Nani kubeba kombe Champions League, Pia nani atabeba Europa League

Nani kubeba kombe Champions League, Pia nani atabeba Europa League

Paris amepitia njia ngumu sana toka makundi alikuwa na man utd, leipzig, akaja barca, munich, city, final.. akiiingia fainali huyu ni true champion [emoji817]

Chelsea ni vice versa of paris tangu makundi amekutana na vibonde tupu akaja mchovu atletico, porto.. hata angekuwa arsenal angefika semi kupitia uchochoro huu wa chelsea

Europa chama langu man halitabiriki likiwa nyumbani ila away am confident [emoji817] linashinda. linaweza kupoteza kwa roma hivi hivi
 
Madrid na Man city final.. Mmoja wao bingwa

Roma na Villarreal final.. Villareal bingwa
 
Anayemtoa Madrid au Barcelona ndio Mara nyingi anakuwa bingwa! So Kwa kuwa PSG alimtoa Barcelona probably anayo nafasi ya kutwaa ndoo!
Otherwise, Madrid achukue ndoo au atakayemtoa Madrid.

Hiyo ndio nadharia ya atakavyopatikana bingwa Wa uefa msimu huu! Save this for the reference.
 
Nadhani PSG ana moto nalo zaidi, kama atafika fainali atalitwa kufika fainali mara 2 mfululizo kisha asilibebe hesabu zangu zinakataa.. 32%

Man city sio wa kubezwa wana timu nzuri mnoo 30%

Madrid wao hili kombe ni kama wamelioa vile, japo sina uhakika kama anaweza kumfunga man city fainali, labda kidogo psg wakikutana fainali.. Shida psg hawana kiungo cha kushindana na madrid wala man city, wao wanategemea zaidi ubora wa strikers wao pale juu, na kidogo ulinzi, wakiomba dua golikipa wao Navas aamke vizuri awastili.. Na hili ni tatizo siku wakikutana na man city, watapata tabu saana
Madrid 28%

Chelsea asibezwe saana kwenye mpira lolote linaweza kutokea 10%
Umedadavua vyema kabisa hasa PSG. Ila kwa ile forward ya PSG City anaweza kutobolewa kirahisi sana. Shida ya City huwa ni kuruhusu Counter Attack kwa maana huwa wanaacha mashimo mengi sana. Angalia jana goli walilofungwa na Chelsea, Angalia Match walilofungwa na Leeds United au Match waliyofungwa na Manchester United. City huwa wakikutana na timu bora kwenye Marking hupata tabu sana.
Ila PSG nao wazembe sana kwenye kutumia nafasi. Final iliyopita waliadhibiwa na Bayern kwa ujinga wao wa kushindwa kutumia clear chances zaidi ya 3 then Bayern wakatumia moja tu tena ngumu.
Ubingwa mgumu sana kuutabiri huu.
Yeyote atachukua.
 
Back
Top Bottom