Wakuu wangu Gang Chomba na Nkwingwa Masuke.....Nataka tu niwaambie kwamba....
Kitu pekee ambacho watu walikuwa hawakijui kwa Marijani ni kwamba alikuwa hapendi kunyonywa/kukandamizwa na alikuwa ana kipaji hali iliyomfanya ajiamini kwamba anaweza na ndio maana baada ya kuona ubabaishaji mwingi na watu wengi wanatajirika kupitia mgongo wake/kwa jasho lake alion ni bora aachane na muziki na kuamua kuuza kanda za muziki wake na maisha yakawa yanasonga mbele.....Hili watu kama akina Mbaraka Mwinyishehe hawakuliona ndio maana walinyonywa sana na kwa taarifa yako ukinda kwa mke wa Mbaraka Mwinyishehe (mama Taji) atakueleza ni jinsi gani wakenya walitajirika na kipaji cha mume wake na kuiacha familia yake masikini....Kitu hicho mtoto wa Kariakoo Doza alikiona na hakutaka kitokee maishani mwake ndio maana akaachana na muziki na kufungua kijiduka cha kuuza kanda zilizotokana na kipaji chake.......
Ni kweli kwamba Marijani alikosa bendi kwa takribani miaka mitatu au minne.....Hapa ieleweke kwamba alichokosa ni bendi ya kudumu na si kwamba aliacha kabisa kupiga muziki, katika kipindi alichokosa bendi ya kudumu alikuwa akipiga deiwakakatika bendi za Mwenge Jazz ya Dsm na Kurugenzi Jazz ya Arusha mpaka alipoungana na wenzake kuunda kundi la Tanzania Stars na baadae kuanzisha kundi lake la Afri Culture ambalo lilikuwa likitumia mtindo wa 'Mahepe Ngoma ya wajanja' . Nataka nimwambie Gang Chomba kwamba Marijani amewahi kuanzisha bendi moja tu ya Afri Culture ambayo hakudumu nayo,ilikufa kutokana na uchakavu na ukosefu wa vyombo, bendi nyingine zote alizopitia za STC, Safari Trippers na Dar International alizikuta zimeanzishwa na wengine mfano Dar International ilianzishwa mwaka 1977 na mwanamuziki mwingine Nguli nchini Abel Barthazar akiwa na Joseph Mulenga,Abdallah Gama,Cosmas Thobias Chidumule,Ali Rajab,Belesa Kakere,Marijan Rajab,Machaku Salum,King Michael Enock,Joseph(Yusuph) Bernard na Habib Jeff na Marijani alijiunga baadae mwaka huohuo na kujiengua mwaka 1978 na mara baada ya kujiengua bendi hiyo ilisambaratika......Sababu kubwa ya bendi hii kusambaratika ni baada ya kupata umaarufu wa ghafla baada ya Marijani kujiunga nayo na umaarufu huo ghafla ni kwa sababu Marijan Rajab aliifanya bendi ipige muziki wenye mahadhi kama ya ule muziki uliokuwa ukipigwa na bendi yao kipenzi ya Safari Trippers hivyo kuzidi kumletea umaarufu Marijan Rajab kitu ambacho inadaiwa hakikupendezwa sana na wanamuziki wengine akiwemo Abel Barthazar ambao waliona kwamba watu wanaichukulia Dar International kama Safari Trippers....Walianza kumpiga vita Marijan Rajab ambaye hakupendezwa na hali hiyo hivyo kuamua kujitoa katika bendi hiyo mwaka 1978 (miezi 9 tu baada ya bendi kuanzishwa).
Baada ya bendi kusambaratika,mmiliki wa Dar International Zachariah Ndebame alimuomba Marijan Rajab arudi kwa ajili ya kuisuka upya bendi hiyo ambapo alikubali na kurudi rasmi kwenye bendi,hapo akakutana na mpiga solo Hamza Kasongo ambaye kwa kushirikiana waliiongoza bendi hiyo kutoa vibao vitamu kama Zuwena,Vick na Mayasa......Vibao hivi viliurudisha umaarufu wa bendi hii kiasi cha kuzitisha bendi ilizozikuta zikitamba wakati huo kama Vijana Jazz,Juwata Jazz,Mlimani Park,Marquiz na Biashara Jazz.....Hali hii ilileta ushindani mkubwa miongoni mwa bendi hizo.....Baadae bendi hii ilipata wanamuziki chipukizi kama Fresh Jumbe ,Tino Masinge 'Arawa', Mohammed Mwinyikondo na wengine na kurekodi vibao vitamu kama Mzee Said,Baba Anna,Masudi amekuwa jambazi,Bwana Mashaka,Pondamali kufa kwaja, Mwajuma, Pendo si kulazimishana, Usimtese Mwana, Chakubanga na nyingine nyingi zilizotamba na kufunika ile mbaya enzi hizo.....Alikaa na Dar International iliyozaliwa upya mpaka mwaka 1986 bendi hiyo ilipokufa kutokana na uchakavu wa vyombo na mmiliki wake kushindwa kuiendesha hali iliyopelekea Marijani aamue kutulia tu na kuamua kufanya Deiwaka Mwenge Jazz na Kurugenzi Jazz mpaka mwaka 1992 alipoanzisha bendi yake ya Afri Culture ambayo hata hivyo haikukaa sana, ilikufa kutokana na uchakavu wa vyombo....
Kitu pekee kilichokuwa kikimsumbua Marijani Rajabu ni uwezo mdogo/umasikini, hakuwa na uwezo wa kununua vyombo na hakufaidika kwa namna yoyote na muziki wake zaidi ya kuwafaidisha wamiliki wa bendi alizokuwa akizitumikia na ndio maana mwaka 1992 aliamua kuachana na muziki na kufungua kijiduka kidogo cha kuuza nyimbo zake pale Kariakoo ili angalau afaidi matunda ya kazi zake ....Pamoja na watu kumfuata ajiunge na bendi zao Marijani aligoma na maradhi ya moyo(ulikuwa mkubwa) yaliyokuwa yakimsumbua yalizidi mpaka mauti yalipomfika tarehe 23/03/1995 kutokana na matatizo hayo ya moyo kuwa mkubwa.....
Pamoja na uwezo/kipaji kikubwa alichokuwa nacho katika kutunga na kuimba Marijani alikuwa na maisha magumu sana mpaka umauti unamfikia.....Alikufa maskini mno licha ya mashairi ya nyimbo zake kutamba na nyingine (Mwanameka) kutumiwa na NECTA hata kwenye mtihani wa kidato cha Nne miaka hiyo....
Siku zote mtu mwenye kipaji hujiamini na hapendi kuburuzwa kutokana na kipaji chake hali ambayo humfanya mtu ahisi kwamba ni mchoyo/mbinafsi.....Mfano mzuri ni Haruna Moshi Shaaban a.k.a Boban wa Coastal Union ya Tanga....