Naomba kujua Nyumba zinazonukia, Wanafanyaje?

Naomba kujua Nyumba zinazonukia, Wanafanyaje?

View attachment 426414 hii kitu ni hatari siijui hata jina ila nilinunuaga kwenye maduka ya waarabu k.koo! unaiwekea tu setting kila baada ya muda fulan inapiga kama chafya fulani hivii..hiyo harufu yake hapo ndan usipime..ni nzur haswaa...[emoji39]
Uje nikakununulie[emoji6] [emoji126]
location please
 
Mimi kwangu huwa natumia air fresheners za kuchomeka kwenye soketi za umeme na ambazo ninaweza kudhibiti kiasi cha marashi yatokayo.

Baadaye nitaweka picha hapa muone nachozungumzia.

Jingine ni kutumia scented candles. Napendelea zaidi brand ya Yankee Candle.

Na huwa sipendi kupika vyakula vyenye shombo kali kama vile kukaanga samaki na kadhalika.

Nikikaanga samaki huwa nakaangia nje kwenye deck.

Halafu huwa napendelea zaidi marashi ya fresh na citrus.

Usafi wa nyumba nao husaidia pia. Hakikisha nyumba yako ni safi na yenye kuingiza na kutoa hewa vizuri.
Ukipata mke mchafu sijui utamuacha? kwa usafi huo hatareeee.
 
Acha kabisa......nilitamani 'kuomba urafiki'
hahaa

nilifika hiyo nyumba for business only....ila ilivyokuwa inanukia nilitamani kujua zaidi kuhusu hilo
Na hao ndo kosa ungemsifia muhusika na ukamuuliza sidhani kama kuna ubaya kuuliza jambo katika kujifunza au kuiga.. ILA Kuna Aifrenshner kama walivyozungumzia walopita za kuspray kawaida na za ukutani, na candles kama aliwasha candles inawezekana zimechania..Japo wengine wamezoea Udi (Oud)...
 
Kwa jinsi nilivyo, kupata mke mchafu ni muhali!
Unafikiri tabia mbaya zinaanza kwenye uchumba? subiri ameolewa amezaa utakuta nguo chafu uvunguni .Wengi huwa hawaamini wake au watu wao wa karibu wamebadilika.Usafi ni mzuri ila ukizidi kila anakuyepitia unamuona mchafu ht mzazi wako utafika wakati utamuona kinyaa.
 
picha itasaidia
1478191974834.jpg


1478192072378.jpg


The Boss
 
Mi mwenyewe natamani ninukie kabla hata ya nyumba kunukia maana kuna thread moja ya maperfume ya maana niliionaga humu mpaka nikachanganyikiwa nitafute ipi

Sasa hii ya nyumba ndo nasikia leo
 
View attachment 426414 hii kitu ni hatari siijui hata jina ila nilinunuaga kwenye maduka ya waarabu k.koo! unaiwekea tu setting kila baada ya muda fulan inapiga kama chafya fulani hivii..hiyo harufu yake hapo ndan usipime..ni nzur haswaa...[emoji39]
Uje nikakununulie[emoji6] [emoji126]
Bei yake?
 
Back
Top Bottom