Nani analikumbuka tukio hili vizuri?

Christopher Wallace

JF-Expert Member
Joined
Dec 8, 2015
Posts
1,479
Reaction score
3,788
Wakuu habari zenu,

Naombeni mnijuze kuhusu tukio la miaka fulani iliyopita, ambapo ilikuwa mechi ya ligi kuu ya Vodacom, golikipa wa timu flani hivi wakati anaenda kucheza krosi ya juu iliyopigwa golini mwake, ghafla alidondoka chini huku akitokwa na damu nyingi kwenye jeraha lilioonekana kama kakatwa na kiwembe, hali iliyopelekea afariki dunia.

Je, golikipa yule aliitwa nani na alikuwa anadakia timu gani? Na vipi uchunguzi ulifanyika kutokana na tukio lile? Wenye kujua karibuni mtujuze zaidi.

Natanguliza shukrani zangu za dhati.
 
Wewe jamaa una kumbukumbu sana.

Nalikumbuka hilo tukio kwa mbali sana, nakumbuka kipa ni kama alikanyagwa hivi na mchezaji aliyevaa viatu vyenye chuma chini.

Acha wenye kumbukumbu zaidi waje.

Kitambo sana hilo tukio! Vijana wa leo hawawezi kujua tukio kama hili, hivyo wakongwe waliopo humu sio mbaya wakaja kutukumbusha uzuri
 
Huyo pesambili nadhani alikuja kuacha soka la ushindani na kuamua kuwekeza nguvu kwenye shule ..inawezekana tukio lile la kusababisha kifo lilimuumiza sana..nilikua namuona akicheza timu ya chuo pale chuo kikuu mlimani daah jamaa anaupiga mwingi yule balaa ..
 
Wewe jamaa una kumbukumbu sana.

Nalikumbuka hilo tukio kwa mbali sana, nakumbuka kipa ni kama alikanyagwa hivi na mchezaji aliyevaa viatu vyenye chuma chini.

Acha wenye kumbukumbu zaidi waje.

Inasemekana Kipa na pesambili Waliruka pamoja juu na kiatu cha pesambili kama kisu kikakata sehemu ya juu ya shingo ya yule kipa..yaani yule kipa alikua kama amechinjwa na kuaga dunia... inasemekana wachache sana waliamini kama tukio lile lilikuwa la kawaida ..walilihusisha na ulozi!..
 

Mpaka leo watu wanaamini uchawi ulihusika kwa 100%
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…