Naomba kujua Nyumba zinazonukia, Wanafanyaje?

Naomba kujua Nyumba zinazonukia, Wanafanyaje?

weka picha
wait mkuu nikipata pia kuna vidonge vya kuweka chini ya karpet ila ni kama zile za kwenye gari tu unaweka chini chini huko mvunguni zinaleta hewa nzuri tu ndani ila ufungue madirisha
 
Embu tuwekeeni mapicha mengi ya ma perfume ya kunukisha house. Mimi nipo gheto, napenda nili pimp ghetto langu likae poa ili nisiwe nalikimbia hasa siku za weekend. Embu tupieni madini ya kutosha
 
Aisee. ahsanteni sana ..hata mi nilitaka kuyajua haya.. ntanunua siku za mbeleni nikisha hamia kwangu.Mungu akipenda
 
interesting...
1477802352308.jpg
hii kitu ni hatari siijui hata jina ila nilinunuaga kwenye maduka ya waarabu k.koo! unaiwekea tu setting kila baada ya muda fulan inapiga kama chafya fulani hivii..hiyo harufu yake hapo ndan usipime..ni nzur haswaa...[emoji39]
Uje nikakununulie[emoji6] [emoji126]
 
Mie natumia automatic air fresher ambayo inatumia batteries, kama upo dsm waeza kwenda nakumat super market, game, au maisha supermarket.. Kama unanunua kwa mara ya kwanza utaipata kwa elfu 25 maximum price ambayo inajumuisha mashine na mkebe wake... Lakin mkebe ukiisha utalazimika kununua mkebe mwingne na kuuweka kwa mashine.. Kuna mkebe wa 5000 na kuna ya 12000 inategemea wataka wa kampuni gan ingawa mashine ni universal yakubali mikebe ya kampuni yoyote iliyokua designed for automatic air fresher.
 

Attachments

  • 1477820823429.jpg
    1477820823429.jpg
    63.8 KB · Views: 315
Nimezipenda hizo vitu hizo za kuchomeka kwny socket Nyani Ngabu
Nilikua natumia scented candles hofu ni kuunguza vitu ndani..japo ni nzuri sana kwa kweli
kando ya hapo air freshener, detergent za usafi,fabric softener ya pazia bado harufu nzuri inakua temporary,..
 
Maua kama muasumini,mkilua then ndan baada ya kusafisha unapulizia udi au unawasha candles zile zenye harufu
Hv kuna mti unaitwa muasumini au ni maua hayo..?kuna mti flani hvi jirani na chumbani basi usiku unatoa harufu nzuri sana...una maua ya njano hivi..siujui jina
 
Mimi kwangu huwa natumia air fresheners za kuchomeka kwenye soketi za umeme na ambazo ninaweza kudhibiti kiasi cha marashi yatokayo.

Baadaye nitaweka picha hapa muone nachozungumzia.

Jingine ni kutumia scented candles. Napendelea zaidi brand ya Yankee Candle.

Na huwa sipendi kupika vyakula vyenye shombo kali kama vile kukaanga samaki na kadhalika.

Nikikaanga samaki huwa nakaangia nje kwenye deck.

Halafu huwa napendelea zaidi marashi ya fresh na citrus.

Usafi wa nyumba nao husaidia pia. Hakikisha nyumba yako ni safi na yenye kuingiza na kutoa hewa vizuri.
Bila shaka wewe ni mhaya, mbwembwe nyiingi kumbe ni mbeba box.
 
Si unajua tena tunatofautiana kwenye mambo ya mnuso? Unaweza kuinusa kitu ukaona inanukia vizuri lkn ikawa kichefuchefu kwa mwenzako. Lakini maza alikuwa anapenda sana kampuni ya AIR WICK.

Zinanukia vizuri sana na zipo za aina tofauti.

Mkuu umesema "MNUSO" nikawa napata shida maana nikiwa mdogo nikienda kwenye sherehe nilikua nasema naenda kwny mnuso...
 
Mleta mada hapa umeokoa weng sanaa... nisaidien na marashi mazur ya kwny gari... yasiwe makali ya kuleta mafua
 
Wakuu, Ukiingia Mlimani City (hasa to pale kwenye corridor au pale Game) Ile harufu inayosikika pale wanatumia Airfresher brand ipi? Au wanafanyaje fanyaje ?
Naipenda sana ile harufu
 
View attachment 426414 hii kitu ni hatari siijui hata jina ila nilinunuaga kwenye maduka ya waarabu k.koo! unaiwekea tu setting kila baada ya muda fulan inapiga kama chafya fulani hivii..hiyo harufu yake hapo ndan usipime..ni nzur haswaa...[emoji39]
Uje nikakununulie[emoji6] [emoji126]
Bei gani mkuu
 
Back
Top Bottom