Lady Whistledown
JF-Expert Member
- Aug 2, 2021
- 1,147
- 2,008
Kati ya Mastaa wa Olimpiki waliotikisa Vichwa vya Habari ni Mturuki Yusuf Dikec na Mkorea Kim Ye-ji katika Mashindano ya Kulenga Bunduki ambao wote walishinda Medali za Fedha
Kim Ye-ji, amekuwa miongoni mwa Wanawake waliovutia Mashabiki wengi, amesifiwa si tu kwa ujuzi wake, bali pia mtindo wake wa Kipekee, akivalia miwani ya kisasa yenye muonekano wa Steampunk na mavazi ya kisasa. Amefananishwa na James Bond na Satoru Gojo, mhusika Maarufu ndani ya Manga Jujutsu Kaisen
Upande mwingine, Picha zilizosambazwa zaidi zinaonyesha Dikec akipiga risasi akiwa amevaa T-shati, mkono mmoja mfukoni, na miwani ya kawaida huku akiwa na uso usioonyesha hisia zozote. Amefananishwa na mtu wa kawaida anayeshindana kwenye Olimpiki, au hata muuaji wa kulipwa
Kim Ye-ji, amekuwa miongoni mwa Wanawake waliovutia Mashabiki wengi, amesifiwa si tu kwa ujuzi wake, bali pia mtindo wake wa Kipekee, akivalia miwani ya kisasa yenye muonekano wa Steampunk na mavazi ya kisasa. Amefananishwa na James Bond na Satoru Gojo, mhusika Maarufu ndani ya Manga Jujutsu Kaisen
Upande mwingine, Picha zilizosambazwa zaidi zinaonyesha Dikec akipiga risasi akiwa amevaa T-shati, mkono mmoja mfukoni, na miwani ya kawaida huku akiwa na uso usioonyesha hisia zozote. Amefananishwa na mtu wa kawaida anayeshindana kwenye Olimpiki, au hata muuaji wa kulipwa