Nani mwenye historia ya John Rupia, Mwana TANU na tajiri wa kwanza mweusi mitaa ya Kariakoo?

Nani mwenye historia ya John Rupia, Mwana TANU na tajiri wa kwanza mweusi mitaa ya Kariakoo?

Nakukumbusha; Alikuwa mmoja wa Waswahili wa mwanzo kabisa kujenga mjengo wa ghorofa katika makutano ya Barabara ya Kitchwele (sasa Uhuru) inapokutana na Msimbazi
 
Mwenye ndondoo za mzee wetu huyu marehemu atushushie..inasemekana alikuwa mfadhili wa TANU..na tajiri wa kariakoo.
Nasikia alikuwaga babu yangu ila baada ya kutusua akampiga pin bibi na kuoa mwinginee.
Aaaaah aah kidding.......!
 
Kuna ukoo wa Lupia huko Tabora, wana macho makubwa kidogo pia ni waongeaji sana,

Bila shaka itakuwa ni sehemu ya familia yake,
Ila hawa nnao wajua mimi wanamaisha ya kawaida sana,
Wengi ni walimu.
 
Nimeweka mkristu kusudi tuu..ili wakija wale wanaotuaminishaga Uhuru walidai wazee wa mitaa wa gerezani tuu kariakoo wasome
Mkristu Mkatoliki. Kanisa ni Chuo cha Uongozi
 
Rekebisha hilo neno, badala ya MKRISTU andika MKRISTO. kuna tofauti kubwa sana kati ya mkristU na mkristO. Ova
 
Rekebisha hilo neno, badala ya MKRISTU andika MKRISTO. kuna tofauti kubwa sana kati ya mkristU na mkristO. Ova

Arekebishe neno Mkristu aweke “MTANZANIA” au “MTANZANIA MWEUSI” maadui walijaribu kutugawa kwa makabila wakashindwa wakajaribu kwa dini pia wakashindwa ila sasa wanarudi kijanja(re-engineering) kujaribu tena kwa dini!!!watagonga mwamba(strong and hard rock)!
 
Sasa si ungemwambia akupe na hizo dondoo nyingine boss...maana Sisi hatumjui vizur huyo jamaa
 
umeandika kitu ambacho una uhakika nacho ila kwa kukufumbua macho kabla ya kupata uhuru tulikuwa na watanzania weusi matajiri mmoja wao ni Marehemu Mzee Lupembe wengine wataongezea wanaowafahamu huyu pia alikuwa miongoni mwa watanzania waliomchangia Mw. Nyerere tiketi ya kwenda umoja wa mataifa
 
Mwenye ndondoo za mzee wetu huyu marehemu atushushie..inasemekana alikuwa mfadhili wa TANU..na tajiri wa kariakoo.
Wakusoma,
Unahitaji nondo za Mzee John Rupia...
Nondo hizi kama unavyoziita zimo katika kitabu cha Abdul Sykes:

Ally Sykes ndiye aliyechora kadi ya TANU na kuchagua rangi na nembo yake. Rangi alizochagua zilikuwa, nyeusi kuwakilisha taifa la Kiafrika na kijani ardhi ya Tanganyika. Mfano wa kadi ya TANU ulitokana na kadi yake ya Tanganyika Legion. Baada ya kumaliza kuichora ile kadi, aliwaendea Tanganyika Standard Newspapers ili wamchapishie. Kutoka mfukoni mwake mwenyewe alichapisha kadi 1000 za kwanza na akitumia fedha za TAGSA alichapisha kadi nyingine 2000. Kadi nambari 1 ilitolewa na Ally Sykes kwa rais wa TANU, Julius Kambarage Nyerere na Ally aliweka sahihi yake kama afisa aliyeitoa. Ilipendekezwa kwamba kadi chache za mwanzo lazima zipigwe mnada na fedha zitakazokusanywa zitiwe kwenye hazina ya chama. Abdulwahid, Ally, Dossa Aziz, Rupia na wengine walipanda dau kununua kadi hizo. Ally alimshinda kaka yake Abdulwahid kwa bei akapata kadi ya TANU nambari 2; Abdulwahid alipewa kadi nambari 3; Dossa Aziz kadi nambari 4; Phombeah kadi nambari 5; Dome Okochi, mmoja wa wale wazalendo kutoka Kenya katika TANU alipata kadi nambari 6 na Rupia kadi nambari 7. Bibi Titi kadi nambari 16; Iddi Tosiri kadi nambari 25.
 
Wakusoma,
Unahitaji nondo za Mzee John Rupia...
Nondo hizi kama unavyoziita zimo katika kitabu cha Abdul Sykes:

Ally Sykes ndiye aliyechora kadi ya TANU na kuchagua rangi na nembo yake. Rangi alizochagua zilikuwa, nyeusi kuwakilisha taifa la Kiafrika na kijani ardhi ya Tanganyika. Mfano wa kadi ya TANU ulitokana na kadi yake ya Tanganyika Legion. Baada ya kumaliza kuichora ile kadi, aliwaendea Tanganyika Standard Newspapers ili wamchapishie. Kutoka mfukoni mwake mwenyewe alichapisha kadi 1000 za kwanza na akitumia fedha za TAGSA alichapisha kadi nyingine 2000. Kadi nambari 1 ilitolewa na Ally Sykes kwa rais wa TANU, Julius Kambarage Nyerere na Ally aliweka sahihi yake kama afisa aliyeitoa. Ilipendekezwa kwamba kadi chache za mwanzo lazima zipigwe mnada na fedha zitakazokusanywa zitiwe kwenye hazina ya chama. Abdulwahid, Ally, Dossa Aziz, Rupia na wengine walipanda dau kununua kadi hizo. Ally alimshinda kaka yake Abdulwahid kwa bei akapata kadi ya TANU nambari 2; Abdulwahid alipewa kadi nambari 3; Dossa Aziz kadi nambari 4; Phombeah kadi nambari 5; Dome Okochi, mmoja wa wale wazalendo kutoka Kenya katika TANU alipata kadi nambari 6 na Rupia kadi nambari 7. Bibi Titi kadi nambari 16; Iddi Tosiri kadi nambari 25.
Abdulwahid, Nyerere, Dossa Aziz na Rupia walikuja uwanja wa ndege kuupokea ujumbe wa TAA toka kwenye mkutano mkuu wa vyama vya siasa vya Afrika ambao kamwe hawakuhudhuria. Makao makuu ya TAA yalikuwa yakifuatilia matukio nchini Rhodesia ya kusini na kaskazini kwa fazaa. Gazeti la Tanganyika Standard lilikuwa na haya ya kueleza:

Reuter imearifu kwamba Itla Ung, mjumbe wa Burma katika Umoja wa Mataifa, amewasili Lusaka kuhudhuria mkutano mkuu wa vyama vya kisiasa vya Afrika, ambao unatafuta njia za kuimarisha ‘’harakati za kitaifa,’’ katika nchi husika za Afrika.
 
Back
Top Bottom