Naomba kujulishwa kuhusu biashara ya kuuza furniture za majumbani

Upepo wa Pesa

JF-Expert Member
Joined
Aug 8, 2015
Posts
21,600
Reaction score
35,158
Habari wana JF!!

Nimekua na hili wazo mda kidogo yaani kifungua duka la kuuza samani za ndani kama meza, makochi, viti,vitanda,mashuka na mengine kama hayo.

Kwa wenye uzoefu tafadhali naomba mawazo yenu hasa katika:

1.Mtaji.
2.Kodi.
3.Sehemu nzuri za kuagiza mzigo na
mbinu za kufanikiwa katika hii biashara!!

Niliplan nianze kuagiza mzigo na kuuweka home alafu nianze kuuza kwenye mitandao kama facebook na instagram alafu badae nichukue room...

Pia nilitaka nifungue ofisi Arusha, Moshi au Dsm!! (hasa arusha)...

Nakaribisha mawazo yenu wakuu!!
 
Nimekupata mkuu ila juzi juzi mahindi yalishuka sana na watu wa mtwara na lindi wanajua kilichowakuta kwenye bei ya korosho...

Nashukuru kwa mchango wako!!
Mimi ni mtu niliepata hasara ya mahindi kutokana na siasa za mwaka jana.


Hapo nilikuwa namaanisha kuuza restaurant ya chakula. Kwa sasa kilimo siwezi lima ila ni mwendo wa kununua nafaka basi hapo lazima upige hela
 
Biashara ya furniture zama zake zimekwisha mkuu, in this time of economic difficult watu wanaspend their money more wisely...its only kwenye basic needs pekee and not otherwise.

Endelea kusumbua akili kutafuta biashara nyingine yenye circulation nzuri maana hata hii ya furniture circulation yake bado ni hafifu sana as people don't always buy furniture. Na kwenye biashara lilia mzunguko na si kingine ndio maana richest businessman in Tanzania hawafanyi biashara za Kariba unayotaka kufanya.

Endelea kufikiri kwa kina tena uje na brilliant idea but kwa hii ya furniture...Mimi kwangu sikuungi mkono.
 
Mimi ni mtu niliepata hasara ya mahindi kutokana na siasa za mwaka jana.


Hapo nilikuwa namaanisha kuuza restaurant ya chakula. Kwa sasa kilimo siwezi lima ila ni mwendo wa kununua nafaka basi hapo lazima upige hela
Nimekupata mkuu... Thanks once again!!
 
kaka biashara ya furniture hailipi kwa sasa,watu wengi kwa sasa wananunua furniture used tu kwenye mitandao ya kijamii hasa instagram
 
Una mawazo mazuri sana, shukran mkuu
 
kaka biashara ya furniture hailipi kwa sasa,watu wengi kwa sasa wananunua furniture used tu kwenye mitandao ya kijamii hasa instagram
Nlikua nawaza vitu kama vitanda, meza, viti na mashuka... Alafu niuze kwa bei ya chin kidogo mkuu... Sintatoboa??
 
Nlikua nawaza vitu kama vitanda, meza, viti na mashuka... Alafu niuze kwa bei ya chin kidogo mkuu... Sintatoboa??
hakuna biashara inayolipa kwa sasa kama chakula,japo hali za watu ni mbaya lakini kila siku lazima watafute chochote kwa ajili ya chakula,siku hizi kuvaa na hata kuwa na furniture nzuri imekuwa kama anasa kutokana na hali ya uchumi
 
hakuna biashara inayolipa kwa sasa kama chakula,japo hali za watu ni mbaya lakini kila siku lazima watafute chochote kwa ajili ya chakula,siku hizi kuvaa na hata kuwa na furniture nzuri imekuwa kama anasa kutokana na hali ya uchumi
Nashukuru sana mkuu kwa mawazo yako!!
 
Barbershop vp?
You can't be serious... Barbershop ni biashara za kutafutia hela ya kula tu mkuu....katika maisha unahitaji kufikiri biashara ambazo ni game changer...ukitaka kufanikiwa katika maisha lazma ufikiri kama akina MO au Bakheresa. They think big..sio ishu za vibabashop hivyo wanawaachia akina Nyandu tozi wanyoane viduku.

Think big, start small.
 
Kama hutakuwa tegemezi kwa biashara hiyo fungua! Vilevile ili kupunguza gharama za bidhaa ni vema ununue malighafi kisha umkodi fundi akufanyie kazi.
 
Kama hutakuwa tegemezi kwa biashara hiyo fungua! Vilevile ili kupunguza gharama za bidhaa ni vema ununue malighafi kisha umkodi fundi akufanyie kazi.
Nashukuru sana mkuu... Nlipanga mzigo mwingi niagize kutoka nje...dubai na china then nije niuze hapa kwetu... Na Sio kutengeneza mwenyewe... Japo nnaweza kufanya hivyo badae!!
 
Mkuu vipi biashara ya chakula, restaurant ukipata sehemu nzuri na wapishi wazuri unatoboa...kingine usidharau faida ndogo, fungua biashara ndogo kisha multiply it...hata kama net faida ni 30k kwa siku ukiwa nazo 5,6..10 si haba
Nashukuru kwa mawazo yako mkuu
 
Nashukuru sana mkuu... Nlipanga mzigo mwingi niagize kutoka nje...dubai na china then nije niuze hapa kwetu... Na Sio kutengeneza mwenyewe... Japo nnaweza kufanya hivyo badae!!
Kumbe uagize mzigo kutoka nje,unafikiri ni watanzania wangap wataaford bei?,mm kwa ushaur wangu nakubaliana na huyo jamaa hapo juu aliekushauri uwe unanunua malighafi mwenyewe then utafute mafundi wawe wanakutolea vitu vya shoppers Kama Dubai

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…