Jiulize kwanza: Philipo yeye kalitoa wapi jambo hilo, maana hawezi kuamka tu usingizini na kwenda kulitamka alivyofanya.
Na kama haitoshi, inakuwaje Makamu akatoa taarifa nzito kiasi kile bila kuwasilianan na wizara husika katika serikali yake?
Hili ni jambo la kushangaza sana.
Sasa turudi kwenye hiyo dawa yenyewe: Haiwezi ikawa chloroform. Chloroform haitumiki kuhifadhi maiti.
Hata hivyo, chloroform ni dhaifu zaidi katika kusababisha saratani. Miaka siyo mingi sana iliyopita, chlorofrm hiyo hiyo ilikuwa ikitumika kuchanganyia dawa za binaadam, na imetumika kwa muda mrefu kiasi, na hapakuwa na wingi wa hiyo saratani. Ndiyo, baadae inadhaniwa kuwa na madhara hayo, lakini siyo kwa kiasi hicho cha kutia woga.
Bila shaka dawa inayozungumziwa hapa itakuwa Formaldehyde (Formalin), ambayo ndiyo hasa kazi yake ni kuhifadhi maiti, na haijawahi hata mara moja kutumika kwa matumizi ya binaadam kwa kumeza au kupaka. Inajulikana zaidi kuwa na madhara ya kusababisha saratani.
Na mwisho: Haya yanayotokea ni dalili wazi kabisa za taasisi zetu kutofanya kazi ipasavyo. Haiwezekani kabisa watu wawe wanatumia vitu hatarishi kwa maisha ya binaadam kirahisi namna hii bila kujulikana.
Hii ni dalili moja wapo ya nchi yetu kuwa 'Banana Republic' kwelikweli.
Ndiyo maana gonjwa hatarishi kabisa linaingia nchini, halafu wanasiasa ndio wanakuwa mstari wa mbele kupinga uwepo wa gonjwa lenyewe!
Si ajabu hata 'Panya Road' wanatamba!
Sijui ni jambo lipi tunaloweza kujivunia kama nchi kwa sasa. Labda mafanikio ya CCM kuwalaza akili waTanzania. Katika hili hakuna mfano unaotufikia sisi.