Naomba kufahamishwa kuhusu toyota brevis 2500cc

Naomba kufahamishwa kuhusu toyota brevis 2500cc

Lita 1/km 8 mbona ni ulaji wa kawaida kabisa huo.
Kama vp mdanganye mwenzio akanunue ka vitz ambako hata power havinaga
km ni power ya engine mshaurini akachukue Harrier (matako ya nyani) inakula mafuta hivyo hivyo 8-11km / litre na linafaa popote si Brevis kila mwezi gereji
 
km ni power ya engine mshaurini akachukue Harrier (matako ya nyani) inakula mafuta hivyo hivyo 8-11km / litre na linafaa popote si Brevis kila mwezi gereji
Jamani wee ukwaju mbona mama yangu ana BREVIS huu mwaka wa pili sasa hajui gereji ipoje ??? Zaidi ya kubadili oili tu. Nakumbuka siku moja tu ndo lilizingua kuwaka tukamuita fundi akaja home akalichokonoloa saa hiyohiyo likawaka,, ukwaju unatudanganya[emoji22]
 
haya km nakudanganya ila mitaani hilo ghost tunalijua
km Mama analo ni vizuri la kuendea Kanisani na sokoni
lkn Dar - Kongwa ni hadithi
Sasa ww unataka nichulie IST inayokula lita 1 kwa km 18 sawa. Lakini siku nikitaka kwenda kijijini kwetu mwanza halifiki kwanza nitaua injini af pili barabara ya kule haipiti
 
Achana na hilo jini mkata kamba,brevis ananyonya sana damu meaning wese,pia hyo engene ni kubwa kuliko body,so hua zikizingua ni ishu,pia,siku ukilichoka hakuna wa kumuuzia dada angu..na yameshuka bei kwasabab hyo ,used had mil7 tena namba D
 
Ukiagiza kupitia Beforward kwenye BF Supported I.D weka 500291 utapata punguzo kwenye gharama za kununua gari
 
Gari inategemea na unapenda nini.

Unaponunua gari kama brevis, mark X, GX 110 , Lexus GS, LS na gari zinazofanana na hizo ambazo injini zake CC inaanzaia 2500 plus

Kuna faida kadhaa utapata

1. Luxury - gari hizo zote zina comfort, Safety ya juu kama ukipata ajali.

2. Injini ina power kubwa, sio tu ya ku overtake na kukimbia, lakini gari inakuwa stable barabarani, gari inatulia na nzito. Inakuwa inamudu barabara complex kidogo, milima nk nk

Tatizo ni moja tu na si tatizo la gari husika ni Tatizo la Masikini sisi. (limited financial)

-Gari inakuwa na unywaji wa mafuta wa juu kidogo kulinganisha na gari ndogo kama Vitz, IST, Porte nk

Sasa hivi Vigari vinavyokunywa Mafuta vizuri. Raha yake na faida ni hapo tu kwenye Mafuta. Hususani ukiwa huna uchumi mzuri lakini Pia pengine ni Cheap kufanya Mantainance /Service.

Lakini hizi gari ndogo Vitz, Porte, IST na ndugu zao wote. Unakosa vitu kadhaa

1. Havina comfort. Sio luxury ni sawa na kulalia Godoro la bei nafuu kabisa linaloumiza mgongo wakati mwenzio analalia Tanform Arusha tena ya Spring

2. Hazina power ya kutosha, kuhimili complex roads, unaweza ingia hata kwenye tope dogo tu usitoke. Lakini hazitulii barabarani kulinganisha na hizo za injini kubwa.

3. Safety yake ni ndogo, ukipata ajali unakunjwa kama karatasi lakini mifumo mingine pia ya kiulinzi inakuwa sio advanced

Mwisho wa siku ni uchaguzi wa mnunuzi nini unataka. Kutokana na gari husika.

Huwezi kulinganisha Raha ya Crown dhidi ya Raum

Kazi ni kwako binafsi bora nipambane na mafuta ila niwe Comfortable
 
Kalanga 1 kwanza hongera sana kwa kufikia hatua ya kununua gari.
Moja kwa moja naomba kwanza nijibu swali la msingi kisha mengine yatafuata.
Ulaji wa mafuta wa Brevis ya 2500cc ni wastani wa 8.77L/100 km. Sasa huo wastani ni wa gari mpya,gari inapozidi kutumika ndo nguvu ya engine inavyopungua na ulaji wa mafuta nao unaongezeka.
Tank la mafuta linachukua lita 70. Sasa hapo ni wewe tu kupiga hesabu uone full tank ni kiasi gani kulingana na eneo ulipo.
Sasa haya ni mengineyo: Kwanza kabisa huwezi kupata Brevis mpya,zilitengenezwa kuanzia 2001-2007. Kwa hiyo utakayonunua lazima iwe ina uchakavu wa miaka 11 hivi na kuendelea.
Engine ya Brevis in inline 6 na nafikiri Brevis ndo gari ya mwisho ya Toyota kutumia inline 6. Ukweli kwa upande wangu napenda sana engine za inline six kwa kuwa zipo so smoooth. Kwa kuwa ni inline six basi ni lazima iwe rear wheel drive kwa kuwa huwezi weka front wheel drive kwa gari yenye inline six configuration. Kwa kawaida gari za rear wheel drive huwa zinalenga soko tofauti na za front wheel drive. Ninamaanisha kuwa mara nyingi rear wheel drive huwa zina bei kubwa kuliko front wheel na walengwa ni tofauti.
Kama ningekuwa nipo kwenye nafasi kama yako,ningejaribu kuangalia gari ambayo ina standard sawa na Brevis but on modern platform,ingawa kama moyo wako umechagua Brevis basi we chukua tuu.
Nakushauri uangalie Toyota Mark X. Hii imeanza kutengenezwa 2004 na mpaka leo kuna toleo jipya.
Nafikiri nimekupa mwanga.
Wadau wa kuongezea waongeze na wenye kukosoa wafanye hivyo.
 
Ninatumia hio gari mwaka wa 2 sasa......haipitishi mwezi sijakatiza bagamoyo road kulenga arusha....nimenunua ikiwa na km 35000 mpaka sasa iko na km 129000 haijawahi nisumbua zaidi ya mumwaga oil....na njian sijawahi kuwa overtaken na gari ingine.....mafuta binafsi naona ni kawaida tuu
Hujakutana na volkswagen toureg (sina hakika na spelling ) speed 260 unashindwaje kupitwa kama kila mtu akimaliza kisahani!
 
km ni power ya engine mshaurini akachukue Harrier (matako ya nyani) inakula mafuta hivyo hivyo 8-11km / litre na linafaa popote si Brevis kila mwezi gereji
Harier matako ya ngedere ni milion 25 , brevis milion 12-13
 
Ukiona mtu hata km 8/ lita anahoji na kushauri gari za cc 1500 ujue hajafikia uwezo wa kumiliki gari anapaswa ajikite kwenye boxer kwanza... ndio uwezo wake kwa sasa kuhusu kumiliki gari asubiri kwanza
 
Hii mkuu siyo ya kununua kabisa inakula mafuta sana ikitaidi km 8 lth 1! Hapo haijaanza kuchoka halafu kama mtu wa kuuza mbeleni itakusumbua last ina tatizo la engine kwa dodosa za kijiweni! Nakushauri tafuta gari walau ya "cc 1300-2000! Im stand to be corrected!
Inakula fresh tena zaidi ya mark x
 
Hizi gari watu wanaziogopa bure. Gari yangu ya kwanza ni hii na ulaji wa mafuta ni kawaida hasa high way. Nimefanya uchunguzi wa kutosha, lita 7 unatembea km 100 bila ac, ukiwasha ac inapungua kidogo.
 
Back
Top Bottom