Ni kweli kabisa kuwa huwezi kumuelewa lakini ni vema ukaelewa yafuatayo;Jana alipopewa ' Fursa ' ya kuzungumza wakati wa ' Show ' ya Saida Karoli Waziri wa Habari, Michezo, Utamaduni na Sanaa Dkt. Harrison Mwakyembe alisema namnukuu " Nipende tu kutoa shukran kwa Waandaji na hasa kwa Msanii Saida Karoli kwa kuweza kuamka tena ila nipende tu kuwataarifu kuwa nimekuja hapa Kuburudika nanyi lakini Mke wangu Mpenzi hivi ninavyozungumza nanyi yupo ICU hivyo naomba wakati tunafurahi pamoja hapa basi pia tumuombee " mwisho wa Kumnukuu Waziri Dkt. Mwakyembe.
Mimi binafsi kama GENTAMYCINE sijamuelewa na hata ' moyo ' wangu hadi sasa ' unakataa ' kabisa kumuelewa kwa kile kitendo cha kumuacha ' Mkewe ' ICU halafu na ' kukimbilia ' Escape One ' kutiririka ' na ' kuserereka ' na Mwanamama Saida Karoli.
Naamini kabisa kuwa humu JF kuna ' Watu ' wengi ' Vichwa / Vipanga ' kabisa hivyo hamtashindwa kunisaidia ' kunielewesha ' juu ya hili jambo ili pengine baada ya ' Ufafanuzi ' wenu basi ' moyo ' wangu uweze ' Kufunguka ' rasmi na nimwelewe Waziri Mwakyembe.
Nawasilisha.
1 Mh. Waziri alikuwa pale kikazi.
2. Anauguliwa na mkewe
3. ICU hairuhusiwi mtu kulala na mgonjwa.
4. Ni mtu wa watu na hivyo matatizo yake pia ni ya wote.