Nani kafaidika kwa kufungwa jana kati ya Simba na Yanga?

Lord OSAGYEFO

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2021
Posts
3,085
Reaction score
4,890
Wapenda Michezo wote TUACHE Ushabiki Tuzungumze Ukweli juu ya Matokeo ya Michezo miwili iliyochezwa jana na Vilabu Vyetu Vikubwa kabisa Nchini SIMBA na YANGA.

YANGA ilicheza na RIVERS ya NIGERIA huko Nigeria na Matokeo ni YANGA kufungwa jumla ya GOLI 2-0.

Na SIMBA alicheza na TP MAZEMBE ya CONGO na Kufungwa Bao 1-0.

Kwa Kifupi Timu zote Zimefungwa.

SWALI
Je Kwa MATOKEO yale Je Timu gani IMEFAIDIKA Sana kwa KUFUNGWA kati ya SIMBA na YANGA?

Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 
Kati ya hizo mechi mbili ipo ilitazamwa na shabiki wengi? Hiyo ndo imeumia. Ova
 
Labda ungesema nani kapoteza lakini sio useme nani kapata faida!
 
Simba wamefaidika na mechi ya jana kwani ilikuwa mechi ya kutest mitambo.
Ulikuwa mechi ya ushindani halisi na uliona jinsi TP walivyofurahi kuwafunga Simba.

Nimefurahishwa sana na mechi ya jana ni kipimo kizuri kwa timu yangu Simba
 
Kufaidika kwenye nini embu fafanua,nani kakwambia kufungwa kuna faida?
Mkuu mechi ya jana Simba kufungwa imeongeza munkari na simba kujitathmini,Simba wangeshinda au kudroo kwenye mechi za kimataifa wangeleta u-father ,ile mechi ya jana itaongeza spirit ya gemu zinazokuja na unamfahamu atakayechakazwa game ya kwanza
 
Mkuu mechi ya jana Simba kufungwa imeongeza munkari na simba kujitathmini,Simba wangeshinda au kudroo kwenye mechi za kimataifa wangeleta u-father ,ile mechi ya jana itaongeza spirit ya gemu zinazokuja na unamfahamu atakayechakazwa game ya kwanza
Spirit bila uwezo ni kazi bure.
 
Tunaweza tusifanane mawazo ila bado tukawa wote msimbazi.

Faida tuliyopata Simba ni kuona mapungufu ya squads yetu hasa tunapokutana na timu classic kama TP Mazembe.

Sina tatizo na ligi ya ndani
Ila hofu na mashaka yasije jirudia yale ya UD Songo.

Tukija upande wa Utopolo wao walikuwa na njia ya mkato na ika feli mazima.

Angalau wangetolewa hatua inayofata wangeenda shirikisho ila sasa Mungu sio Mzee mkumba.

Sasa wao watajikita na michuano ya ndani tu

HATA WAKISHINDA KESI YA MORISSON watarudishwa CAF[emoji16]
 
Matokeo ya jana ni faida kubwa kwa Simba. Kivipi?
-Simba kufungwa na TP Mazembe ni kipimo cha kuiamsha simba aongeze bidii, mambo sio mchezo mchezo.
-Kufungw kwa Yanga ilikuwa ni kufurahi kwa Simba, maana Yanga hatakuwepo tena mashindanoni kimataifa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…