Nani kawadanganyeni kuwa Uganda Cranes ( Timu ya Taifa ya Uganda ) itatuachia mwakani mwezi Machi kuna Uwanja wa Taifa?

Huyu kocha hata kama ikatokea muujiza tukamchapa Uganda. Afungashiwe virago tu.

Jibu alilotoa "...stars sio simba" limeonyesha anashida ktk kumanage wachezaji. Pia ana mbinu dhaifu sana uwanjani.

Na hapo alipoitaja Simba SC yangu ndiyo nimezidi ' Kumchukia ' maradufu sasa.
 
Ila hii ni dharau kubwa sana Amunike katufanyia..

Hivi kweli kwa squad hii tusingepata hata goli moja?

Jamaa hafai kuwepo / kurudi Tanzania apitilize kwao kabisa.
 
mbona kwao walishindwa????
 
kwenye miaka ya 2007 au 2008 hivi,ilikua tumpige au tudroo na msumbiji pale shamba la bibi,ilitwende afcon dah kilichotokea ni aibu ya macho.........
Sasa nikivuta picha ya Okwi na pale taifa anavyofunga anavyotaka naiona nafasi yetu ya kutokea nikubwa sana...........

Amunike asibishane na ukweli najua anataka kutengeneza Timu Bila kutumia wachezaji wa klabu za kulwa na Doto Ila nimkumbushe tu Hao Kulwa Na Doto ndio wanamiliki wachezaji wenye UWEZO WALAU KUTUVUSHA TULIPO

Ila tuombe lile bomba la mafuta pale Tanga mpaka Uganda Lihusike katika kutoa tokeo
 
Naona tumetoka Kufa Maseru nchini Lesotho na hatimaye sasa Rais Museveni anakuja Kushuhudia Maziko yetu rasmi pale Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam nchini Tanzania tarehe 22, March 2019.
Ni hatari sana.. jamaa kashatoa ruksa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…