Naomba kufahamu tofauti ya Kutajirika na Kufanikiwa

Naomba kufahamu tofauti ya Kutajirika na Kufanikiwa

Hyrax

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2023
Posts
964
Reaction score
2,675
Haya maneno mawili yananichanganya kidogo naomba mwenye uelewa aniandikie hapa nijifunze Kufanikiwa si ndio kutajirika huko au kutajirika ndio kufanikiwa kwenyewe mi sielewii.
 
Utajiri umo ndani ya mafanikio
Uttajiri ni Mali nyingi.
Unaweza Kufanikiwa kupata Cheo au Mamlaka katika ngazi fulani.
Utajiri ni jumla ya kila kitu wewe unamiliki kuanzia pesa bank ( Ukwasi )na Assets
Ukwasi unakata.... Tajiri anafilisika.
Unaweza Kufanikiwa Kwa njia tofauti tofauti katika Maisha.
Ila utajiri ni mmoja tu wa pesa na Mali.
 
Haya maneno mawili yananichanganya kidogo naomba mwenye uelewa aniandikie hapa nijifunze Kufanikiwa si ndio kutajirika huko au kutajirika ndio kufanikiwa kwenyewe mi sielewii.
unaweza kufanikiwa lakini usiwe tajiri, utajiri ni zaidi ya kufanikiwa
 
kutajirika ni kupata mali na thamani (vitu)

kufanikiwa ni kutimiza ama kufika malengo yako

utajiri upo ndani ya kufanikiwa. Yani kwa maana nyingine kufanikiwa ni jambo kubwa sana kuliko kutajirika

tukiutoa utajiri ndani ya mafanikio, utajiri unabaki kuwa kama zali tu au upepo wa kisulisuli yani unaweza kukupitia na badae ukaenda zake.

mfano: mtoto aliezaliwa ndani ya familia yenye utajiri (mali & thamani ya vitu) anaweza kukuwa na kuishi kwa upepo huo wa utajiri lakini binafsi akwa hana mafanikio yoyote.

niandike sana kwani kuna bonus!! ndo hivyo lakin nadhani umeelewa kidogo
 
Haya maneno mawili yananichanganya kidogo naomba mwenye uelewa aniandikie hapa nijifunze Kufanikiwa si ndio kutajirika huko au kutajirika ndio kufanikiwa kwenyewe mi sielewii.
Kufanikiwa ni kupata ulichotaka ulivyotaka.

Mfano, kuna profesa wangu mmoja alipanga kuwa Jaji, kufundisha Chuo Kikuu na kuandika kitabu. Alifanikiwa kufikisha lengo lake hilo.

Hapi amefanikiwa bila kujali kama alitajirika au hapana.

Kutajirika nako kupo kwa aina nyingi, lakini wengi wakiongelea kutajirika wanaongelea kiuchumi.

Kuna mtu ndoto yake ni kuwa baharia, akipata kazi ya ubaharia anakuwa kafanikiwa kwenye hilo, bila kujali atatajirika au hatatajirika.

Kuna mwingine anataka kuwa mbunge, lakininhafanikiwi katika hilo, anakuwa mfanyabiashara aliye tajiri sana kiuchumi, lakini hajafanikiwa kutumikia watu kama mbunge.

Kuna mwingine alitaka kuwa padri, lakini hakufanikiwa katika hilo, kaishia kuwa makamu wa rais.
 
Kutajrikika imekaa kiuchumi zaidi (Pesa, mali, vitu vya thamani)
Kufanikiwa ni kupiga hatua kwenye nyanja zote maishani ikiwemo uchumi, kwa maneno mengine kutajirika kuko ndani ya kufanikiwa. Mfano una uzito mkubwa wa mwili wako (Kg 100) na unataka upungue, ukifanya juhudi labda kufanya mazoezi, kula kwa mpangilio maalum na kupunguza uzito wako hadi kufikisha kilo 80, hapo utakuwa umefanikiwa. Kama una ndugu ambao hawana maelewano mazuri, na wewe ukabeba jukumu la kuwapatanisha hadi wakaelewana, hapo umefanikiwa lakini hujatajirika.
 
Kufanikiwa ni kupata ulichotaka ulivyotaka.

Mfano, kuna profesa wangu mmoja alipanga kuwa Jaji, kufundisha Chuo Kikuu na kuandika kitabu. Alifanikiwa kufikisha lengo lake hilo.

Hapi amefanikiwa bila kujali kama alitajirika au hapana.

Kutajirika nako kupo kwa aina nyingi, lakini wengi wakiongelea kutajirika wanaongelea kiuchumi.

Kuna mtu ndoto yake ni kuwa baharia, akipata kazi ya ubaharia anakuwa kafanikiwa kwenye hilo, bila kujali atatajirika au hatatajirika.

Kuna mwingine anataka kuwa mbunge, lakininhafanikiwi katika hilo, anakuwa mfanyabiashara aliye tajiri sana kiuchumi, lakini hajafanikiwa kutumikia watu kama mbunge.

Kuna mwingine alitaka kuwa padri, lakini hakufanikiwa katika hilo, kaishia kuwa makamu wa rais.
Kwa maelezo yako kufanikiwa ni zaidi ya kutajirika?
mtu ni bilionea lakini alitaka ubunge akaukosa kwahiyo hajafanikiwa? Hapo umeenda kwenye mada nyingine
 
Kwa maelezo yako kufanikiwa ni zaidi ya kutajirika?
mtu ni bilionea lakini alitaka ubunge akaukosa kwahiyo hajafanikiwa? Hapo umeenda kwenye mada nyingine
Naam,

Nitakupa mfano.

Kuna tajiri bilionea mkubwa wa Kimarekani anaitwa Ted Turner. Yeye ndiye kaanzisha CNN, alikuja kuiuza baadaye. Katika watu wanaomiliki ardhi kubwa sana Marekani yeye pia yumo, kuna wakati alikuwa ndiye mtu binafsi wa kwanza anayemiliki ardhi sehemu kubwa zaidi Marekani.

Kuna siku alikuwa anafanyiwa mahojiano, akaulizwa, katika maisha yake anaona kuna mapungufu wapi? Wapi hajafanikiwa?

Akajibu kwamba, anaona hajafanikiwa katika maisha ya ndoa, alitamani sana awe na maisha ya ndoa yaliyonyooka bila talaka, lakini ndoa yake na Jane Fonda, muigiza sinema wa Kimarekani, iliishia kwenye talaka.

Kwa hivyo, yumkini mafanikio si kitu kimoja tu, yana nyanja mbalimbali, na katika upande wa biashara, uchumi, Ted Turner amefanikiwa sana, kafanya deals kubwa sana za mabilioni ya US dollar, anamiliki ardhi sehemu kubwa sana Marekani, lakini kwenye sehemu ya mafanikio ya maisha ya ndoa hata yeye mwenyewe anasema hajafanikiwa.

Na kama Ted Turner mwenyewe akiona kuwa maisha ya kudumu katika ndoa nyoofu ni kitu muhimu zaidi ya utajiri, kiujumla katika maisha yake atajiona hajafanikiwa, licha ya utajiri wa kiuchumi mkubwa sana alionao.

Kuna watu matajiri sana kiuchumi, lakini wanaona utajiri wao hauna purpose, na kwa sababu wanataka kuishi maisha ya purpose na kuacha legacy, licha ya utajiri wote huo wa kiuchumi, wanajiona hawajafanikiwa.

Kwa sababu, wanaona, utajiri unaweza kuupata hata kwa bahati nasibu, kitu chenye maana zaidi kwao na kuonekana kuwa ni mafanikio ni kuishi maisha ya purpose na kuacha legacy, mambo ya Abraham Maslow pyramid of needs hayo.

Watu wengi waliokuwa self actualized pesa si mafanikio, kuacha legacy ndiyo mafanikio.

Ndiyo maana unaweza kukuta mtu kama Julius Nyerere, amefariki hana pesa nyingi sana, lakini kuna watu wanaweza kusema kuwa kaumba nchi moja, kajenga nchi, kasaidia kukomboa nchi za Afrika, amefanya mambo makubwa ambayo mengine hata pesa haiwezi kuyafanya (of course ana mapungufu yake, lakini tuangakie achievements hapa).

Ukimlinganisha Nyerere ambaye amefariki bila hela nyingi na mtu kama Mobutu aliyefariki na mabilioni ya US dollar, watu wengi wanaweza kusema Nyerere amefanikiwa kuliko Mobutu kwa heshima aliyojijengea kimataifa, licha ya kushindwa kutimiza ndoto zake, lakini alikuwa na falsafa mpya, aliumba nchi moya, watu wake walimuheshimu na kumoenda sana, aliandika falsafa zake nyingi watu wanasoma na kumnukuu mpaka leo kama mtubwa jutoa muingozo, hivyo, hata bila ya kuwa na pesa nyingi, amefanikiwa kwa kiasi fulani.

Mobutu naye amefanikiwa katika wanaooenda ubadhirifu wa mali ya umma na utajiri uliokithiri.


maslow-hierachy-of-needs-min-1536x1086.jpg
 
Unaweza kuwa tajiri lakini huna mafanikio na unaweza kuwa umefanikiwa lakini huna utajiri.
Katika ngazi tano za Maslow za kufikia self-actualization, utajiri wa kiuchumi ni ngazi ya pili kutoka chini, maana yake ukimaliza utajiri kuna ngazi nyingine tatu za kupanda.


Sisi masikini tu ndio tunapapatikia utajiri.

Kuna mtu anaitwa Grigory Perelman, jamaa ni genius la mahesabu, yeye kwake mafanikio ni kutatua matatizo magumu ya hesabu.

Kati ya mwaka 202 na 2003 alikuja kutatua tatizo kubwa la hesabu linaitwa "Poincare's Conjecture", akapewa zawadi ya mamilioni ya US dollar, jamaa likakataa zwadi, likakataa kwenda kwenye tour ya lecture.

Yeye alichotaka ni ku solve hiyo mathematical challenge, hayo mambo yenu mengine ya hela na ujiko kukaa kwenye makamera alikwa hataki.

Na huyo naye kafanikiwa sana zaidi ya utajiri, kwa sababu ndiye mtu pekee aliyeweza ku solve Poincare's Conjecture, tatizo lililowashinda wanamahesabu wa dunia kwa miaka zaidi ya mia.

 
Back
Top Bottom