umepekua mabuku kuisoma.
Amani Msumari,
Sishangai kuwa leo unaulizwa ushahidi kuhusu Dossa.

Kwani huko nyuma nilishangaa sana kwani hata jina lake ilipoandikwa
historia ya TANU na Chuo Cha Kivukoni, halikuwapo kitabu kizima.

Wala sikushangaa Dossa aliposahauliwa wakati Nyerere alipotoa medali
zaidi ya 3000 kwa watu waliotoa mchango mkubwa katika Tanzania.

Waarabu wana msemo wanasema, ''Sababu huondoa ajabu.''

Ama hilo la kuwa historia hii ingelijulikana hata mimi kama ninsingeandika
labda niseme kuwa kwa mara ya kwanza nilipoandika historia hii na kuchapwa
na gazeti la Africa Events (London), toleo zima lilikusanywa na kutolewa katika
mzuguko lisisomwe.

Jina la makala yangu ilikuwa, ''In Praise of Ancestors,'' March/April 1988.
Nafahamu mengi sana kuhusu historia hii.

Ukitaka kuthibitisha hebu soma historia ya babu yangu mmoja wa wazalendo
waliopigania uhuru wa Tanganyika kwa hali na mali:
Mohamed Said: KUTOKA JF: BABU YANGU SALUM ABDALLAH

Mimi sikupekua buku lolote kuijia historia hii.

Chanzo changu cha kwanza ni nyumbani kwetu na chanzo cha pili ni Nyaraka
za Sykes.

Ingia hapo chini:
Mohamed Said: NYARAKA ZA SYKES KATIKA KAVAZI LA MWALIMU NYERERE
 
Ndugu Mohamed Said,kutokana na maelezo yako,bila shaka utakuwa ni mtu ambae umekwenda umri.
Unaeleza kuwa chapisho lako katika gazeti la Africa Events (London) la mwaka 1988ukilipa kichwa cha habari "In Praise of Ancestors" lilitolewa kwenye mzunguko. MASWALI;
1. Je, ni nani aliyatoa magazeti/makala hayo kwenye mzunguko?

2. Unadhani ni sababu gani iliyosababisha yatolewe kwenye mzunguko?

3. Je, unahisi marehemu Dossa alifanya kosa gani mpaka historia yake ipotezwe ilihali wapigania uhuru wengine wametajwa na kupewa medali/tuzo?

Nawaza tuu kwa sauti kuwa John Okello hakuwa Mzanzibar lakini bado anatajwa mchango wake kwenye historia ya mapinduzi matukufu ya Zanzibar.

Sir Richard Turnbull alikuwa gavana wa kikoloni lakini anatajwa mchango wake kwenye historia ya ukombozi wa Tanganyika.

Kunani?
 
Amani Msumari,
Hakika mimi ni mtu mzima sasa mwaka kesho penye uhai nitakuwa na miaka 65.

Alhamdulilah.

Swali lako la nani alitoa magazeti yale kwenye mzungumzaji linaweza likajijibu
lenyewe kwa kuuliza swali.

Nani anaweza kuwa nä uwezo wa kukusanya magazeti katika mitaa ya Dar es
Salaam? Swali lako la pili litajibiwa nä yaliyofuatia baada ya makala ile.

Makala yangu ilijibiwa na Dr. Mayanja Kiwanuka aliyekuwa katika Sekretariati
ya Uhamasishaji Umma ya CCM Dodoma kwa kibri, kejeli nä vitisho.

Huyu Dr. Kiwanuka ndiye alikuwa kiongozi wa jopo la Chuo Cha Kivukoni lililoandika historia ya TANU mwaka wa 1981.

Kilichomkera ni kusema kuwa Waislamu walitoa mchango mkubwa katika kupigania
uhuru wa Tanganyika nä kutaja majina ya Abdul na Ally Sykes, Saadan Abdu Kandoro nä wengineo.

Jibu hilo hapo juu naamini limejibu swali lako la tatu.

Ili tuwe nä mipaka katika mjadala huu nimeacha kwa makusudi kumgusa John Okello ingawa ninayo yake mengi.
 
Back
Top Bottom