Uchaguzi 2020 Nani ataibuka mshindi kwenye kinyang'anyiro cha Kiti cha Ubunge 2020 jimbo la Arusha Mjini, kati ya Mrisho Gambo na Godbless Lema?

Uchaguzi 2020 Nani ataibuka mshindi kwenye kinyang'anyiro cha Kiti cha Ubunge 2020 jimbo la Arusha Mjini, kati ya Mrisho Gambo na Godbless Lema?

' Logically ' tu Kitendo cha aliyekuwa Mkuu wa Mkoa Gambo ' Kutumbuliwa ' na Rais JPM tayari ' ameshahalalisha ' Kutokushinda Kwake Ubunge.
Pia Gambo ana makando kando mengi sana. Yakiwekwa wazi ubunge atausikia kwenye tv.
 
Japo ni demokrasia ila itaniuma saana Gambo akishinda.... the guy is arrogant and mshamba wa vyeo.

Ni afadhali Lema apite tena....wanaarusha tupambane kwa namna yoyote.
Hawezi kushinda

JESUS IS LORD[emoji120]
 
Japo ni demokrasia ila itaniuma saana Gambo akishinda, the guy is arrogant and mshamba wa vyeo.

Ni afadhali Lema apite tena, wana Arusha tupambane kwa namna yoyote.
Mimi naona bora Gambo, Lema ameivuruga sana Arusha. halafu ni mtu mropokaji sana hana staha hata kidogo hafai hata kuwa mjumbe wa Shina.
 
Mimi naona bora Gambo, Lema ameivuruga sana Arusha. halafu ni mtu mropokaji sana hana staha hata kidogo hafai hata kuwa mjumbe wa Shina.
Gambo!! Visa...sifa za kijanga...arrogant....

Hapana. Afadhali Lema. Mengi yamefanyika kipindi cha Lema.

Lema sio mzuri saana ila kwa Gambo Lema ni mzuri saaana.
 
Lema amesaidia sana Arusha kwa maendeleokuiamsha serikali. Serikali imejitahidi kufanya mengi,barabara, mradi mkubwa wa maji kuwashawishi wananchi wabadili mtazamo, bado Arusha inamhitaji Lema zaidi.
 
Gambo hajapita bado maamuzi ya juu hayajampitisha subiri muvi ndio kwanza jambazi yupo anaogelea
Mkuu nipe mwanga ktk hili, unaposema bado maamuzi ya juu unamaanisha kuna uwezekano wa mamlaka za juu za chama wakapuuza maoni ya mamlaka za chini kichama na kuamua kupuuza chaguo lao na kuja na mgombea mwingine ambaye hakuchaguliwa na mamlaka za chini? Nimeona mdau mwingine nae kachangia hiki ulichokisema.
 
Godbless Lema ni Mbunge aliyemaliza muda wake na Mrisho Gambo ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha aliyetumbuliwa.

Lema anekuwa Mbunge kwa zaidi ya miaka kumi sasa lakini mara nyingi amekuwa akizitumikia kesi Mahakamani na kukosa muda wa kutosha wa kuwahudumia wapiga kura wake.

Wakati Gambo amekuwa Mkuu wa Mkoa kwa kipindi kifupi sana amabacho amekitumia kuhamasisha maendeleo kwa baadhi ya maeneo na hasa eneo la Muriet analoishi.
Kwa maneno yako tu umeshaonesha unampamba nani hapa. When you ask a question don't be biased
 
Gambo kacheza gambo ati kuuachia ukuu wa mkoa kisa kuutaka ubunge ambao kwake ni ndoto!!
 
Wakuu, sisi wakazi wa Kaskazini ambao tunaishi huku, tunaweza kukuambia majimbo ambayo Chadema inaweza kupoteza. Na kitu kingine kipya ni hali ya uchangamfu na ushabiki umepungua sana 2020. Kipindi kama hichi cha uchaguzi 2015 ukitembelea huku ilikuwa unajua Nchi inakwenda Upinzani.

Ushabiki wa kwetu Kaskazini ni wa wazi hauna kificho, iwe sokoni, Baa, kilabu cha pombe za kienyeji, mashambani, kanisani na popote penye mkusanyiko wa watu.

Na usidanganywe na mtuu yeyote, kuna hali fulani ya kusema ngoja tupigie CCM tuone labda kuna matunda. Hii ndio hali haklisi ila kuna majimbo au jimbo linalo weza kubaki Chadema.

Nguvu ya upinzani imepungua sana huku Kaskazini yote, kuna hali ya kuona tukiendelea tutatengwa.

KINYUME NA HUU USHAHIDI NI KINYUME NA HALI HALISI LABDA KUJIPA MOYO.
 
Back
Top Bottom