Nani kati ya Makamu wa Rais na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi analidanganya taifa kuhusu suala la Samaki?

Nani kati ya Makamu wa Rais na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi analidanganya taifa kuhusu suala la Samaki?

Kwani ni lazima kila jambo litatuliwe Kwa matamko kwanza? Mambo mangapi serikali inayadhibiti bila raia kujua?
Mimi sijasema "kila jambo litatuliwe kwa matamko kwanza", inawezekana ni akili yako ndiyo inayokutuma wewe kufikiri hivyo.
 
Kikubwa hapa ni tatizo la mawasialiano ndani ya Serikali! ingawa taarifa ya Makamu wa Rais zina uhakika zaidi kwakuwa anazungukwa na taarifak kutoka vyanzo vingi vya usalama
Hapana.

Tatizo siyo "mawasiliano" pekee, bali tatizo kubwa ni kushindwa kufanya kazi kwa taasisi zilizopewa majukumu kulinda afya za wananchi na mambo mengine.

Hayo mambo mengine ya "ubepari" n.k., huo ni mjadala mwingine, ambao nao ningekataa hiyo dhana yako unayoiamini wewe.
 
Hapana.

Tatizo siyo "mawasiliano" pekee, bali tatizo kubwa ni kushindwa kufanya kazi kwa taasisi zilizopewa majukumu kulinda afya za wananchi na mambo mengine.

Hayo mambo mengine ya "ubepari" n.k., huo ni mjadala mwingine, ambao nao ningekataa hiyo dhana yako unayoiamini wewe.
Sawa, mjadala mzuri ni pamoja na ww kutoa mawazo mbadala!

Makamu wa Rais anavyanzo vingi vya taarifa kuliko waziri! Nalo unabisha??

Nilizungumza athari za taarifa aliyotoa Vice katika uchumi na impact yake!

Mifano niliyotoa, juu ya silaha na mapebari, ni kuonesha tu namna gani nchi zilizoendelea ziko makini na mambo ya uchumi na fedha
 
Sawa, mjadala mzuri ni pamoja na ww kutoa mawazo mbadala!

Makamu wa Rais anavyanzo vingi vya taarifa kuliko waziri! Nalo unabisha??

Nilizungumza athari za taarifa aliyotoa Vice katika uchumi na impact yake!

Mifano niliyotoa, juu ya silaha na mapebari, ni kuonesha tu namna gani nchi zilizoendelea ziko makini na mambo ya uchumi na fedha
Duh, mkuu 'Lubengera', unajitahidi sana kunivuta kwenye mjadala huu mwingine, ambao kwa kweli kwa sasa sina muda mzuri nao.

Lakini itoshe tu kukueleza kwamba, biashara ya silaha, ni biashara, kama zilivyo biashara nyingine zote. Mnunuzi anayo hiari ya kununua anapohitaji. Hili linalojadiliwa hapa ni tofauti kabisa. Hii siyo biashara iliyohalalishwa na sheria yoyote, in fact inakiuka sheria zote katika nchi yoyote ile.

Sasa kama bado hunielewi kwa maelezo haya mafupi ambayo nimeyafanya 'direct', hapo utakuwa na jambo jingine kabisa.
Kuhusu hilo la Makamo wa Rais kuwa na "vyanzo vingi", unataka nibishe kitu gani katika hilo! Kuwa na vyanzo vingi vya kupata habari, ndiyo iwe sababu ya kuficha jambo la hatari kwa raia? Ili habari ziwe za chini chini na biashara inayokiuka sheria zote iendelee?
Haya ni mawazo ya namna gani haya!
 
Duh, mkuu 'Lubengera', unajitahidi sana kunivuta kwenye mjadala huu mwingine, ambao kwa kweli kwa sasa sina muda mzuri nao.

Lakini itoshe tu kukueleza kwamba, biashara ya silaha, ni biashara, kama zilivyo biashara nyingine zote. Mnunuzi anayo hiari ya kununua anapohitaji. Hili linalojadiliwa hapa ni tofauti kabisa. Hii siyo biashara iliyohalalishwa na sheria yoyote, in fact inakiuka sheria zote katika nchi yoyote ile.

Sasa kama bado hunielewi kwa maelezo haya mafupi ambayo nimeyafanya 'direct', hapo utakuwa na jambo jingine kabisa.
Kuhusu hilo la Makamo wa Rais kuwa na "vyanzo vingi", unataka nibishe kitu gani katika hilo! Kuwa na vyanzo vingi vya kupata habari, ndiyo iwe sababu ya kuficha jambo la hatari kwa raia? Ili habari ziwe za chini chini na biashara inayokiuka sheria zote iendelee?
Haya ni mawazo ya namna gani haya!
Itoshe kusema, Vice hakupaswa kutoa taarifa hii hadharan maana ina impact kubwa hata katika biashara na uchumi
 
Itoshe kusema, Vice hakupaswa kutoa taarifa hii hadharan maana ina impact kubwa hata katika biashara na uchumi
Kwa hiyo ulitaka sisi raia, tuendelee kufa kwa kansa?🥺
 
Itoshe kusema, Vice hakupaswa kutoa taarifa hii hadharan maana ina impact kubwa hata katika biashara na uchumi
Naona hukuelewa nilichoeleza hapo juu, pamoja na wewe kunipa 'like' kama ulivyofanya!

Basi shikilia msimamo wako huo, pamoja na kwamba ni msimamo potofu.
 
Jiulize kwanza: Philipo yeye kalitoa wapi jambo hilo, maana hawezi kuamka tu usingizini na kwenda kulitamka alivyofanya.

Na kama haitoshi, inakuwaje Makamu akatoa taarifa nzito kiasi kile bila kuwasilianan na wizara husika katika serikali yake?
Hili ni jambo la kushangaza sana]
Sasa hicho ndicho kilichofanyika. Angewasiliana na Wizara husika Naibu Waziri asingeongea aliyoongea.
 
Naibu Waziri kajibu kisiasa, anafanya utani na mzaha kwenye uhai na maisha ya watanzania, nadhani Ulega must resign haraka sana, Mh. Rais aunde tume huru haraka kuchunguza hili suala, ni jambo hatari sana, huku Naibu Waziri akijibu kisiasa wala hajali kitu.
Mh. Makamu wa Rais atakuwa sahihi na najua ana taarifa zote, huku wizara na mawaziri wake wakikaa kimya na kula raha tu, mfano huyo Ulega ni bomu kweli huyo, hafai kabisa hata kuwa mbunge tu, yaani Naibu Waziri anajibu kirahisi tu kwa jambo hatari hivi tena anapinga alichosema Boss wake yaani Makamu wa Rais..
Naibu Waziri ni mtaalam wa hayo mambo. Hajajibu kisiasa. VP ndiye aliyekurupuka
 
Katika siku za Karibuni, zimetolewa kauli mbili tofauti toka kwa viongozi wakubwa kabisa Katika Serikali yetu ya CCM.

Kwanza ilitolewa kauli na Makamu wa Rais, Dkt. Philipo Mpango, akiwa jijini Mwanza kikazi, ambaye aliagiza vyombo vyote vinavyozibiti maji ya kuoshea maiti yenye dawa ya chloroform, aliyodai kuwa yanatumika kuhifadhi samaki, kwa hiyo akaelezea wasiwasi wake kuwa, kuna ongezeko kubwa la wagonjwa wa saratani nchini, ambao kwa maelezo yake, ongezeko hilo linatokana na ulaji huo wa samaki, ambao wanahifadhiwa kwa kutumia maji hayo ya kuhifadhia maiti.

Baada ya siku chache, akaibuka Naibu Waziri wa Mifugo na uvuvi, Abdallah Ulega, tena ndani ya Bunge letu jijini Dodoma, akikanusha vikali taarifa hiyo ya Makamu wa Rais, Dkt Philipo Mpango, aliyoitoa na kuiita kuwa ni ya uongo na ya kufikirika!

Watanzania tunataka kuujua ukweli, Katika hili jambo nyeti Sana, linalohusu uhai wetu, je ni Makamu wa Rais, Dkt Philipo Mpango, au ni Naibu Waziri wa Mifugo na uvuvi, Abdallah Ulega, ambaye amelidanganya Taifa letu?

Kuliacha jambo hili hivi hivi tu, ni kuhatarisha uhai wa mamilioni ya watanzania, ambao ni watumiaji wa samaki hao, iwapo kauli ya Makamu wa Rais, Dkt Philipo Mpango itakuwa ya kweli.

Mimi binafsi ninaamini kuwa, kauli iliyotolewa na Makamu wa Rais, Dkt Philipo Mpango, siyo ya kukurupuka na itakuwa na ukweli, kwani atakuwa amepewa taarifa za uchunguzi na wataalamu wa wizara hiyo ya Mifugo na uvuvi.

Kwa kuwa jambo hili ni kubwa Sana na linahusu uhai wa mamilioni ya raia wa nchi hii, wanaotumia bidhaa hiyo ya samaki, ninapendekeza kuwa iundwe Tume huru ya kulichunguza jambo hili na matokeo ya Tume hiyo, yatolewe hadharani kwa Umma wa watanzania na itakapogundulika mmoja wao, Kati ya Makamu wa Rais, Dkt Philipo Mpango au Naibu Waziri wa Mifugo na uvuvi, Abdallah Ulega, amelidanganya Taifa, basi awajibike kwa kujuzulu wadhifa wake mara moja, kwa kuudanganya Umma wa watanzania 🥺

Mungu ibariki Tanzania.
Tume tena! Ya watu wangapi? Ifanye kazi siku ngapi? Iwajibike kw nani? Ilipwe kiasi gani? Na je ikikuta Mh. Mpango ndo mwongo isemeje? Kwamba Makamu wa Rais wa Tz ni muongo! Au huyo mwingine!?...nk. Ni hivi, ktk nchi yenye viongozi wenye kujiheshim na wawajibikaji, mambo haya hayahitaji tume. Hakuna kutofautiana hadharani-mkubwa na mdogo, kwamba ikiwa mdogo ana la kumpinga bosi wake, anajiuzulu kwanza halafu akaelezee kwa nni baadae. Ona ss, watu wanajadili uwezekano wa Mak. Rais kuwa aliropoka au muongo na hawezi tena kutoa ufafanuzi wa aliyosema! Haya matume yanakula muda, yanakula kodi zetu bure, yanaongeza tozo na hayana tija... fatilia uone
 
Linapokuja suala la usalama wa watu, biashara inawekwa nyuma.

Dunia nzima inazungmzia transparency,wewe unaongelea mambo kufanyika gizani, kisa eti biasharara! Crap!

Kama Dr. Mpango ana taarifa sahihi, amefanya sahihi sana kuiweka taarifa hiyo public. Ni kweli ilikuwa inajulikana kuwa wagonjwa wa saratani, zaidi ya 60% wanatoka kanda ya Ziwa. Lakini sababu haijulikani. Huo ndio ukweli. Watu wa Kanda ya Ziwa, ambao ndio waathirika wakuu, wanatakiwa kujulishwa na mamlaka za Serikali, sababu ni nini?

Hypothesis ya kwanza imekwishatolewa. Utafiti wa kina unatakiwa kufanywa, lakini kwa kuwa matokea yanaweza kuchukua miaka, kipindi hicho, wananchi wanatakiwa kuchukua tahadhari. Kwa nchi zinazowajibika, kipindi chote cha kusubiria matokeo ya utafiti, ulaji wa samaki hao na biashara ya samaki hao, vingedhibitiwa kwa kiasi kikubwa mpaka uhakika wa jambo hili utakapopatikana.

Kwa sasa, tahadhari imekwishatolewa kinamna, unayesema mambo hayakustahili kuwekwa hadharani, endelea kula samaki hao bila tahadhari yoyote, wanaojali afya zao wachukue tahadhari.
Ndani ya polisi Kuna vitengo vingi mpaka vya udukuaji na ushushushu. Yeye kama mkubwa ameshindwa Nini kutuma kikosi kazi Cha kupeleleza na kudhibiti?
Inawezekana ni kweli, unadhani wataacha kutumia hizo kemikali kwa matamko ya majukwaani?
Je Nchi za nje wakapiga marufuku ya usafirishaji minofu kutoka Tanzania, watanzania wakakosa ajira, huyu atalisha familia zao?
Matamko yake Yana athari mbaya zaidi kuliko faida.

Eti "transparency" Dunia Yako hii!
Corporate espionage isingekuwepo kama pangekuwa na transparency

Kwa hiyo wewe unaacha kula Samaki, unajiona unachukua tahadhari, hongera.
Ila nikwambie tu, hakuna kilicho na usalama kuanzia kuku unaokula, nyama ya buchani, mayai, njegele unazokula, maharage, sembe n.k Mimi nipo kwenye sekta ya Kilimo na ufugaji miaka 8. Kuna matumizi ya madawa ambayo hayafuati masharti. Labda uwe unajilimia chakula chako. Take care mwerevu!
 
Sasa hicho ndicho kilichofanyika. Angewasiliana na Wizara husika Naibu Waziri asingeongea aliyoongea.
Hapana.
'Protocol' haipo hivyo. Katika ziara hiyo Wizara husika ilitakiwa iwe imejiandaa, na katika msafara huo kuwe na mwakilishi, kama siyo huyo huyo Naibu waziri mwenyewe kuwepo hapo na kumfahamisha Makamu usahihi wa mambo kama upo.Makamu wa rais hawajibiki kwenda kutafuta taarifa wizarani. Wewe vipi bhwanah!
 
Tume tena! Ya watu wangapi? Ifanye kazi siku ngapi? Iwajibike kw nani? Ilipwe kiasi gani? Na je ikikuta Mh. Mpango ndo mwongo isemeje? Kwamba Makamu wa Rais wa Tz ni muongo! Au huyo mwingine!?...nk. Ni hivi, ktk nchi yenye viongozi wenye kujiheshim na wawajibikaji, mambo haya hayahitaji tume. Hakuna kutofautiana hadharani-mkubwa na mdogo, kwamba ikiwa mdogo ana la kumpinga bosi wake, anajiuzulu kwanza halafu akaelezee kwa nni baadae. Ona ss, watu wanajadili uwezekano wa Mak. Rais kuwa aliropoka au muongo na hawezi tena kutoa ufafanuzi wa aliyosema! Haya matume yanakula muda, yanakula kodi zetu bure, yanaongeza tozo na hayana tija... fatilia uone
Tume. Tume ya nini, kuchunguza uzembe?

Jambo sahihi hapa ni kuwajibisha watendaji wasiotimiza wajibu wa kazi zao, basi.
 
Hapana.
'Protocol' haipo hivyo. Katika ziara hiyo Wizara husika ilitakiwa iwe imejiandaa, na katika msafara huo kuwe na mwakilishi, kama siyo huyo huyo Naibu waziri mwenyewe kuwepo hapo na kumfahamisha Makamu usahihi wa mambo kama upo.Makamu wa rais hawajibiki kwenda kutafuta taarifa wizarani. Wewe vipi bhwanah!
Ukisema kila ziara ya VP viongozi wa Wizara mbalimbali wawepo kwenye msafara hakuna kazi itakuwa inafanyika na kutakuwa na matumizi mabaya sana ya fedha. Katika mikoa mingi karibu kila sekta ipo sasa Manaibu Waziri wangapi waongozane na VP ili kutoa maelezo? Yeye VP hata kama aliambiwa au kusikia kuhusu hiyo issue HAKUPASWA kuitangazia dunia kuwa kuna kitu hiki kinafanyika bila kupata ufafanuzi wa kina kutoka sekta husika. Mara nyingi kama uko sehemu ukapata taarifa za namna hiyo na huna uhakika huwa tunasema serikali imelichukua na italifanyia kazi then anatuma wasaidizi wake au PM kuhoji suala hilo kwenye Wizara husika.
 
Ukisema kila ziara ya VP viongozi wa Wizara mbalimbali wawepo kwenye msafara hakuna kazi itakuwa inafanyika na kutakuwa na matumizi mabaya sana ya fedha. Katika mikoa mingi karibu kila sekta ipo sasa Manaibu Waziri wangapi waongozane na VP ili kutoa maelezo? Yeye VP hata kama aliambiwa au kusikia kuhusu hiyo issue HAKUPASWA kuitangazia dunia kuwa kuna kitu hiki kinafanyika bila kupata ufafanuzi wa kina kutoka sekta husika. Mara nyingi kama uko sehemu ukapata taarifa za namna hiyo na huna uhakika huwa tunasema serikali imelichukua na italifanyia kazi then anatuma wasaidizi wake au PM kuhoji suala hilo kwenye Wizara husika.
Kwa hiyo una maana ya kwamba hao walioko mikoani hawajui yaliyoko woizarani?
Kama walikuwepo, mbona hawakutoa ufafanuzi ili Makamo asiongelee jambo ambalo hana ukweli nalo?

Bado unajisikia wizara yako haitimizi wajibu wake? Unatetea kitu gani hapa kama siyo uozo!
 
Kwa hiyo una maana ya kwamba hao walioko mikoani hawajui yaliyoko woizarani?
Kama walikuwepo, mbona hawakutoa ufafanuzi ili Makamo asiongelee jambo ambalo hana ukweli nalo?

Bado unajisikia wizara yako haitimizi wajibu wake? Unatetea kitu gani hapa kama siyo uozo!
Nakwambia tena hivi, VP alikurupuka. Hayo mambo hayaendi hivyo. Kama VP alisikia hayo maneno huko mitaani na hakuuliza watu walioko kwenye sekta iwe huko Halmashauri au Wizarani akayaongea hadharani amekurupuka. Period.
 
Back
Top Bottom