Nani kwa Hakika alistaili ufalme wa rhymes ~2004?

Nani kwa Hakika alistaili ufalme wa rhymes ~2004?

Mfalme wa rhymes ilikuwa inachukuliwa kwa nyimbo za ndani ya mwaka, sio uwezo wa mwanamuziki kiujumla, ni wimbo fulani katika mwaka husika ndio unashindanishwa.
Sasa kwa mwaka 2003/2004 darubini kali haikuwa na mpinzani tizama mistari yake mule, kidogo nhoma nyingine kali nadhani ni msinitenge ya prof jize..
Fid q hakuwa na ngoma kali msimu huo..
Ila fid alikuwa anaelekea kuchukua ya mwaka 2005 na ngoma yake ya mwanza mwanza kama sikosei, ila watu ndio wakaleta zengwe shindano likafa na wasanii walileta utata baada ya kuona mshindi ameshajulikana..
Ukisikiliza ngoma ya nako2nako na fid inaitwa hakuna mahali kama, fid ameongelea hii ishu.

Darubini ilitoka baada ya kupewa tayari ufalme was rhymes lakini kwenye mashindano aliingia na wimbo mtazamo ambao aliwashirikisha wasanii Wawili.Afande sele alibebwa sana katika ushindi ule kwa kuchukuwa wimbo ambao tyr alibebwa pia
 
mbona mnakazania wimbo wa mtazamo, afande kwenye lile shindano aliingia na wimbo darubini kali na sio mtazamo

Nakataa Kipindi ambacho Afande anachukuwa Ufalme wa rhymes wimbo wa tarubini kali ulikuwa hautoka Mkuu.
Darubini ulitoka baada ya kupewa ushindi
 
Prof J alistahili usinitenge ilikuwa kali na ujumbe wa kutosha, darubini kali ulikuwa wa kawaida tu
 
Wakati ule AfandeSele alikuwa juu ya wote!
Mimi nilikuwa form 5 nakumbuka kila kitu.

Kwnye mtazamo kuna mstari anasema " mimi naogopa sana tunavyotukanana"

"Isije huko mbele tukachinjana"

Wakati huo alikuwa amechinjwa Steve 2k jamaa akaonekana kama nabii!

Afande alikuwa kileleni bhana, watu waliridhika japo haiwezekani wote wafurahie, fid q enzi hizo Alikuwa anatumbua tu chunusi!
 
Verse ya jay kwenye wimbo upi
Alistahili professor Jay. Afande alikua anaujua fika uwezo wa professor, hata wakati wa kurecord 'mtazamo' afande alifuta original verse yake baada ya kuisikiliza verse ya professor Jay.
 
Darubini ilitoka baada ya kupewa tayari ufalme was rhymes lakini kwenye mashindano aliingia na wimbo mtazamo ambao aliwashirikisha wasanii Wawili.Afande sele alibebwa sana katika ushindi ule kwa kuchukuwa wimbo ambao tyr alibebwa pia
Mzee mwenzangu hebu tuwekane sawa mtazamo imetoka mwaka gani na darubini kali imetoka mwaka gani?
Nakumbuka mkali wa ryhmes afande sele aliperfom darubini kali.
Kidhati kabisa afande sele alistahili.
 
Alistahili professor Jay. Afande alikua anaujua fika uwezo wa professor, hata wakati wa kurecord 'mtazamo' afande alifuta original verse yake baada ya kuisikiliza verse ya professor Jay.
Mbona sasa hakuingia hata top 5? Kama sijakosea top 5 ilikua;
1.Afande Sele
2.Inspector Harun
3.Man dojo na Domokaya
4.Mwanafa
5.JayMo
 
Uzee huu nshasahau..
Kama sjamix ma file,angeshinda profesa jay na wapili awwle afande,but siku ya shindano profesa akasahau mistari stejini then afande akapeta na point lukuki.
 
Back
Top Bottom