Nyamtajanyalwa
Member
- Jan 31, 2021
- 15
- 10
Tanzania ni nchi salama yenye hali nzuri ki siasa, kijamii na kiusalama, lakini kama watanzania ama mtanzania napenda kusimama kuzungumza na kushauri mambo kadhaa hasa yanayohusu vyombo vyetu vya ulinzi na usalama polisi na jeshi.
Polisi na Jeshi katika utaratibu wao wa kufanya kazi ni nani anawasimamia, ama wanafanya kazi bila taasisi inayowasimamia? Mfano wenzetu Kenya wana tume ya usimamizi wa maadili ambao hufuatilia utendaji wa polisi na wanajeshi. Ikitokea Polisi wala rushwa, hukamatwa na tume na kufikishwa mbele ya sheria.
Kwetu hapa nchini kumekuwa na matukio ya polisi, wanajeshi kuvunja sheria katika ukamataji ama ndani ya jamii, kutisha, ubabe na fujo, kudhurumu, kuendesha vyombo vya usafiri vibovu, kula rushwa, kupiga raia na kadharika, lakini wanapokamatwa husimamiwa na walewale polisi wenzao na haki haitendeki. Mfano kuna tukio lilitokea Dar es Salaam ambapo polisi aliyekuwa doria kwenda kwenye baa akanywa pombe kisha akaanza kitishia raia kwa bunduki.
Kuna mifano ya matukio ya wanajeshi kupiga raia mtaani. Je, hapa raia anapata vipi haki yake tena kesi inasimamiwa na polisi ama wanajeshi walewale?
Nashauri kiwepo chombo kinachojitegemea kitakachowasimamia polisi na wanajeshi lengo kuchangiza utendaji na weledi wao hii itapunguza malalamiko ya wananchi kwa polisi ama wanajeshi
Pili nashauri liwepo dawati katika kila kata ambalo litadumisha mahusiano mema baina ya raia na wahusika wa vyombo hivi vya usalama.
Polisi na Jeshi katika utaratibu wao wa kufanya kazi ni nani anawasimamia, ama wanafanya kazi bila taasisi inayowasimamia? Mfano wenzetu Kenya wana tume ya usimamizi wa maadili ambao hufuatilia utendaji wa polisi na wanajeshi. Ikitokea Polisi wala rushwa, hukamatwa na tume na kufikishwa mbele ya sheria.
Kwetu hapa nchini kumekuwa na matukio ya polisi, wanajeshi kuvunja sheria katika ukamataji ama ndani ya jamii, kutisha, ubabe na fujo, kudhurumu, kuendesha vyombo vya usafiri vibovu, kula rushwa, kupiga raia na kadharika, lakini wanapokamatwa husimamiwa na walewale polisi wenzao na haki haitendeki. Mfano kuna tukio lilitokea Dar es Salaam ambapo polisi aliyekuwa doria kwenda kwenye baa akanywa pombe kisha akaanza kitishia raia kwa bunduki.
Kuna mifano ya matukio ya wanajeshi kupiga raia mtaani. Je, hapa raia anapata vipi haki yake tena kesi inasimamiwa na polisi ama wanajeshi walewale?
Nashauri kiwepo chombo kinachojitegemea kitakachowasimamia polisi na wanajeshi lengo kuchangiza utendaji na weledi wao hii itapunguza malalamiko ya wananchi kwa polisi ama wanajeshi
Pili nashauri liwepo dawati katika kila kata ambalo litadumisha mahusiano mema baina ya raia na wahusika wa vyombo hivi vya usalama.
Upvote
1