Nani anayekagua na kudhibiti ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG)?

Nani anayekagua na kudhibiti ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG)?

Mmeanza kutafuta mchawi
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚

CAG hayumbishwi na wapiga makelele majukwaani
😁😁😁😁😁😁😁😁😁😁
 
Sasa umewahi kusikia report yoyote inayotokana na ukaguzi ofisi ya CAG? Nashauri kila mwaka huyo mkaguzi huru awe anatujuza matumizi pia ofisi ya CAG kwa kila mwaka. Kule nako kuna wanadammu sio malaika.
Sasa kusikia ama kutokusikia report unadhani kosa litakua la nani? Ni la CAG au bunge kupitia PAC? Kwani wewe umeshawahi kusikia CAG kakataa kukaguliwa?
 
Nilikua najiuliza hivi ofisi ya CAG na watu wake wote ni kama malaika hakuna anaeiga tabia ya watumishi wengine hapa Tanzania? tumeona mapungufu walioyaona kote huko walikokagua, nkatamani tuwe na utaratibu wakupata pia report ya ukaguzi ofisi ya CAG na watumishi wake. Mana wanapata mgao wa matumizi kutoka Serikalini.
Utakuwa ni utaratibu mzuri wakutuonyesha masurufu wao wanayatumiaje?

Ongea na Maza kama.vipi poa
 
Watashindana lakini hawatashinda" in mzee wa upako voice
Kwa Taarifa tu

Kama lengo Ni kumpata Prof Assad kupitia Ukaguzi wa Ofisi yake Basi Ukaguzi wa Ofisi yake sio Njia sahihi

CAG sio Accounting Officer wa Ofisi yake ya Ukaguzi ya Taifa

Hahusiki Na Manunuzi,Malipo wala mambo ya Utawala kwa jumla


Yeye Kazi yake Ni kukagua tu

Wazungu walipounda Mfumo Na utendaji wa CAG walishajua Fitna itakayomkumba akifanya Kazi yake vyema

Kama lengo Ni kufahamu tu utendaji na Matumizi ya Rasilimali Za Nchi kwa jumla tutafanikiwa Lakin Kama kumnasa CAG tutafute mbinu nyingine

Kuna Vigazeti vilijaribu kutafuta kashfa Kwenye Ofisi yake Na kumhusisha Lakin humu humu JF tukawaambia CAG hahusiki Na Manunuzi ya Ofisi yake kwa namna yoyote ile walipotambua hilo wakaacha Tena kufuatilia tukajua target Was Prof Assad sio kingine

Wakaibukia kwenda Hijja Bila ya Kibali Cha Ikulu nako wakakwama kwa Kuwa alikuwa Na Kibali Na alitumia Fedha zake binafsi


Kamati ya Roho mbaya irudi Kwenye kikao Kazi kutafuta mbinu nyingine

MIMI
 
Safari hii lile swali la, "Nani anayemkagua CAG?" mbona haliulizwi?

Ila mi nimekuwa nikijiuliza hilo swali kila mwaka. Maana nafahamu utaratibu wa taasisi yoyote lazima ikaguliwe.

Naamini CAG naye ana Mkaguzi wa kutoka nje (External Auditor).

Ila ni kwa nini taarifa za ukaguzi wake haziwekwi wazi, ukichukulia yeye anawaanika wengine?
 
Mkwepa Kodi kumbuka hata ofisi ya CAG inatumia pesa ya mulipa kodi ambao ni sisi wananchi. Pesa wanapewa na Serikali .Tunahitaji kujua wanatumiaje?
Halafu hao watakaokuwa wanakagua ofisi ya CAG watakaguliwa na nani, kutakuwa na msururu mrefu wa ukaguzi usio na tija
 
Kwa Taarifa tu

Kama lengo Ni kumpata Prof Assad kupitia Ukaguzi wa Ofisi yake Basi Ukaguzi wa Ofisi yake sio Njia sahihi

CAG sio Accounting Officer wa Ofisi yake ya Ukaguzi ya Taifa

Hahusiki Na Manunuzi,Malipo wala mambo ya Utawala kwa jumla


Yeye Kazi yake Ni kukagua tu

Wazungu walipounda Mfumo Na utendaji wa CAG walishajua Fitna itakayomkumba akifanya Kazi yake vyema

Kama lengo Ni kufahamu tu utendaji na Matumizi ya Rasilimali Za Nchi kwa jumla tutafanikiwa Lakin Kama kumnasa CAG tutafute mbinu nyingine

Kuna Vigazeti vilijaribu kutafuta kashfa Kwenye Ofisi yake Na kumhusisha Lakin humu humu JF tukawaambia CAG hahusiki Na Manunuzi ya Ofisi yake kwa namna yoyote ile walipotambua hilo wakaacha Tena kufuatilia tukajua target Was Prof Assad sio kingine

Wakaibukia kwenda Hijja Bila ya Kibali Cha Ikulu nako wakakwama kwa Kuwa alikuwa Na Kibali Na alitumia Fedha zake binafsi


Kamati ya Roho mbaya irudi Kwenye kikao Kazi kutafuta mbinu nyingine
Yaani umeiweka vizuri saaana tu. Team roho Mbaya wakatafute mbinu nyingine!!!
 
Naye pia anawajibika katika matumizi ya fedha za umma
 
Serikali huajiri kampuni za kimataifa kukagua ofs ya CAG
 
Na huyo atakayemkagua CAG naye atakaguliwa na nani?? --- mlolongo wa kukaguana utaendelea hadi wapi??
Anakaguliwa na kampuni binafsi ya ukaguzi (Independent Audit Firm) mara nyingi huwa ya kimataifa eg PWC

Halafu hizi kampuni binafsi huwa zinakaguana
 
Anakaguliwa na kampuni binafsi ya ukaguzi (Independent Audit Firm) mara nyingi huwa ya kimataifa eg PWC

Halafu hizi kampuni binafsi huwa zinakaguana


Okay βœ”βœ”
 
Wakuu hili bandiko la Swali.

Ofisi ya Mthibiti na mkaguzi mkuu wa Serikali hukaguliwa na nani? Naomba kufahamishwa.
 
bunge huteau auditor,ambaye hukagua na kisha kuwasilisha ripoti kwa spika.
 
Huwa kuna external auditing hufanyika kwenye taasisi ya CAG na majibu hupelekwa kwa spika na ofisi ya Rais.
 
Hata hivyo sidhani kama ofisi ya CAG ina mambo mengi? Hii ni kwa sababu haisimamii mradi wowote ule. Hawa wanaokaguliwa wanatengewa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya serikali. Kwa hiyo CAG hukagua fedha hizo kama zimetumika ipasavyo.
 
Back
Top Bottom