Nani wa kuvunja mnyororo wa michango ya harusi?

Nani wa kuvunja mnyororo wa michango ya harusi?

Masulupwete

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2012
Posts
2,366
Reaction score
2,424
Ninavyoona hii michango ya harusi ni mnyororo wa kutajirisha watu tu kwa kisingizio cha kuwanufaisha/ kusherehesha wanaharusi.

Kiukweli, mnyororo huu itabidi ifike wakati uvunjwe (kama sio kizazi hiki basi kijacho) kwani kamwe haupo kwa maslahi ya wanaharusi kama inavyodhaniwa na wengi, zaidi unawaacha wanaharusi na ndugu wa karibu na mizigo ya madeni isiyomithilika.

Najua povu litakuwa jingi hapa na pengine kwa tulipofika ni ngumu kuuvunja mnyororo huu hasa kwa sababu wafaidika ni wengi na kumejengeka mazoea kuwa ndo kitu "kilichozoeleka".

Kiukweli wanaofaidika ni hawa:

(i) Ma-MC
(ii) Wapambaji maharusi na kumbi
(iii) Wenye kumbi za harusi
(iv) Wapiga picha za mnato na za kutembea
(v) Wasafirishaji wa maharusi na wageni waalikwa
(vi) Waleta misosi
(vii) Waleta vinywaji
(viii) Madensa, waimbaji na wachekeshaji
(ix) Waleta vifaa kama viti, majamvi n.k
(x) Wanakamati
(xi) Waleta vipazasauti & muziki
(xii) n.k.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu mimi sina ham na michango....maana nlmchangiaga mtu hlf akahama mtaa....hata kadi hakunikumbuka..!!yan ukinambia mambo ya mchango naweza kukutukana
Ninavyoona hii michango ya harusi ni mnyororo wa kutajirisha watu tu kwa kisingizio cha kuwanufaisha/ kusherehesha wanaharusi.

Kiukweli, mnyororo huu itabidi ifike wakati uvunjwe (kama sio kizazi hiki basi kijacho) kwani kamwe haupo kwa maslahi ya wanaharusi kama inavyodhaniwa na wengi, zaidi unawaacha wanaharusi na ndugu wa karibu na mizigo ya madeni isiyomithilika.

Najua povu litakuwa jingi hapa na pengine kwa tulipofika ni ngumu kuuvunja mnyororo huu hasa kwa sababu wafaidika ni wengi na kumejengeka mazoea kuwa ndo kitu "kilichozoeleka".

Kiukweli wanaofaidika ni hawa:

(i) Ma-MC
(ii) Wapambaji maharusi na kumbi
(iii) Wenye kumbi za harusi
(iv) Wapiga picha za mnato na za kutembea
(v) Wasafirishaji wa maharusi na wageni waalikwa
(vi) Waleta misosi
(vii) Waleta vinywaji
(viii) Madensa, waimbaji na wachekeshaji
(ix) Waleta vifaa kama viti, majamvi n.k
(x) Wanakamati
(xi) Waleta vipazasauti & muziki
(xii) n.k.


Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi kazini nimetengwa na baadhi ya wapumbavu kwasababu ya hii michango.
Nilishaapa sitachangia sherehe.
Fanya sherehe kwa gharama zako na size yako.
Una shida nitakusaidia hata kama sikujui, but sio upuuzi wa kuchangia sherehe.
Ndoa nimefunga kwa mkuu wa wilaya
 
Hii tabia itaondoka/kufa kwa watu kususia kuchangia hatusi.
Mleta mada, kuchangia harusi sio sheria bali ni mfumo uliojijenga kutokana na hulka.
Hulka ni tabia, na ili tabia ikome ni watu wenye tabia hiyo mmoja mmoja kuamua kwa dhati kuiacha.
Mleta mada..acha kuchangia harusi!
Mwisho wa siku tabia hii itakoma.
 
Hii tabia itaondoka/kufa kwa watu kususia kuchangia hatusi.
Mleta mada, kuchangia harusi sio sheria bali ni mfumo uliojijenga kutokana na hulka.
Hulka ni tabia, na ili tabia ikome ni watu wenye tabia hiyo mmoja mmoja kuamua kwa dhati kuiacha.
Mleta mada..acha kuchangia harusi!
Mwisho wa siku tabia hii itakoma.
Umenena.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom