Naomba kujuzwa Engine Oil na Gear Box Oil nzuri kwa gari ndogo aina ya Honda Fit

Vipi kwa mfano Toyota ie (Toyota Tanzania) wana oil zao zimeandikwa TOYOTA vipi nazo zinafaa?
 
Vipi kwa mfano Toyota ie (Toyota Tanzania) wana oil zao zimeandikwa TOYOTA vipi nazo zinafaa?
Ni very high quality hata bei yake ni kubwa mkuu. Zinafaa ila kama kawaida lazima ujue grade ya oil yako
 
Samahan mkuu iv WS ni nin
 
Yes,au we unasemaje?

Naona 5w30 Inaweza kutumika hadi 35 degrees. Ila kwa hapa Dar kipima joto kinaweza kusoma 32deg lakini real feel ikawa hata zaidi ya 35deg. So kuwa safe ni kutumia 5W40. Ni mtazamo wangu lakini kufuatana na hiyo chart ya viscocity hapo chini.

 
Mkuu, 5w30 ni 50+ degree za sentigredi. Dar imewahi kufika nyuzi joto hiyo lini? Pia oil viscosity ni zaidi ya joto kuna factors nyingine, ndio maana oil ya Scania Kwa mazingira hayo hayo ya DSM inayo viscosity yake. Someni Manual za magari yenu mkuu.
 
Angalia kwenye oils viscicity chart hapo juu. Mwisho wa 5w30 ni 35 degrees!
Mkuu hata hivyo dar haijawahi kufika 35 degree na pia hata Dubai wanatumia hiyo na joto lake hufika 40 degree. Mkuu kikubwa nachotaka kusema ni kuwa oil viscosity ni zaidi ya joto, karibu kila engine joto lake huwa zaidi kuliko joto la nje.
 
Mkuu hata hivyo dar haijawahi kufika 35 degree na pia hata Dubai wanatumia hiyo na joto lake hufika 40 degree. Mkuu kikubwa nachotaka kusema ni kuwa oil viscosity ni zaidi ya joto, karibu kila engine joto lake huwa zaidi kuliko joto la nje.

Joto linaloangaliwa sio la engine wewe🤣. Ni la nje. Kwa Dar joto linaweza kuwa linasoma 32 deg lakini real feel ikawa hata 38 deg. Normal engine operating temperature ni btn 90deg an 104deg. (kama mtu kachomoa thermostart haitakaa ifike hapo kwenye hiyo range.
 
Nimeelewa vyema sana mkuu, ninachosema kama oil inafanya kazi kwenye engine yenye joto la 100 inakuwaje isifae kwenye sorrounding temperature ya 40?

Kikubwa ninachosema ni kuwa Manual ya gari inaeleza vizuri oil grade ipi itafaa kwa gari lako. Mimi binafsi naweka oil kwa kusoma Manual ya gari na sio maelekezo ya fundi ama mtu
 

Labda tuwaulize watengenezaji ni kwa nini wameweka specs za oil kwa style hiyo. Kwenye manual za magari huwa wanaweka viscocity charts pia ambayo inakuonyesha uweke oil gani kwa mazingira yapi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…