Naomba kufahamu kisheria hii imekaaje?

Naomba kufahamu kisheria hii imekaaje?

hmaloh

Senior Member
Joined
Nov 22, 2018
Posts
162
Reaction score
314
Habarini ndugu zangu wapendwa wanajamvi,

Naomba kufahamu ikiwa inawezekana kama mzazi kuwajibishwa kwa kosa alilofanya mtoto wangu. Hali iko hivi: hapa mtaani kuna mzee fulani anasema anataka kunipeleka kwenye vyombo vya sheria kwa sababu binti yangu alivunja kioo cha gari yake.

Walikuwa watoto wengi wakicheza mchezo wa kurushiana mawe, ila bahati mbaya kioo kilivunjwa na binti yangu.

Mzee huyo aliniita kwa ajili ya uharibifu uliofanyika, nami nilifika na kumwambia nitamlipa pesa hiyo ya kioo, ila sasa hivi sipo vizuri kifedha. Cha ajabu ni kwamba, mzee huyo anaendelea kunitishia na kuniambia atanionesha kwa sababu sijamlipa pesa hiyo.

Je, sheria inasemaje kuhusu suala hili? Naweza kuchukuliwa hatua kwa kosa lililofanywa na mwanangu?

NB: Kwa taarifa, binti yangu ana umri wa miaka 6.
 
Hilo sio Swali ni jibu mkuu.

Umeshindwa kumchunga Mtoto wako Mpaka anasababisha Hasara kwèñye Vitu vya Watu Wengine.

Wewe ndiye unayewajibika

Kama mbuzi asiye na ufahamu akifanya uharibifu utakayegharamika ni wewe
 
Lipa mkuu,ndo kulea huko...
Kopa sehemu lipa...watu wamevurugwa sikuhizi.
 
Habarini ndugu zangu wapendwa wanajamvi,

Naomba kufahamu ikiwa inawezekana kama mzazi kuwajibishwa kwa kosa alilofanya mtoto wangu. Hali iko hivi: hapa mtaani kuna mzee fulani anasema anataka kunipeleka kwenye vyombo vya sheria kwa sababu binti yangu alivunja kioo cha gari yake. Walikuwa watoto wengi wakicheza mchezo wa kurushiana mawe, ila bahati mbaya kioo kilivunjwa na binti yangu.

Mzee huyo aliniita kwa ajili ya uharibifu uliofanyika, nami nilifika na kumwambia nitamlipa pesa hiyo ya kioo, ila sasa hivi sipo vizuri kifedha. Cha ajabu ni kwamba, mzee huyo anaendelea kunitishia na kuniambia atanionesha kwa sababu sijamlipa pesa hiyo.

Je, sheria inasemaje kuhusu suala hili? Naweza kuchukuliwa hatua kwa kosa lililofanywa na mwanangu?

NB: Kwa taarifa, binti yangu ana umri wa miaka 6.
Usianze kutafuta mbinu za kisheria za kukimbia suala hili, ni mwanao kafanya kosa yajenge na mwenye gari myamalize. Ukijifanya mjuaji kuna siku atamgonga huyo mtoto na atalipa elfu 50 mahakamani na kesi itakua imeishia hapo.
 
Back
Top Bottom