Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 21,470
- 40,593
Kwenye nchi za Ulaya na Marekani ni ufahari mtu kununua kitu chochote kile kilichotumiwa au kumilikiwa na mtu maarufu ama mashuhuri kwa bei kubwa sana na kuhifadhi kwenye majumba yao.
Lakini ni nani kwa mfano kwa sasa anamiliki kiatu alichovaa Steven Kanumba saa chache kabla ya kufariki kwake. Hivi nguo alizovaa Diamond wakati wa ku - shoot wimbo wa Mbagala ziko wapi kwa sasa.
Nani anajua Gitaa la Mbaraka Mwinshehe lilipo kwa sasa ama mashahiri ya wimbo wa "Dada Asha" yaliyoandikwa kwa mkono na Shemu Kalenga mwenyewe nani anayo? Vitu gani alivyokuwa anamiliki Shaabani Robert wakati wa kufanya kazi zake za fasihi bado vipo na vipo kwa nani?
Jee utamaduni wa kununua vitu vya watu mashuhuri na Maarufu unaweza kuwepo hapa kwetu Tanzania?
Lakini ni nani kwa mfano kwa sasa anamiliki kiatu alichovaa Steven Kanumba saa chache kabla ya kufariki kwake. Hivi nguo alizovaa Diamond wakati wa ku - shoot wimbo wa Mbagala ziko wapi kwa sasa.
Nani anajua Gitaa la Mbaraka Mwinshehe lilipo kwa sasa ama mashahiri ya wimbo wa "Dada Asha" yaliyoandikwa kwa mkono na Shemu Kalenga mwenyewe nani anayo? Vitu gani alivyokuwa anamiliki Shaabani Robert wakati wa kufanya kazi zake za fasihi bado vipo na vipo kwa nani?
Jee utamaduni wa kununua vitu vya watu mashuhuri na Maarufu unaweza kuwepo hapa kwetu Tanzania?