Naomba kujua namna ya kuhamia kufundisha vyuo vikuu, kutoka kuwa mwalimu wa sekondari

Naomba kujua namna ya kuhamia kufundisha vyuo vikuu, kutoka kuwa mwalimu wa sekondari

  1. Tambua chuo na program zinazotolewa kama zinaendana na masomo uliyosomea.
  2. Angalia unaomba kama nani?! Tutorial Assistant (ukiwa na Bachelor degree) au Assistant Lecturer (Masters degree) na kadhalika, bila kusahau vigezo vyake.
  3. Andika barua rasmi ya kiofisi kuulizia kama kuna nafasi ya kuhamia kwa cheo na eneo la utaalamu kwenye hicho chuo.
Kama mabosi wako sio wanoko, unaweza kuipitishia kwao kuongeza mkazo zaidi. Hili huwa ni lazima, japo unaweza kufanya kimya kimya.
Mara nyingi vyuo hutangaza nafasi za kuhamia pia. Hii ni nafasi nzuri zaidi, maana huelekeza hadi namna ya kuomba kuhamia, japo process sio ngumu.
  1. Baada ya kuandika barua ya kuulizia nafasi ya kuhamia, kaa utulie usubiri majibu. Utajibiwa kwa maandishi na utaratibu wote utapewa, lakini mara nyingi utaelekezwa kuandika barua rasmi ya kuomba kuhamia hiyo taasisi. Utaiaddress hii barua kwenda utumishi, ukiambatanisha barua uliyojibiwa na taasisi kua kuna nafasi ya kuhamia.
Barua hii lazima ipitie kwa mwajiri wako wa sasa, akipitisha kwa kukubali ombi lako, imeisha hiyo mzee.
  1. Hadi hapo, utasubiri tu barua ya uhamisho toka utumishi, halafu unaenda kureport kituo kipya cha kazi.
Kama kuna upungufu wowote katika maelezo yangu, wadau wataongezea kukupa mwongozo zaidi.
Uko sahihi kabisa , ila hapo namba 4 kwenye kupitishiwa na muajiri wako wa sasa ndo kwenye kimbembe, wengi hukwamishwa hapo
 
Mkuu vipi ulifanikiwa???
Kuna jirani yangu pia anataka hamia huko,!!
 
Naomba kuuliza ukifanya usahili vyuo vikuu alafu ni mwajiriwa WA halmashauri X barua ya uhamisho inapitia kwa mwajira wangu au?
 
hatuwataki nyie ndo mnakuja kutusumbua marks mnatukazia bila sababu na mademu mnawala.

hadi sahivi sijalala kisa vi lecturer uchwara pumbavu kabisa.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Hiyo ni undergraduate na masters ni 4.4
Khaaa, mtu una GPA tamu hivyo halafu unasotea mshahara wa TGS!!! Ebu ingia ajira portal jisajili huko ukapambane kwenye usahili nafasi zikitoka. Hilo nalo ni lakuelekezwa!! Tena kwa assistant lecturer competition huwa siyo kubwa kama tutorial assistant plus una experience in pedagogical field.
 
Khaaa, mtu una GPA tamu hivyo halafu unasotea mshahara wa TGS!!! Ebu ingia ajira portal jisajili huko ukapambane kwenye usahili nafasi zikitoka. Hilo nalo ni lakuelekezwa!! Tena kwa assistant lecturer competition huwa siyo kubwa kama tutorial assistant plus una experience in pedagogical field.
Ishu ni kupitishiwa barua
 
  1. Tambua chuo na program zinazotolewa kama zinaendana na masomo uliyosomea.
  2. Angalia unaomba kama nani?! Tutorial Assistant (ukiwa na Bachelor degree) au Assistant Lecturer (Masters degree) na kadhalika, bila kusahau vigezo vyake.
  3. Andika barua rasmi ya kiofisi kuulizia kama kuna nafasi ya kuhamia kwa cheo na eneo la utaalamu kwenye hicho chuo.
Kama mabosi wako sio wanoko, unaweza kuipitishia kwao kuongeza mkazo zaidi. Hili huwa ni lazima, japo unaweza kufanya kimya kimya.
Mara nyingi vyuo hutangaza nafasi za kuhamia pia. Hii ni nafasi nzuri zaidi, maana huelekeza hadi namna ya kuomba kuhamia, japo process sio ngumu.
  1. Baada ya kuandika barua ya kuulizia nafasi ya kuhamia, kaa utulie usubiri majibu. Utajibiwa kwa maandishi na utaratibu wote utapewa, lakini mara nyingi utaelekezwa kuandika barua rasmi ya kuomba kuhamia hiyo taasisi. Utaiaddress hii barua kwenda utumishi, ukiambatanisha barua uliyojibiwa na taasisi kua kuna nafasi ya kuhamia.
Barua hii lazima ipitie kwa mwajiri wako wa sasa, akipitisha kwa kukubali ombi lako, imeisha hiyo mzee.
  1. Hadi hapo, utasubiri tu barua ya uhamisho toka utumishi, halafu unaenda kureport kituo kipya cha kazi.
Kama kuna upungufu wowote katika maelezo yangu, wadau wataongezea kukupa mwongozo zaidi.
Mkuu vizuri umefafanua vyema sana, eti kama unataka kutuma barua kwa katibu mkuu utumishi ni vitu gani muhimu ambavyo unatakiwa uviambatanishe
 
hIvi kuna uwezekano taasisi unayoomba nafasi ikakuombea kibali utumishi cha uhamisho?
 
Back
Top Bottom