Naomba kupata elimu kuhusu ufugaji wa kuku wa kienyeji

Naomba kupata elimu kuhusu ufugaji wa kuku wa kienyeji

Kuku wa kienyeji Hana magonjwa au ha athiriki sana na magonjwa kama Hawa wa kisasa

Cha kufanya zingatia chanjo zote na Kwa muda sahihi.

Wape chakula sahihi na chenye virutubisho.

Usafi Kila inapohitajika

Wafuge nusu huria na

Panda miti ya madawa yao ya kienyeji

Mfano usikose hii miti

Mipapai
Mwaribaini
Mlonge
Alobera
Pilipili kichaa hii itakusaidia wewe na kuku wako pia.


Mwisho Mungu awe nawe katika jitihada zako.
 
Kabla hatujafika kwenye chamgamoto

Jambo la kwanza ikiwa utawafuga kibiashara. Hakikisha CHAKULA cha hao kuku kipo na kiwe cha bei nzuri au uzalishe wewe mwenyewe.

Chakula ni 70%ya gharama na lishe duni ni chanzo cha magonjwa na tabia mbaya kama kudonoana, kuvimba macho, etc Weka stock ya kutosha.

Jambo la pili, BANDA. Liwe imara kuzuia mapanya, wanyama waharibifu kama vicheche, nk.

Tatu, weka GHARAMA za mtaalamu. Kubali kulipia na kutembelewa na mataalamu ambaye anaweza kukushauri mengi. Hii fanya kabla hujaanza chochote.
Ikiwa eneo ulilopo hakuna mtaalamu tafuta mfugaji mkubwa kamtembelee jifunze
 
Nahitaji kufuga kuku wa kienyeji lakini nahitaji kujua changamoto ambazo huwa zinajitokeza na namna ya kuziepuka.
Kiukweli hii biashara wengi huiponda, lakini nimefanya utafiti sana, inalipa lakini ukubali kufuga kisasa! Kwanza upate elimu, uwajue vizuri, mbinu za kuwazalisha kwa muda mfupi, magonjwa, chakula, changamoto yao kubwa hawa ni kukua, wanakua taratibu, so lazima ujue kubalance chakula, ili wakue haraka na wewe upate faida, so ujifunze chakula mbadala, Azola, funza, lakini pia kuna sehemu niliona, kuku wa siku moja, analishwa stata mpaka afike mwezi, analishwa usiku na mchana, kisha wanaanza kulishwa kawaida, lakini pia hawa kuku hawataki kufungiwa ndani hawa wanapenda huria, so unakuwa na wavu unazungushia ili wawe huria ndani ya uzio, chanjo, chanjo,chanjo! Hapo usipitishe hata moja tena! Chanjo wapewe kwa wakati! Vitamins na dawa za mafua ziwepo muda wote. Banda lizingatie vigezo vyote, ukubwa kulingana na kuku ulionaao, Soko lipo la kutosha tu.
 
Kuku wa kienyeji Hana magonjwa au ha athiriki sana na magonjwa kama Hawa wa kisasa

Cha kufanya zingatia chanjo zote na Kwa muda sahihi.

Wape chakula sahihi na chenye virutubisho.

Usafi Kila inapohitajika

Wafuge nusu huria na

Panda miti ya madawa yao ya kienyeji

Mfano usikose hii miti

Mipapai
Mwaribaini
Mlonge
Alobera
Pilipili kichaa hii itakusaidia wewe na kuku wako pia.


Mwisho Mungu awe nawe katika jitihada zako.
asante sana mkuu
 
Naona wenzangu wametoa mchango mzuri hapo juu,La msingi ni usafi(Jitahidi sana tena sana mazingira yawe masafi iwe unapowafugia au mazingira yakuzurura )
~Jitahidi uwe kichaa ..yaani usitegemee sana madawa madawa uwe unawapa na vitu vingine vya asili kama booster mfano majani makavu,majani ya mbogamboga,Migomba hapa wakishafika umri wa kujitegemea yaani chochote kizuri cha asili weka nyanya,alovera n.k

La mwisho na la msingi ni kuwa mfuatiliaji wa mwenendo wa kuku wako mfano unaona kuna magonjwa kama minyoo,kikohozi haraka unawapatia tiba stahili
 
Back
Top Bottom