Nani kwa Hakika alistaili ufalme wa rhymes ~2004?

Nani kwa Hakika alistaili ufalme wa rhymes ~2004?

Pure_sapiens

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2016
Posts
2,228
Reaction score
2,064
Habari zenu!
Hasa wapenda burudani wa mziki huu wa bongo fleva miondoko ya hip hop kwa Hapa Tz.
Unajuwa miaka ya zamani kidogo kuanzia 1997~2009 mziki wa Tanzania ulipiga hatua kubwa sana katika uandishi wa mashahiri kuliko miaka hii ya hivi karibuni,ingawa katika miaka hiyo nilikuwa mdogo lakini nilipenda sana kusikiliza miondoko ya hip hop kutoka nyumbani Tanzania.
Wasanii kama Afande Sele,Solo Theng(traveler),Juma nature,East Coast team,Balozi,Imamu Abasi,Adili,Fanani,Soggdog,Jaymo,Sugu,na wengine wengi hawa walifanya nipende mziki wa hip hop kwa Bongo.

Lakini nakumbuka mwaka 2004 kuliandaliwa shindano lililopewa jina la mfalme wa rhyme ambalo liliteka vichwa vya habari Tanzania na nchi Jirani.Nakumbuka katika mwaka 2004 nilikuwa darasa la 4 lakini nilikuwa nafuatilia kwa umakini sana Haya mashindano.Wasanii wengi sana walishiriki katika shindano la mfalme wa rhymes ambalo liliandaliwa na Global publisher(Erick shigongo).Kama yalivyo mashindano mengine yale lazima apatikane mshindi hivyo katika mashindano Haya msanii Afande sele Aliibuka mshindi.
Kwa umri wangu sikujuwa kama mshindi Alipatikana kwa njia gani?Kama kupiga kura au alichaguliwa na majaji(ushindi wa mezani).Lakini ninachojuwa baada ya kutangazwa Afande sele kuwa ni mshindi kuliibuka migogoro,sintofaham,chuki,na wivu miongoni mwa wasanii hivyo ule umoja na urafiki ulipotea kabisa.

Kwa kuwa uongo ukisemwa sana kwa kurudia rudia bila kukanushwa hugeuka/huwa kweli na kwa kuwa historia haibadiliki ila inasahihishwa basi ni nani alistaili kuwa mshindi wa rhymes kwa mwaka ule 2004.Kumb ilifanyika mwaka mmoja tu na hii kutokana na matatizo yaliyojitokeza.
Karibuni.
IMG_3105.JPG
IMG_3107.JPG
Hii ilikuwa ni moja ya collabe kali kabisa iliyokutanisha vichwa 3 ndani ya track moja.Mtazamo By Afande sele ft Joseph Haule na Solotheng.
 
Kwa mtazamo wangu Fid Q nae alikuwa mstahili na kilichombeba zaidi afande ni wimbo wa Darubini kali ukiacha mbali mtazamo
 
Afande sele alideserve... ila solo thang pia mkali sana.. profjizze.... pia mkali......
Afande sele aliimba nyimbo moja na watu pori mpaka leo kila siku naiskizila.. inaitwa nafsi ya mtuuuu...

Mwingine anakuja kwako anashida tena mikono nyuma amekondaa,
Unamtazama kwa huruma na kukwepa lawama unasema looo lazima nimpige tafuu, kwa moyo mkunjufu, tena bila kujali skendo zake za uhalifuu, na uchafuu wa mwili na tabia unakua nae unaishi nae kama waifuuu.. kumbe ni naifuu anakusifu machoni moyoni anakusanifuuuu..

Aiseeee acha kabisa hii.verse
 
Ulikuwa unafuatilia kwa ukaribu?ulikuwa unafuatilia nini kama vigezo vilivyotumika kumpata mshindi huvijui?

Kipindi Haya mashindano yanafanyika nilikuwa katika umri mdogo hivyo hata uwezo wa ku perceive mambo makubwa in detail sikuwa nao.
Lakini kwa wakati ule lazima niseme nilikuwa nafuatilia kwa ukaribu kulingana na umri wangu
 
Afande sele alideserve... ila solo thang pia mkali sana.. profjizze.... pia mkali......
Afande sele aliimba nyimbo moja na watu pori mpaka leo kila siku naiskizila.. inaitwa nafsi ya mtuuuu...

Mwingine anakuja kwako anashida tena mikono nyuma amekondaa,
Unamtazama kwa huruma na kukwepa lawama unasema looo lazima nimpige tafuu, kwa moyo mkunjufu, tena bila kujali skendo zake za uhalifuu, na uchafuu wa mwili na tabia unakua nae unaishi nae kama waifuuu.. kumbe ni naifuu anakusifu machoni moyoni anakusanifuuuu..

Aiseeee acha kabisa hii.verse

Kibongo bongo hatuna utamaduni wa kuwapa heshima legendary kama hawa ila tunawadhihaki na kuwakejeli ila waliweka misingi imara ya huu mziki.
 
Back
Top Bottom