Naomba Kujua Pombe ni Dhambi au ni haramu? Imekatazwa na Quran au Mtume Mohamed?

Naomba Kujua Pombe ni Dhambi au ni haramu? Imekatazwa na Quran au Mtume Mohamed?

Allah anasema wenye hekima wanajua utamu wa pombe


Koran 16:67 And from the fruits of date palms and grapes, you derive strong drink and a goodly provision. There is indeed a sign in this for those of reason
 
Asante,
Kwanza kabisa tujue misamiati haramu na dhambi, pili tujue pombe, kisha tatu tujue Mtume Muhammad (hadithi) na Quran halafu mwishoni kabisa tumalize kwa kujibu swali lako. Nitatumia tafsiri zisizo rasmi ili niweze kueleweka kirahisi kwa baadhi ya vipengele ila maana ni ileile sitatoka nje ya Sheria ya dini ya kiislam

Haramu
Haramu ni jambo ambalo limekuwa prohibited kwa muumini, yaani amepigwa marufuku kulitenda na akikengeuka basi anakuwa amemkosea Muumba na itamletea madhara yeye (wakati mwingine na jamii yake) duniani na baada ya kufa. Haramu ni mambo mabaya na maovu

Dhambi
Dhambi ni chumo analopata mtu kwa kumkosea Mola wake, yaani ukitenda haramu malipo yake ni dhambi kama ilivyo kwa anayetenda halali (mambo mema na mazuri) malipo yake yakawa ni thawabu. Ikumbukwe uislamu una hukumu kuu Tano na katika hizo, mbili maarufu ni HALALI na HARAMU ambapo ukifanya halali utapata thawabu na ukifanya haramu utapata dhambi

Pombe au ulevi kwenye uislamu ni Kila chenye kuharibu akili na hapa naomba ieleweke kwamba kuharibu siyo kusambaratisha maana wapo wanaojisifu kwamba wanakunywa lakini wanajitambua hivyo pombe Haina shida kwa upande wao, sub'hanaallah! Kuharibu akili ni kufanya mtu awe tofauti na kawaida yake mfano kutembea, kuongea, utendaji, nk

Mtume Muhammad ni mtu ambae alipewa ujumbe wa kuwafikishia binadamu kama ilivyo kwa binadamu waliotangulia kabla ya kizazi chake ambapo walikuwa wakichaguliwa watu miongoni mwao na kupewa maelekezo maalumu ya namna ya kuishi

Kama ilivyokuwa kwa watu (mitume) wengine, Mtume Muhammad nae alipewa muongozo maalumu wa maisha kwajili ya kuufuata yeye na watu wa kizazi chake. Mwongozo huo ndio unaofahamika kama QURAN

Swala likaja sasa kwenye kuuelewa na kuutekeleza huo mwongozo ambapo Mtume Muhammad akawa akilazimika kutafsiri na kuchambua kinaganaga maneno yaliyotumika kwenye huo mwongozo ili kuwarahisishia watu katika utekelezaji wake (hii ilitokana na kwamba kuna mambo mengine yaliyohitaji vitendo zaidi pia mengine yalikuwa ni misamiati mipya katika lughat waliyozoea kuitumia)

Uchambuzi huo na utekelezaji wake aliokuwa akiudemonstrate Mtume Muhammad ndo unajulikana kama mwenendo wa Mtume yaani Sunnah na hadithi. Kwahiyo mtu hawezi kutenganisha suna ya Mtume na maneno ya MwenyeziMungu (Quran na hadithi) kwani hadithi ni mwenendo au utekelezaji wa Quran yenyewe

Majibu ya swali lako
Pombe imekatazwa katika mwongozo wa Quran soma sura ya Tano Aya ya 90 hadi 91. Mwongozo huu haukuacha kitu pia ukatoa na sababu za kuharamisha/kuzuia pombe>>> rejea surah Al baqara Aya ya 219 na surah Al Maida Aya ya 93. Ikumbukwe kwamba haramu au halali zipo ambazo unapewa direct madhara au faida zake, zingine hupati bali unadokezwa tu ili kwa mwenye kuweza kutafiti akatafiti kupata majibu na zingine zipo kwa mkato tu kwamba ni haramu au halali ila utafiti au ukweli wake utauona ukishakufa huko

MwenyeziMungu ndiye mjuzi zaidi
 
majibu yako kwa huyu jamaa hapo chini
1.jpg
 
Pombe sio haramu na wala si dhambi kutumika. Matumizi ya pombe kupita kiasi ndio yanayopelekea kukiuka kanuni za maisha.
Kila chakula au kinywaji kilichoko ndani ya mamlaka ya binadamu kikitumika kwa kiasi ni halali hadi pale tunapovuka mipaka.
Kwa mujibu wa imani ipi?
 
Pombe haijawahi kuwa dhambi, au haram! Ila matendo mabaya yatokanayo na hiyo pombe sasa, ndiyo yatampeleka mtu kutenda dhambi! Na hivyo mwisho wa siku kuchukuliwa kama haram.

Haya basi kila mmoja huru kupiga gambe ila asifanye hayo matendo...hehehe

screenshot_20230422-193635-jpg.2596519
 
Mm mpk Leo nilikua najua pombe sio Dhambi....
Ila ukiwa umelewa je? Wachawi, majini na mapepo yanaweza kukuvaa wakati ukilewa ni najisi.....??

Wadau karibuni...
 
Wadau hamjamboni nyote?

Kwa heshima kubwa naombeni mnipatie majibu kupitia vyanzo sahihi kwa kuzingatia kichwa cha habari.

Je Pombe ni dhambi au ni haramu?
Je Pombe imekatazwa na Quran tukufu ama Mtume Mohamed?

Kashfa ya aina yeyote nitaomba Moderator afute Uzi huu

Aksante Niwatakie Jumapili njema
Kuna mito ya pombe akhera. Kula beer, usiumize roho yako, muhimu kiasi. Tumbo halina dini.
 
Back
Top Bottom