Nani anapaswa kuwa na muhuri wa Serikali ya Kijiji kati ya Afisa Mtendaji na Mwenyekiti wa Kijiji?

Kwanza hujui Kiswahili; ni tafadhali. Pili kikatiba ni mwenyekiti wa Kijiji na anamiliki kijiji kama Mkuu wa Mkoa anavyomiliki mkoa na Rais kumiliki nchi ya Tanzania.
 


Huyo afisa mtendaji huwa "anatenda" kitu gani??, naye huyo mwenyekiti huwa anakalia kiti cha madaraka gani??--- kwanza tuanzie hapo.
 
Jiandae mwaka huu na wewe uapishwe na SSH kazi iendelee
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI CCM
Bwana Chawa Chila hebu tuelimishe..ni ktk mazingira gani Mihuri hii Inatumika ...wa Mwenyekiti na Mtenfaji?!
 
Haya maupumbavu aliyaleta magufuri lengo likiwa ni kuwakomoa wenyeviti wa chadema maana ukweli n kwamba watendaji ni makada wa ccm tupu. Kama mwenyekti hapaswi kuwa na muhuri uchaguzi wa serikali za mitaa huwa tunafanya wanini kwa malengo gani? Taifa hili lina maujinga ujinga mengi na majinga mengi sn yaliyoko ccm yenyewe yanalinda utawala tu si watanzania..
 
Wewe ndo hujui kabisa.
 
... hoja ya jamaa ni sawa na kuuliza DC na DED nani mmiliki wa mihuri? DED ndiye mtendaji; DC ni political figure tu yule. Au Waziri vs Katibu Mkuu; Katibu MKuu ndiye mtendaji wa Wizara.
 
Wewe ni mtu wa chama . Mimi ni mwajiriwa wa serikali wa halmashauri. Nakupatia taratibu jinsi kazi zinavyofanyika. Kama kazi za kijijini especially zinazohitaji mhuri zitafanywa na mwenyekiti hakuna haja serikali kuajiri mtendaji wa kijiji
 
Mwenyekiti hapaswi kuwa na muhuri. Mwenye ofisi ni Mtendaji wa kijiji na ndio maana yeye ndio mwenyekiti waa ulinzi na usalama wa kijiji. Yeye ndio ana migambo wa kijiji, mwenyekiti yeye wake ni wananchi lkn dola iko chini ya Mtendaji
 
Bro usiuziwe kiwanja ukapigiwa muhuri wa mtendaji wa kijiji, wew jua umepigwa hapo mkuu...

Muhuri wenye mamlaka ni wa serikali sio wa mwanasiasa. Muhuri wa serikali ni wa VEO huu wa mwana siasa hauna nguvu ki mamlaka...

Muhuri unapaswa kuwa wa ofisi na mtendaji na msimamizo wa shughuli zote za ofisi ni VEO
 
Acha kudanganya umma. Anakuaje Rais wa kijiji wakati hana mamlaka ya kumuwajibisha VEO wake. Dola iko kwa VEO
Huyo VEO na hata Rais hawawezi kumuwajibisha Mwenyekiti wa kijiji. Kijiji ni serikali kamili, yenye mammalaka na ardhi.
 
Bwana Chawa Chila hebu tuelimishe..ni ktk mazingira gani Mihuri hii Inatumika ...wa Mwenyekiti na Mtenfaji?!
Hutumika tu baaada ya mkutano mkuu kuazimia jambo, au serikali ya kijiji kuazimia jambo,,,,,kifupi hutumika kwenye mihutasali halali ambayo veo na m/kiti wameisain, hapa ndipo muhuri w serikali ya kijiji hutumika tu
 
Mtendaji ndo official anaetambuliwa na serikali mkuu hawa wenyeviti wahuni wahuni tu
Wenyekiti ni wazawa, unoko wao una kipimo, hawa watendaji ni wanoko kuliko kawaida.
Huwa wanajiona miungu ya vijiji na kata.
Hopeless!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…