Nani anajali hatima ya Tanzania?


kuna hii na hii hapa


aisee...!!
 
Naamin maskini akichoka ni mtu mbaya sana... kuna siku watu watachoka na hizi habar. ... thats y siipend siasa ya tanzania.
 
Na Edo Kumwembe

Ni nchi ya ajabu kwa mwanadamu makini kuweza kuishi. Ni nchi inayoshangaza sana, ingawa raia wake hawaonyeshi kushangazwa na matukio kadhaa yanayotokea.

Leo nimeona trafiki anakamata daladala kiukweli bila sababu ya msingi kwa maana daladala nyingi ni mbovu. Basi akawa anamwandikia faini na nikawa najaribu kuwaza ni kiasi gani daladala anapata mpaka aweze kulipa faini ya 30,000/-!
Sasa ndani ya gari wamejaa abiria hata pa kujigeuzia hamna lakini hakuna hata mmoja anayeonekana kupinga ule uonevu, na hata mama mmoja aliyejaribu kuongea unaona kabisa ni kujitutumua kwa woga wa hali ya juu usio na matendo. Ndio niakjua kuwa kwa mtaji huu katiba ya Chenge haina kizuizi!

 
Kapten Komba anasema Mzee Joseph Sinde Warioba hana maadili ndani ya BMK, wenzake wanashangilia kama mazuzu
 
kaka edo angalia kaka...punguza spidi...dakika sifuri tu unaweza kumfuata AMINA. Tulia na endelea kutojali...!! Ngoja tuwahi mechi ya Liverpool na Everton.
 
Nchi iko mikononi mwa mapanya na mafisi waeamua kuingamiza kwa kila namna huku wakisaidiwa na vitengo vyao vya maharamia wenyewe wakiviita vyombo vya dola ikiwemo mahakama, polisi na jeshi.

Nani anajali ??
 

Muda utaamua!
 
Kaka Edo nimekuelewa sana, ukiisoma lazma ujawe na simanz, labda akina naniliu........................: wale wanapatikan jengo la kijana lumumba.
I appreciate u Edo
 
Kwa kinachoendelea nchini namuona zitto bonge la mjanja,watanzania tumelala tunaamshwa ila inaonekana hatuamki leo wala kesho kwa nini asichukue chake mapema.Wapinzani wamefanya kazi kubwa sana kilichobaki ni sisi kufanya maamuzi.
 
kuna kitu kibaya sana kinainyemelea nchi yetu lakini cha kusikitisha si kikwete si pinda wala usalama wa taifa wanakiona, watu wamechoka kuvumilia madudu yanayoendelea uoga polepole unatoweka ni km wanasubiria kengele walianzishe coz tension inaongezeka kila siku miongoni mwa wananchi
 
Nani anajali wakati polisi wenyewe wanawaogopa CCM kama vile ndio waliowaajiri? Nani anajali kuhusu katiba mpya kuchezewa?Nani anajali kama Chadema wanaandamana kwa haki?Nani anajali kama kuandamana ni haki ya msingi?Nani anajali kama wakuliama wetu wananyonywa sana na serikali inayosema ni sikivu?Wacha wee wenye meno wataendelea kutafuna sana nchi hii.
 
nimesoma najikuta napata uchungu wa hali y juu n nchi yangu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…