Nani wa kuvunja mnyororo wa michango ya harusi?

Nani wa kuvunja mnyororo wa michango ya harusi?

Tsh laki moja inanunua mifuko sita ya cement pamoja na usafiri.. Ukiweza kuchangia harusi kumi basi hiyo ni mifuko 60 inayoweza kufyatua tofali 2,000 za block.
 
Ninavyoona hii michango ya harusi ni mnyororo wa kutajirisha watu tu kwa kisingizio cha kuwanufaisha/ kusherehesha wanaharusi.

Kiukweli, mnyororo huu itabidi ifike wakati uvunjwe (kama sio kizazi hiki basi kijacho) kwani kamwe haupo kwa maslahi ya wanaharusi kama inavyodhaniwa na wengi, zaidi unawaacha wanaharusi na ndugu wa karibu na mizigo ya madeni isiyomithilika.

Najua povu litakuwa jingi hapa na pengine kwa tulipofika ni ngumu kuuvunja mnyororo huu hasa kwa sababu wafaidika ni wengi na kumejengeka mazoea kuwa ndo kitu "kilichozoeleka".

Kiukweli wanaofaidika ni hawa:

(i) Ma-MC
(ii) Wapambaji maharusi na kumbi
(iii) Wenye kumbi za harusi
(iv) Wapiga picha za mnato na za kutembea
(v) Wasafirishaji wa maharusi na wageni waalikwa
(vi) Waleta misosi
(vii) Waleta vinywaji
(viii) Madensa, waimbaji na wachekeshaji
(ix) Waleta vifaa kama viti, majamvi n.k
(x) Wanakamati
(xi) Waleta vipazasauti & muziki
(xii) n.k.


Sent using Jamii Forums mobile app
Hili ni suala la principle na utamaduni.Unaanza wewe tu kukataa kuchangia watu na ikifika zamu yako hawakuchangii basi inakuwa umekata mnyororo
 
Kwa sie wengine fungulia mbwa tunazama mwishoni kula na kucheza singeli.. Tujuane..

Yaani ntafanya makosa yote ikiwemo hilo la kuchangia. Lakini la kuondoka bila kula hilo siwezi kosea
 
MaMC kujeni hapa. Maghorofa mengi mliyojijengea yanatokana na michango ya harusi. Gharama zenu hazipungui shilingi milioni moja na hazikatwi kodi kabisa! Kwa mwezi mmoja mnaingiza si chini ya milioni nne. Vivyo hivyo kwa Wapishi, Video Shooters na wote ambao hutoa huduma katika sherehe hizi. Niliwahi kumsikia MC Pilipili akitamba kuwa yeye bila ya milioni mbili hawezi kusherehesha katika harusi.
 
Back
Top Bottom