Nani yupo sahihi,Afande Sele au Mrisho Mpoto?

Nani yupo sahihi,Afande Sele au Mrisho Mpoto?

Pamoja na kuwa Mpoto yuko sahihi, ila nae apunguze unafiki na kujipendekeza sana, pia Afande sele angetutajia walau majina ya wasanii waliondolewa kwenye orodha ya wimbo husika tupate kuwapima kama kweli ni wazalendo au lah
 
Ila hapa mrisho mpoto kajibu kwa akili sana!!!
Mifano hai justify uzalendo wa Bella, angesema Bela amefanya nini zaidi ya wengine. Mrisho Mpoto anachangany kati ya UZALENDO na UMOJA. Ingekuwa ni kampeni ya UMOJA (UNITY) tungewashirikisha watu wa pande zote meaning mataifa mbalimbali......uzalendo una uhusiano wa moja kwa moja na homeland.......Atuambie basi kwanini anathani Bela ni mzalendo kuliko wazawa....
 
Maneno Makali ya AFANDE SELE kutoka Instagram Kwa MRISHO MPOTO na Majibu ya MPOTO kwa AFANDE SELE...

Afande Sele King - Rafiki yangu mkubwa mjomba mpoto kama ni kweli wewe ndio ulikua kinara ktk kusimamia utayarishaji wa wimbo maalumu wa kuhamasisha uzalendo kwa taifa halafu ukashawishi kuondolewa kwa baadhi ya wasanii wazawa ndani ya wimbo huo na badala yake ukampa nafasi rafiki yetu christian bella kushiriki ktk wimbo huo unaowahusu watanzania wkt ukijua wazi kuwa bella pamoja na ukweli ni rafiki yetu sana lkn bado yeye sio mtz bali ni mcongoman....ktk hili mjomba umetukosea sana watanzania wenzako na kwa hakika kama ingekua kitendo chako hicho umekifanya kwa nchi zilizoshiba uzalendo na zisizovaa joho la unafki mjomba ulistahili kukatwa nywele zako na kupigwa risasi angalau tano kichwani kwa uchache tena hadharani kwani ulichofanya ni usaliti kwa nchi yako na ni aina flani ya uhaini...

Majibu

Mrisho Mpoto Akijibu - Kaka yangu @afandeseleking Bado narudia kusema kwamba heshima nnayokupa inatoka Mbali sana kwenye chumba cha nne cha moyo Wangu... Sihitaji kupoteza wino Mwingi kukukumbusha tofauti iliyopo kati ya UZALENDO, UZAWA na URAIA kwasababu nina uhakika unazifahamu vyema isipokuwa huenda leo haujaamkia ule ubavu sahihi na ule wa ukarimu wako ulionao siku zote, mpaka ukakataa uwepo wangu hapa Duniani Kwa kunichagulia adhabu ya kupigwa risasi tano tena za kichwa... kwakua hukuniuliza hili jambo kabla Itoshe kusema hunitaki tena...hivyo basi kabla sijapigwa hizo risasi tano nitakachofanya ni kukupa maelezo machache yatakayokufanya uipate picha ya UZALENDO.. Hivi unajua kama John Okello alipigania uhuru wa Zanzibar!? Majeshi yetu yamepigania uhuru wa msumbiji na hata Chegu sio mcuba na alipigania uhuru wa Cuba na Congo pia.. Na je unajua kama kuna wazawa wanaoangamiza maslahi ya nchi na kuna wazalendo wasiobagua!? Kaka, Afrika ni moja na waafrika wote ni ndugu zetu ( umajumui Afrika, tena ukichimba huko sana kwa hapa nchini utakuna na Prof Shivji) .. na ndio maana hata mwenge wa uhuru uliwekwa juu ya mlima kilimanjaro ili kumulikia nchi nyingine.. Kumbuka hiyo mitizamo ya KIUZAWA Mwalimu aliita mitizamo membamba.. kwa maana ya kwamba ipo kwa ajili ya Kuiangamiza afrika

Na mwisho ningependa kukuuliza--->Je umezisikia shangwe za wazalendo na wazawa leo hapa dodoma baada ya kusikia Babu Seya na familia yake wamepewa msamaha wa rais!!? Wewe ni RASTA kaka.. kumbuka siku zote CHUKI HUMUUMIZA ANAYEIHIFADHI.. [HASHTAG]#AfrikaUnite[/HASHTAG] ✊


Nani yupo sahihi kati ya hawa mafahari wawili?
Je kuwa Mzalendo ni lazima uwe mzawa wa nchi husika?[/Q
Hii imenikumbusha alivowakilisha kenya uko nchi za watu kwenye tamasha la kiswahili japo alijitetea sana
afande yupo sahihi vp mwanamuziki wa bongo
 
MPOTO YUKO SAHIHI ILA KWA TAHADHARI



KWA MFANO
IKITOKEA MGONGANO WA MASLAHI KATI YA DRC NA TZ, CHRISTIAN BELA ATAKUWA TAYARI KUTUMWA NA DRC DHIDI YA TZ ILA HAWEZ KUTUMWA NA TZ DHDI YA DRC.

NADHANI NIMEELEWEKA
Jibu sahihi umelitoa ila hujiamini. Mpoto HAYUKO SAHIHI kuhusu uzalendo na sababu ni hiyo ambayo wewe umeieleza vyema. Mpoto aweke akilini kuwa kuna tofauti kubwa sana kati ya UZALENDO na USHIRIKIANO.
 
Ni aibu kujivunia mipaka iliyowekwa na wazungu , Mpoto kamaliza kila kitu
 
Nyimbo ya uzalendo inahusu nchi yangu bado niimbiwe na wasanii wa nchi jirani shubaaaamiti ubata uo
 
Maneno meeeeengi na ngonjera hakuondoi definition ya Uzalendo.

patriotism
ˈpeɪtrɪətɪz(ə)m/
noun
noun: patriotism
the quality of being patriotic; vigorous support for one's country

Huwezi kuwa mzalendo kwa nchi isiyo yako. Askari wetu kwepo Congo, hakumaanishi wao ni Wazalendo wa DRC, NO. Christian Bella anaweza kuipenda Tanzania, lakini hawezi kuwa mzalendo kwa nchi yetu. Hawezi kuipigania Tanzania dhidi ya nchi yake, na hapo ndio maana ya uzalendo inapatikana.
saaaafiiii
 
Uzalendo sio rangi au asili ya nchi unakotoka!Bali ni fikra na utayari kuipigania nchi kwa ajili ya maendeleo na ukombozi wa wanyonge!Alichoeleza mpoto kina maana na ndio fikra hasa za uzalendo!Kuna mijitu imezaliwa hapa na mijizi haina huruma na wanyonge,kisa mweusi utamwita mzalendo?lakini kuna mtu mfano prof shivji ni muasia kwa asilia lakini ana imani na yuko tayari kuipigania TZ mpaka kifo tutamwitaje??
Afande sele akue....
Sipendi ili neno Wanyonge
 
Kama kweli mpoto kawatoa wabongo wenzake na kumuweka huyo mzaire amekosea sn,la sivyo asingewatoa watz na huyo mcongo angemwacha aimbe,Messi ni mchezaji mzuri sn na ameisaidia sana barcelona kutwaa mataji lkn kamwe hawez kuitwa timu ya taifa ya Hispania
 
Nenda Kaishi hapo Kenya wewe Mtanzania uone utakavyobaguliwa ndio utajua Afande Sele yuko sahihi.....Mrisho Mpoto ni mjinga kumuingiza huyo mcongo
 
Afande Sele yupo sahihi kwasababu hoja kubwa hapo ni kuwatoa baadhi ya wasanii wa Tanzania na kumuweka msanii wa Congo Bella, unawatoaje wasanii wenzio kwasababu ya msanii mwingine ambaye hata si raia na kuita ni uzalendo hii si sawa.
 
Kwanza kumsirikisha mtu ambaye si Mtanzania kisa tu ana sauti nzuri ni kukosa uzalendo, maana yake umejikataa jinsi ulivyo sasa utaipenda nchi yako kweli wakati watu wake huwapendi
 
Afande Sele yupo sahihi kwasababu hoja kubwa hapo ni kuwatoa baadhi ya wasanii wa Tanzania na kumuweka msanii wa Congo Bella, unawatoaje wasanii wenzio kwasababu ya msanii mwingine ambaye hata si raia na kuita ni uzalendo hii si sawa.
Wasaniii gani wametolewa? hakuna msanii aliyetolewa .....wasanii fulani kutoimba sio kwamba walitolewa..... hapo kuna nyimbo zaidi ya mbele....Afande ameokoteza maneno ya mitaani na vijiweni... Hapo kinacho muuma Afande ni Bela kuimba na si hivyo tuuu Afande ana wivu kweli muziki umemshinda kabaki kuwapiga madongo walio fanikiwa na wanaopiga hela kwa sasa.

Majuzi alikuwa anaongelea maswala ya maadili akawa anaponda nyimbo za kina Msaga sumu,GIgy na Zaidi kisa watanzania wana zisikiliza sana...
Lakini najiuliza wakati yeye ana vua nguo kule club na kubaki na chupi alikuwa ana hubiri maadili gani?
Afande maneno yake ya mejaa chuki na wivu dhidi ya walio fanikiwa...
Mpoto anapiga hela kweli kweli kwa hiyo Lazima Afande kwa hali aliyo nayo atafute njia ya kumfanya mpoto aonekane mtu mbaya.........
 
Wasaniii gani wametolewa? hakuna msanii aliyetolewa .....wasanii fulani kutoimba sio kwamba walitolewa..... hapo kuna nyimbo zaidi ya mbele....Afande ameokoteza maneno ya mitaani na vijiweni... Hapo kinacho muuma Afande ni Bela kuimba na si hivyo tuuu Afande ana wivu kweli muziki umemshinda kabaki kuwapiga madongo walio fanikiwa na wanaopiga hela kwa sasa.

Majuzi alikuwa anaongelea maswala ya maadili akawa anaponda nyimbo za kina Msaga sumu,GIgy na Zaidi kisa watanzania wana zisikiliza sana...
Lakini najiuliza wakati yeye ana vua nguo kule club na kubaki na chupi alikuwa ana hubiri maadili gani?
Afande maneno yake ya mejaa chuki na wivu dhidi ya walio fanikiwa...
Mpoto anapiga hela kweli kweli kwa hiyo Lazima Afande kwa hali aliyo nayo atafute njia ya kumfanya mpoto aonekane mtu mbaya.........
Sawa alikosea kuvua nguo stejini,je hilo linahalalisha wasanii wengine kuimba matusi?huoni kuwa Afande Sele amekuwa balozi mzuri wa kukemea vitu visivyofaa pengine baada ya kuhisi kuwa aliteleza huko nyuma?Tukubali tukatae,Afande Sele anabaki kuwa mmoja wa watunzi bora wa muziki tanzania.Hoja kuwa muziki umemshinda sitaki kusadiki kwasababu ni sisi wenyewe wanajamii ndio tuliokataa nyimbo zenye ujumbe ili tuimbiwe matusi na akina giggy na msaga sumu.Hivi tungo za nyimbo kama
1.Mayowe
2.Mkuki moyoni
3.Darubini kali
4.Usinichukie
5.Malaria
6.Mbele yako nyuma yangu
7.pesa
8.Nitarudi na roho yangu?
Unaanzaje kuziweka nyimbo tajwa hapo juu katika kapu moja na mwanaume mashine au nampa papa?Ifikie mahali tuwe wakweli,inawezekana ni kweli kuwa humpendi Afande Sele kwa kadiri moyo wako unavyokuagiza ila kusema kuwa muziki umemshinda hapo sio kweli.Kama "mwanaume mashine" unakuwa namba moja katika chati za muziki wetu,huo unaoshika namba 10 utakuwaje sasa?UPENDO KWA WOTE CHUKI SI KWA YEYOTE
 
Apa najaribu kuwaza ila nakumbuka kitu alafu muniambie huu ulikuwa uzalendo au kitu gani?,kombe la dunia 2002 wachezaji wengi wa Senegal kila walipokuwa wanaimba wimbo wao wa taifa walikuwa na hisia sana na wengine walikuwa wanaimba uku machozi yanawatoka alafu wakiwa uwanjan iyo shughuli yake wafaransa walipata shida hasa.
 
Back
Top Bottom